Machafuko/vurugu kubwa Kigamboni

Machafuko/vurugu kubwa Kigamboni

Joined
Mar 23, 2013
Posts
15
Reaction score
4
tetesi machafuko/vurugu kubwa kutokea‘'mjimpyamtarajiwa'' ferry kigamboni ni baada ya kuwepo kwa taarifa zisizo rasimi toka kwa mh diwani doto msawa, na nakuwapandisha jaziba na hasira wananchi zikiwataka wananchi kuvunja, bila yeye kufata utaratibu za kuvunja majengo au mabanda ndani ya sikwata.hivyo wavunje na kuhama eneo hilo au kuvunjiwa kwa nguvu nyumba na mabanda yao ya biashara yaliyopo katika eneo ambalo mpaka sasa ni sikwata, endapo hawatotii amri hiyo ya diwani wao.!!!!!!!!!!!!!!!!!!


diwani wa kata ya ferry doto msawa ''aka mkono wachuma'' ni kati ya madiwani wachache wajimbo la kigamboni, waliokaribishwa na waziri tibaijuka ,kuudhuria mkutono wa bajeti wa bunge kama wageni wa waziri huyo, bila mbunge wao ndugu ndungurile kuwa na taarifa za ujio wao bungeni hapo. Madiwani hao wakiwa na taarifa feki za kukubarika kwa mradi wa mji mpya kigamboni na wananchi, walitaka kusababisha mtafaruku mkubwa bungeni na kigamboni.
bila ya kutosheka na kero hiyo, hivi sasa yeye na mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa feri bwana juma mihambo na watendaji wao wameanzisha operation ya kutekeleza ujio wa mji mpya kwa kuanza na kuondoa nyumba na mabanda yaliyopo feri sokoni barabara inayoelekea tungi,kisiwani,na vijibweni.
Tarehe 22/03/2013 mwenyekiti akiwa na watendaji waamefika eneo hilo kuwapa maelekezo ya wapi pakuvunja wapi pakuacha kwa macho na mikono maafisa waliowaita maafisa wa tanroad na kuacha tena taarifa kwa wamiliki wa nyumba hizo na mabanda wavunje na kuondoa nyumba na mabanda yao kabla ya jumatatu tarehe 25/03/2013

historia fupi ya tabia hii chafu ya viongozi wa chama na serikari kuwafanyia fitina wafanya biashara walio maeneo mazuri kibiashara ya ferry.

  • chuo cha mwalimu nyerere ni mahara ilipo stendi ya vijibweni mnamo mwezi wa tano 2011 ambapo mh diwani alivamia usiku wa manane nakuvunja mabanda yote yaliyopo katika stendi hiyo na kupora mali zote zilizo kuwamo katika mabanda hayo.
· tajiri mmoja mwenye asiri ya kiarabu, scaba scuba na mh diwani wamejimilikisha kama wawekezaji wa eneo la soko na hivyo kujenga .na ukitaka eneo lolote hapo sio ukamwone mwenyekiti wa soko au kiongozi yeyote sokoni, bali watafute matajiri hawa.hivyo wao ndio wanaoongoza soko (diwani na matajiri) kwa sasa kwani kupitia kwao ndio unapata kuingia sokoni,na sio kupitia uongozi wa soko.

· mpaka sasa haya ndio maendeleo wanayosema wamefanya.kwahakika ni faida kwao na kuendeleza ubabe kwa kutafuta maeneo mengine zaidi.

ü wamejenga banda la mama lishe ambao mh diwani aliwavunja mabanda yao katika stendi ya vijibweni iliyopo chuo cha mwalimu nyerere, humo wanalipia mia tano kwa siku. Bandahilo muda si mrefu litabadilishwa frem kwani mamalishe wanachemka kwakuwa hakuna wateja na wanashindwa kulipa mia tano.

ü pia wame jenga eneo la kuuzia bidhaa za mazao.

Eneo hilo la soko mh diwani doto msawa anadai kapewa na mh.jakaya mrisho kikwete raisi ,ili kuliendeleza .hivyo kulichukua kutoka kwa wana wanachama wawili mmoja anafamika kwajina moja kiwia na mwenyekiti ya serikali ya mtaa bwana juma mihambo, anaefanya nae zowezi hili.

Mwenyekiti alikuwa na banda la voda la enzi hizo lakupigia simu kwa malipo kwa watu waliohitaji mawasiliano na hawakuwa na simu ambalo aliambiwa alitoe na akalitoa kulipeleka eneo la bandari ambapo ndio anafanyia kazi zake za kuudumia m-pesa na kiwia alikuwa akimiliki bar kwa jina la green garden.ilipokuwa green garden ndipo ambapo jengo la soko lipo. Na sasa limezungukwa na fremu za maduka ya matajiri.

· mbele kabisa ya eneo la soko amekabidhiwa mwingine anaefaamika kwajina la scaba scuba tajiri wa kigamboni, kajenga frem za maduka ambazo yeye ndie anaelipwa na kuzikodisha kwa kodi ya kuanzia kwa tsh 200000-300000/- frem hizo

ü inasemekana pia ni matajiri hawa hawa ndio wanataka eneo waliloambiwa wananchi waondoe vitu vyao kufikia juma pili, ili jumatatu zoezi la kuvunja lianze, kupisha analodai ni eneo la mtaro.

· mmiliki wa bar ya pentergon anamaumivu mpaka leo yakuvunjiwa kwa mikono bar yake iliyokuwapo eneo la kontena bar ya sasa pale kivukoni ferry kigamboni
· pia eneo ilipokuwa bar ya nevada zamani, sasa kuna ferry restaulant, japo kuwa bar ilivunjwa kwa madai ni eneo la barabara
matukio yote haya yametokea na hapakuwahi kuwa na mtu wa kusimama na kumwambia diwani doto au viongozi wengine husika katika matukio haya inatosha, sio viongozi wa chama wala wa serikali.hivyo basi kwa taarifa iliyopo wakati wa kumwambia kwa njia yeyote inayowezekana kwake kuelewa umefika.na hili litafanywa na wenye nchi na waliompa dhamana ya udiwani nawanaona, sasa inatosha, na kwakuwa hakuna wakumfunga paka kengere basi watamfunga panya kwa umoja wao wote.
:fear::fear::fear::fear::fear::crying::crying::crying::crying::crying::crying::crying::crying::crying:
 
Aisee! Huu unyama sasa, toa magamba hapo weka CDM
 
diwani wa kata ya ferry doto msawa ''aka mkono wachuma'' ni kati ya madiwani wachache wajimbo la kigamboni, waliokaribishwa na waziri tibaijuka ,kuudhuria mkutono wa bajeti wa bunge kama wageni wa waziri huyo, bila mbunge wao ndugu ndungurile kuwa na taarifa za ujio wao bungeni hapo. Madiwani hao wakiwa na taarifa feki za kukubarika kwa mradi wa mji mpya kigamboni na wananchi, walitaka kusababisha mtafaruku mkubwa bungeni na kigamboni.

Kesi ya Diwani Kigamboni kunguruma kesho
Kesi ya Diwani Kigamboni kunguruma kesho.


Wana Ferry wana haki ya kuendelea kuvumilia.Ukipanda Mahindi usitegemee kuvuna Maharage
 
Kati ya jambo baya lililowahi kuisibu nchi hii ni kuasisiwa kwa genge la kiharifu la "MTANDAO". Dhambi na laana ya mtandao itamfuata hadi kaburini kiongozi wake na members wake wote. Genge la mtandao ni genge lililokuja ku-paralyze mfumo mzima wa maadali ya uongozi, liliondoa hadhi ya utu (human dignity) na kuifanya sawa na bidhaa, liliondoa heshima ya mwanadamu na kumfanya sawa na kitu cha kufugwa na kinachoweza kuuzwa sokoni kwa wakati wowote. Ndio maana wanakigamboni you are there for sale, mtauzwa tu kama kuku wa kienyeji sokoniGenge la mtandao, genge la kiharifu, kwa kukamia kutwaa uongozi wa nchi lilipanga mipango kadhaa ya kimafia (organized crimes), mojawapo nikwenda BoT kupola mapesa ya EPA, MEREMETA, DEEP GREEN na mengine ambayo hayajawahi kujulikana lakini yapo, kwa mfano ukienda kwenye mifuko ya pension NSSF, PPF, n.k kunauharifu wa kutisha ambao haujawahi kuwekwa bayana lakini upo tena unatisha.Sasa hivi kila mfumo wa uongozi, wa kutoa maamuzi na haki uko-paralyzed. Nenda serikalini, nenda kwenye mahakama, nenda kwenye mashirika ya umma, nenda kwenye taasisi za umma, nenda wizarani, utakuta kwamba wale walioko kwenye viti hawana maamuzi kabisa ila kuna genge fulani nje ya mfumo rasmi ndilo linalotoa maamuzi ya nini kifanyike na nini kisifanyike. Nchi hii ina hali mbaya sana kimfumo, institutions ziko paralyzed kutokana na LAANA YA MTANDAO. Napendekeza kwamba mara baada ya uchaguzi 2015 iundwe tume maalum ya kuwabaini wanamtndao na kina cha maafa waliyoisababishia nchi hii kisha wapelekwe mahakamani.
 
Nasikia tunavutia wawekezaji kwa kuwadharau wananchi na kuwapora haki zao
 
Yaani ukisoma sred hizi unahisi uko Iraq au afghan
 
It's their choice-kukubali kutoka kwa kuwa wanatii sheria bira shruti au wawe kama wakazi wa Loliondo.
 
Ndugu zangu wana jamii mi nawashangaa sana, nimeleta taalifa baadhi yetu wanataka kuzodoana kuhusu vyama sasa yanaowakuta huku kigaboni, sio wa chama furani tu bali wote walasi mafungu ya watu, ni kutoka vyama vyote kwani tuna jua wazi fery ni sehemu iliyo changanya watu tofauti tofauti! jambo hili ni la kweli na ninafikili kwa baadhi ya wenye mamraka katika sisi wanataarifa
 
Back
Top Bottom