Mabomu ya machozi yanarindima wakati huu jimbo La Iramba Magharibi mkoani Singida ambapo Mgombea ubunge jimbo hilo kupitia CHADEMA Bi Jesca Kishoa inasemekana amekamatwa na kufungiwa ofisi za msimamizi wa uchaguzi.
Chanzo cha mabomu hayo kinadaiwa kuwa ni vurugu zilizotokea baada ya kutokea mabishano makali kati ya mgombea huyo na Msimamizi wa Uchaguzi, Inadaiwa kuwa JESCA KISHOA alimwekea pingamizi mgombea mwenzake kupitia CCM, Dkt Mwigulu Nchemba na mpaka sasa msimamizi amekataa kutoa majibu yake. Hali ya kukataa kutoa majibu ya pingamizi imepelekea hasira kwa mgombea huyo pamoja na wafuasi wake na ndiyo chanzo cha kuzuka kwa vurugu.
Mabom hayajawahi kuwa suluhu ya aman, bali haki ndio nguzo kuu ya Iman, ccm wanaotetea amani hawatetei haki, sisi tunaotetea haki tunambiwa tunafanya uchochezi wa kuvuruga amani, msingi au ngozo ya amani ni haki nasivinginevyo.
Mabomu ya machozi yanarindima wakati huu jimbo La Iramba Magharibi mkoani Singida ambapo Mgombea ubunge jimbo hilo kupitia CHADEMA Bi Jesca Kishoa inasemekana amekamatwa na kufungiwa ofisi za msimamizi wa uchaguzi...
Ungeanza tu ww mkuu kutoa mfano kama yule mwarab wa Tunisia muuza mchicha alivyo jitoa muhanga kwa faida ya watunisia wote, alafu sisi tupo nyuma yako kamanda..