Machinga wapinga agizo la RC Dar kuzuia uuzwaji wa Filamu za nje ya nchi, Waandamana

boyskillz

Senior Member
Apr 29, 2013
109
104


Nimesikia kwenye vyombo vya habari kuwa mkuu wa mkoa wa Dar amezuia biashara ya Kuuza DVD zenye picha mnato (movies) zá nje ya nchi, mfano zile za kikorea, kihindi, kifilipino nk.

Nilichunguza lengo la yeye kufanya vile nikatambua kuwa anafikiri hio Ndiyo njia itakayosaidia waigizaji wa muvi za nyumbani maarufu kama bongo movie kuuza zao.

Ningependa kumshauri bure tu, kitendo hiki kamwe sio suluhisho la kumsaidia msanii wa nyumbani. Bali kinaweza kusababisha mtafaruku wa kiuchumi kwa wale watanzania waliokuwa wamekwisha kujiajiri katika biashara hii, mfano wale walioweka sauti ndani ya Hizo muvi kwa lengo la kutafsiri na pia kitendo hiki kitakua fimbo ya kiuchumi kwa wale wanaoziuza mitaani kwani ndio biashara inayowaweka mjini.

Jambo la kwanza nafikiri Mheshimiwa huyu angejiuliza kwanini watanzania wengi wanapendelea hizo muvi za nje, hapo angeweza kuona kwamba pengine muvi za nje zina ubora (HD), ama pengine zina stori tamu nk. Na kama hayo yakiwa Ndiyo majibu basi angeyapeleka kwao Bongo Movie kama changamoto ili kesho na wao waweze kupambana ili kufikia hatua hiyo ya kununulika zaidi sokoni.

Naweza toa mifano ya sinema kama za Merlin, 24legacy na Jumong, hizi ni lazima zizidi kimauzo sokoni ukilinganisha na zile za akina Hemed PHD, na hili halipingiki. Vile vile watazamaji wanatofautiana kwenye interest zao, unakuta huyu anapenda za Hollywood, yule Bollywood na huyo Bongo Movie. Sasa kwa mawazo ya kudhania kuzitoa Hizo zingine sokoni zibaki Bongo Movie Pekee ndio kuisaidia tasnia hii ni kujidanganya, mfano kuna rafiki yangu mmoja yeye ukimwambia muvi moja kwa moja mawazo yake Anajua ni ya kikorea akikuta sio anaachana nayo hapo hapo.

Kama mheshimiwa angetaka kuwasaidia hawa bongo movie basi angeangalia namna ya kuzilinda kazi zao zisiibiwe ama kunakiriwa na maharamia (piracy) wa muvi ili kuhakikisha wananufaika vilivyo na kazi zao. Na pia angetafuta hata njia ya kuwapunguzia kodi ili wasibanwe na adha za sokoni.

Lakini kwa hatua hii aliyochukua hapo naweza kusema amechemka, maana anakwenda kudidimiza uchumi wa yule machinga anayelisha familia yake kwa biashara hii. Na uchumi wa hawa wanyonge ukianguka hata pato la taifa litapungua kwa asilimia flani kwasababu hawa machinga mfano waliopo soko la mwenge ama kariakoo wanalipa ushuru wa meza ama kodi ya pango.

Kama kuna washauri wa washauri wake naomba wakafikishe ujumbe huu kwake na wakatafute njia nyingine ya kuwasaidia hawa wasanii maana hii haina msaada wowote ule na badala yake inaleta tatizo lingine mtaani.

Na Enock Ally Skills
---------
Heshima kwenu,

Mara baada ya uteuzi, Waziri wa Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo wakati huo Mh. Nape Nnauye, alipanga kuwafurahisha Bongo Movies. Alipita Kariakoo na kukamata CD zilizoitwa feki, zisizokuwa na muhuri/stamp ya TRA. Ilikuwa sahihi.

Baadaye akatoa maagizo kuwa CD za nje hazitakiwi kuuzwa, ziuzwe za Bongo tu, lengo ni kusaidia wasanii wa ndani. Zoezi hill liliambatana na kukamata CD zote za nje.

Msambazaji mkuu wa CD hizo kutoka China, mwenye duka na stop anayeuza kutoka Hotel ya Butterfly, alisombewa mzigo wote, akafunga duka, hakurudishiwa kitu. Maofisa wa wizara ya Nape walikuja tena na kukamata CD kwenye duka hill na kuwaambia wauzaji waweke stamp za TRA wakawaambia haiwezekani kwa kuwa mzigo unatoka China moja kwa moja. Wakalazimishwa waingie mkataba na watengenezaji.

Leo hii kulikuwa na zogo Kariakoo na wauza CD walifunga maduka juu ya suala hilo hilo. Ijulikane kuwa so watu wote hupenda Bongo Muvie kwa kuwa hazina quality kama za nje. Kulazimisha watu wanunue kitu wasichokipenda kwenye karne hii ni makosa.

Serikali inavunja sheria kufanya hivi. Wananyima umma haki yao na wanawatia hasara watu waliowekeza kwenye biashara hiyo. Biashara ya CD sio ya viroba. Sababu nyingine zitolewazo na wizara hazina mashiko.

Tuchangie
 
.

Nimesikia kwenye vyombo vya habari kuwa mkuu wa mkoa wa Dar amezuia biashara ya Kuuza DVD zenye picha mnato (movies) zá nje ya nchi, mfano zile za kikorea, kihindi, kifilipino nk.

Nilichunguza lengo la yeye kufanya vile nikatambua kuwa anafikiri hio Ndiyo njia itakayosaidia waigizaji wa muvi za nyumbani maarufu kama bongo movie kuuza zao.

Ningependa kumshauri bure tu, kitendo hiki kamwe sio suluhisho la kumsaidia msanii wa nyumbani. Bali kinaweza kusababisha mtafaruku wa kiuchumi kwa wale watanzania waliokuwa wamekwisha kujiajiri katika biashara hii, mfano wale walioweka sauti ndani ya Hizo muvi kwa lengo la kutafsiri na pia kitendo hiki kitakua fimbo ya kiuchumi kwa wale wanaoziuza mitaani kwani ndio biashara inayowaweka mjini.

Jambo la kwanza nafikiri Mheshimiwa huyu angejiuliza kwanini watanzania wengi wanapendelea hizo muvi za nje, hapo angeweza kuona kwamba pengine muvi za nje zina ubora (HD), ama pengine zina stori tamu nk. Na kama hayo yakiwa Ndiyo majibu basi angeyapeleka kwao Bongo Movie kama changamoto ili kesho na wao waweze kupambana ili kufikia hatua hiyo ya kununulika zaidi sokoni.

Naweza toa mifano ya sinema kama za Merlin, 24legacy na Jumong, hizi ni lazima zizidi kimauzo sokoni ukilinganisha na zile za akina Hemed PHD, na hili halipingiki. Vile vile watazamaji wanatofautiana kwenye interest zao, unakuta huyu anapenda za Hollywood, yule Bollywood na huyo Bongo Movie. Sasa kwa mawazo ya kudhania kuzitoa Hizo zingine sokoni zibaki Bongo Movie Pekee ndio kuisaidia tasnia hii ni kujidanganya, mfano kuna rafiki yangu mmoja yeye ukimwambia muvi moja kwa moja mawazo yake Anajua ni ya kikorea akikuta sio anaachana nayo hapo hapo.

Kama mheshimiwa angetaka kuwasaidia hawa bongo movie basi angeangalia namna ya kuzilinda kazi zao zisiibiwe ama kunakiriwa na maharamia (piracy) wa muvi ili kuhakikisha wananufaika vilivyo na kazi zao. Na pia angetafuta hata njia ya kuwapunguzia kodi ili wasibanwe na adha za sokoni.

Lakini kwa hatua hii aliyochukua hapo naweza kusema amechemka, maana anakwenda kudidimiza uchumi wa yule machinga anayelisha familia yake kwa biashara hii. Na uchumi wa hawa wanyonge ukianguka hata pato la taifa litapungua kwa asilimia flani kwasababu hawa machinga mfano waliopo soko la mwenge ama kariakoo wanalipa ushuru wa meza ama kodi ya pango.

Kama kuna washauri wa washauri wake naomba wakafikishe ujumbe huu kwake na wakatafute njia nyingine ya kuwasaidia hawa wasanii maana hii haina msaada wowote ule na badala yake inaleta tatizo lingine mtaani.

Na Enock Ally Skills
Kusema la ukweli kutoka moyoni katika vitu au movie ambazo nikiangalia usingizi unakuja hapo hapo ni hizi za kibongo yaani movie inaanza ushajua mwisho wake nyingine zinaisha unaona kabisa nje ya box hii ingetakiwa iendelee
 
.

Nimesikia kwenye vyombo vya habari kuwa mkuu wa mkoa wa Dar amezuia biashara ya Kuuza DVD zenye picha mnato (movies) zá nje ya nchi, mfano zile za kikorea, kihindi, kifilipino nk.

Nilichunguza lengo la yeye kufanya vile nikatambua kuwa anafikiri hio Ndiyo njia itakayosaidia waigizaji wa muvi za nyumbani maarufu kama bongo movie kuuza zao.

Ningependa kumshauri bure tu, kitendo hiki kamwe sio suluhisho la kumsaidia msanii wa nyumbani. Bali kinaweza kusababisha mtafaruku wa kiuchumi kwa wale watanzania waliokuwa wamekwisha kujiajiri katika biashara hii, mfano wale walioweka sauti ndani ya Hizo muvi kwa lengo la kutafsiri na pia kitendo hiki kitakua fimbo ya kiuchumi kwa wale wanaoziuza mitaani kwani ndio biashara inayowaweka mjini.

Jambo la kwanza nafikiri Mheshimiwa huyu angejiuliza kwanini watanzania wengi wanapendelea hizo muvi za nje, hapo angeweza kuona kwamba pengine muvi za nje zina ubora (HD), ama pengine zina stori tamu nk. Na kama hayo yakiwa Ndiyo majibu basi angeyapeleka kwao Bongo Movie kama changamoto ili kesho na wao waweze kupambana ili kufikia hatua hiyo ya kununulika zaidi sokoni.

Naweza toa mifano ya sinema kama za Merlin, 24legacy na Jumong, hizi ni lazima zizidi kimauzo sokoni ukilinganisha na zile za akina Hemed PHD, na hili halipingiki. Vile vile watazamaji wanatofautiana kwenye interest zao, unakuta huyu anapenda za Hollywood, yule Bollywood na huyo Bongo Movie. Sasa kwa mawazo ya kudhania kuzitoa Hizo zingine sokoni zibaki Bongo Movie Pekee ndio kuisaidia tasnia hii ni kujidanganya, mfano kuna rafiki yangu mmoja yeye ukimwambia muvi moja kwa moja mawazo yake Anajua ni ya kikorea akikuta sio anaachana nayo hapo hapo.

Kama mheshimiwa angetaka kuwasaidia hawa bongo movie basi angeangalia namna ya kuzilinda kazi zao zisiibiwe ama kunakiriwa na maharamia (piracy) wa muvi ili kuhakikisha wananufaika vilivyo na kazi zao. Na pia angetafuta hata njia ya kuwapunguzia kodi ili wasibanwe na adha za sokoni.

Lakini kwa hatua hii aliyochukua hapo naweza kusema amechemka, maana anakwenda kudidimiza uchumi wa yule machinga anayelisha familia yake kwa biashara hii. Na uchumi wa hawa wanyonge ukianguka hata pato la taifa litapungua kwa asilimia flani kwasababu hawa machinga mfano waliopo soko la mwenge ama kariakoo wanalipa ushuru wa meza ama kodi ya pango.

Kama kuna washauri wa washauri wake naomba wakafikishe ujumbe huu kwake na wakatafute njia nyingine ya kuwasaidia hawa wasanii maana hii haina msaada wowote ule na badala yake inaleta tatizo lingine mtaani.

Na Enock Ally Skills
Hili umemsingizia hili swala la movie za nje ilizuiwa na Nape akiwa waziri jaribu kuwa mfatiliaji kwanza
 
Ameteleza kivipi!?

Acheni kudandia hayo yana mengi sana hata juu ya kodi na kuiba kazi za watu kusambaza bila kibali.

Wakitaka wamuombe wakae nae chini awasikilize, na sio kufanya maandamano sijui kupiga kelele mtaani kila kona huku wananajua kuwa wana makosa tele tele na wanavunja sheria.

Afanye biashara inavyotakiwa.


Hapa kazi tu
 
Ameteleza kivipi!?

Acheni kudandia hayo yana mengi sana hata juu ya kodi na kuiba kazi za watu kusambaza bila kibali.

Wakitaka wamuombe wakae nae chini awasikilize, na sio kufanya maandamano sijui kupiga kelele mtaani kila kona huku wananajua kuwa wana makosa tele tele na wanavunja sheria.

Afanye biashara inavyotakiwa.


Hapa kazi tu
Kizuri cha jiuza chenyewe.
 
.

Nimesikia kwenye vyombo vya habari kuwa mkuu wa mkoa wa Dar amezuia biashara ya Kuuza DVD zenye picha mnato (movies) zá nje ya nchi, mfano zile za kikorea, kihindi, kifilipino nk.

Nilichunguza lengo la yeye kufanya vile nikatambua kuwa anafikiri hio Ndiyo njia itakayosaidia waigizaji wa muvi za nyumbani maarufu kama bongo movie kuuza zao.

Ningependa kumshauri bure tu, kitendo hiki kamwe sio suluhisho la kumsaidia msanii wa nyumbani. Bali kinaweza kusababisha mtafaruku wa kiuchumi kwa wale watanzania waliokuwa wamekwisha kujiajiri katika biashara hii, mfano wale walioweka sauti ndani ya Hizo muvi kwa lengo la kutafsiri na pia kitendo hiki kitakua fimbo ya kiuchumi kwa wale wanaoziuza mitaani kwani ndio biashara inayowaweka mjini.

Jambo la kwanza nafikiri Mheshimiwa huyu angejiuliza kwanini watanzania wengi wanapendelea hizo muvi za nje, hapo angeweza kuona kwamba pengine muvi za nje zina ubora (HD), ama pengine zina stori tamu nk. Na kama hayo yakiwa Ndiyo majibu basi angeyapeleka kwao Bongo Movie kama changamoto ili kesho na wao waweze kupambana ili kufikia hatua hiyo ya kununulika zaidi sokoni.

Naweza toa mifano ya sinema kama za Merlin, 24legacy na Jumong, hizi ni lazima zizidi kimauzo sokoni ukilinganisha na zile za akina Hemed PHD, na hili halipingiki. Vile vile watazamaji wanatofautiana kwenye interest zao, unakuta huyu anapenda za Hollywood, yule Bollywood na huyo Bongo Movie. Sasa kwa mawazo ya kudhania kuzitoa Hizo zingine sokoni zibaki Bongo Movie Pekee ndio kuisaidia tasnia hii ni kujidanganya, mfano kuna rafiki yangu mmoja yeye ukimwambia muvi moja kwa moja mawazo yake Anajua ni ya kikorea akikuta sio anaachana nayo hapo hapo.

Kama mheshimiwa angetaka kuwasaidia hawa bongo movie basi angeangalia namna ya kuzilinda kazi zao zisiibiwe ama kunakiriwa na maharamia (piracy) wa muvi ili kuhakikisha wananufaika vilivyo na kazi zao. Na pia angetafuta hata njia ya kuwapunguzia kodi ili wasibanwe na adha za sokoni.

Lakini kwa hatua hii aliyochukua hapo naweza kusema amechemka, maana anakwenda kudidimiza uchumi wa yule machinga anayelisha familia yake kwa biashara hii. Na uchumi wa hawa wanyonge ukianguka hata pato la taifa litapungua kwa asilimia flani kwasababu hawa machinga mfano waliopo soko la mwenge ama kariakoo wanalipa ushuru wa meza ama kodi ya pango.

Kama kuna washauri wa washauri wake naomba wakafikishe ujumbe huu kwake na wakatafute njia nyingine ya kuwasaidia hawa wasanii maana hii haina msaada wowote ule na badala yake inaleta tatizo lingine mtaani.

Na Enock Ally Skills
Kwanza hii issue haipo chini ya mamlaka yake sisi tumeingia kwenye free trade hili linatakiwa liwe addressed na mawaziri husika to mean waziri wa viwanda na biashara pamoja na waziri wa habari, utamaduni na. ... sio kazi ya mkuu wa mkoa
 
Sijawahi kujua bongo Movies huwa zinafundisha nini? Huu ni ulimwengu mpya ambao mipaka haina thamani sana hasa juu ya vitu! Nunua original bongo Movies ukiangalia Mara tatu inagoma! Kijana hajui umuhimu wa elimu! Tanzania nakupenda kwa moyo wote!!
 
Huu ni mpango ulikuwepo muda mrefu kabla ya makonda yeye kasimamia tu. Kimsingi hawajakatazwa bali wametakiwa wafuate taratibu zinazotakiwa ambazo ni kuwa ni kibali cha kampuni iliyotoa sinema husika na kulipia kodi nakala zote ambazo zitakuwa kwenye makubaliano. Kinachofanywa na wafanyabiashara wa movie za nje ni piracy kwa sab piracy sio lazima ziwe za ndani kuruhusu kuuzwa piracy nchini ni kukiuka mikataba ya kimataifa kulinda kazi za wasanii ambayo tanzania imeingia. Wameshindwa kutimiza mashart husika ndio wamefunga maduka kabla ya siku waliyopewa kama mgomo. Kuwapo kwa cd za nje za bei rahisi kunachangia sana kushuka kwa movie za nyumbani japo kuna changamoto nyingi ndani ya tasnia. Dunia nzima piracy hairuhusiwi tofauti ni utekelezaji tu. Kama unakumbuka defao alizimia alivyokuja tz miaka ya 90 na kukuta mwimbo wake mpya unauzwa kama njugu wakati hakuna kampuni yoyote nchini iliyoingia mkataba wa kusambaza mwimbo huo.
Hakuna hatua yoyote ya kimaendeleo ambayo haitaathiri upande mwingine tuvumilie na tusonge mbele kwa mfano ujenzi wa train ya umeme utaathiri mabus na malori je usitishwe?
 
India na Pakistan wana historia ya uhasama.Ila wana historia ya undugu pia. Kwa hiyo Wa Pakistan wanapenda sana kuangalia movie za Bollywood.

Basi kulitokea rabsha fulani Kashmir mpakani huko, serikali ya Pakistan ikaweka mwiko wa kuingiza sinema za Bollywood.

Ilibidi waachie wenyewe kutokana na nguvu za soko.

Haya mambo hayataki kutumia nguvu.
 
Back
Top Bottom