Watu wakishapata madaraka wanajisahau sana, kiongozi mzima anaongea kwa kurahizisha eti silaha hazijatumiaka...
Huwezi kuamini kuwa anamaanisha hizo silaha hazijatumika kwa mama zake, Baba zake, Dada zake, Kaka zake Bibi Na Babu zake.
Viongozi wetu waache ulevi wa madaraka kujiona wao ndio bora kuliko wananchi wa kawaida.
Hizo silaha zikianza kutumika hata wao wenyewe Na familia zao hawatakua salama, unaweza kumkimbiza mke Na watoto wako nje ya nchi lakini Baba,mama, Dada,shangazi,na Ndugu wengine watakua wahanga wa hizo silaha unazojivunia.
Kovu ambalo litamuumiza Na yeye kwa kipindi cha uhai wake wote.