Mabalozi wa Mashina ya CCM wapigwe marufuku kujihusisha na masuala ya Serikali

Zakaria Lang'o

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
2,593
2,767
Mods naomba maoni haya yamfikie Mhe. Tundu Lissu kama mwanasheria na mpigania haki na utawala wa Sheria katika nchi yetu.
Kwa miaka mingi tangu ujio wa vyama vingi, Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikiwatumia Mabalozi wa mashina ya Chama kwa shughuli za kiserikali isivyo halali. Mabalozi hawa ambao hawamo katika mlolongo wa uongozi wa serikali kikatiba na kisheria wamekuwa wakifanya yafuatayo isivyo halali:
  • Kusikiliza kesi na mashauri katika maeneo yao huku wakijuwa wazi kuwa hawana mamlaka kisheria ya kufanya hivyo. Tabia hii imesababisha Chama cha Mapinduzi kupitia kwa mabalozi hawa kupoka mamlaka ya viongozi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji.
  • Kushiriki kuuza maeneo kwa kugonga mihuri yao ya shina katika karatasi za mauziano yanayofanywa na wananchi kinyume cha utaratibu. Miongoni mwa lawama wanazotupiwa viongozi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji juu ya matumizi mabaya ya mihuri kwa hakika wahusika wakuu ni mabalozi waliojivika majukumu ya kiserikali kinyume cha utaratibu wa kikatiba na kisheria.
  • Kutambuliwa na taasisi mbalimbali za kiserikali na za kibinafsi kama polisi, mahakama, mabenki n.k ni ishara mbaya ya vyombo vyetu kutojali kanuni za utendaji wa serikali, hivyo kusababisha mkanganyiko wa kuchanganya utendaji wa viongozi wa Chama cha Siasa na ule wa serikali. Inashangaza kwamba hata mahakama ambayo ndiyo inapaswa kusimamia sheria huweza kumwita balozi wa shina kuto
 
Wewe ndio hujui, hao ni mabalozi wa serikali na wanagombea, sema watu wamekariri ni lazima wawe CCM.
 
Mods naomba maoni haya yamfikie Mhe. Tundu Lissu kama mwanasheria na mpigania haki na utawala wa Sheria katika nchi yetu.
Kwa miaka mingi tangu ujio wa vyama vingi, Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikiwatumia Mabalozi wa mashina ya Chama kwa shughuli za kiserikali isivyo halali. Mabalozi hawa ambao hawamo katika mlolongo wa uongozi wa serikali kikatiba na kisheria wamekuwa wakifanya yafuatayo isivyo halali:
  • Kusikiliza kesi na mashauri katika maeneo yao huku wakijuwa wazi kuwa hawana mamlaka kisheria ya kufanya hivyo. Tabia hii imesababisha Chama cha Mapinduzi kupitia kwa mabalozi hawa kupoka mamlaka ya viongozi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji.
  • Kushiriki kuuza maeneo kwa kugonga mihuri yao ya shina katika karatasi za mauziano yanayofanywa na wananchi kinyume cha utaratibu. Miongoni mwa lawama wanazotupiwa viongozi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji juu ya matumizi mabaya ya mihuri kwa hakika wahusika wakuu ni mabalozi waliojivika majukumu ya kiserikali kinyume cha utaratibu wa kikatiba na kisheria.
  • Kutambuliwa na taasisi mbalimbali za kiserikali na za kibinafsi kama polisi, mahakama, mabenki n.k ni ishara mbaya ya vyombo vyetu kutojali kanuni za utendaji wa serikali, hivyo kusababisha mkanganyiko wa kuchanganya utendaji wa viongozi wa Chama cha Siasa na ule wa serikali. Inashangaza kwamba hata mahakama ambayo ndiyo inapaswa kusimamia sheria huweza kumwita balozi wa shina kuto
wenyeviti wa mitaa wa Chadema walipoambiwa ninyi sio viongozi wa serikali rudisheni mihuri wacha wakatae Lisu Hilo halioni? Chadema ukiwagusa kwenye mulo mmmmmmm
 
wenyeviti wa mitaa wa Chadema walipoambiwa ninyi sio viongozi wa serikali rudisheni mihuri wacha wakatae Lisu Hilo halioni? Chadema ukiwagusa kwenye mulo mmmmmmm
Sizungumzii wenyeviti wa mitaa wa Chadema, nazungumzia kitendo cha watu wasio na kiapo chochote cha uongozi wa kiserikali kufanya kazi za serikali kinyemela! Kama unataka kuwazungumzia hao wa Chadema anzisha uzi wako ndugu.
 
Sasa kwa Lissu pesa mbele, uko tayari kumlipa au unadhani ni mjomba wako huyo
 
Zakaria Lang'omwanangu 19985577 said:
Sizungumzii wenyeviti wa mitaa wa Chadema, nazungumzia kitendo cha watu wasio na kiapo chochote cha uongozi wa kiserikali kufanya kazi za serikali kinyemela! Kama unataka kuwazungumzia hao wa Chadema anzisha uzi wako ndugu.
Hao ni wawakilishi wa wananchi na wanagombea.Fuatilia ujue
 
Hao ni wawakilishi wa wananchi na wanagombea.Fuatilia ujue
Kuna watu wengi wenye uelewa potofu kama wako. Ukweli ni kuwa balozi ni kiongozi wa shina la Chama cha Mapinduzi na anachaguliwa na wanachama wa CCM walio katika shina husika. Kitendo cha kudhaniwa kuwa ni kiongozi wa serikali ni ujuha tu wa watu kama wewe.
 
Kuna watu wengi wenye uelewa potofu kama wako. Ukweli ni kuwa balozi ni kiongozi wa shina la Chama cha Mapinduzi na anachaguliwa na wanachama wa CCM walio katika shina husika. Kitendo cha kudhaniwa kuwa ni kiongozi wa serikali ni ujuha tu wa watu kama wewe.
Mkuu wewe ni kama wale.Hiyo imerithiwa toka chama kimoja ila ni wawakilishi wa serikali, sema watu wamekariri ni lazima awe CCM.Ni kama watu walivyokariri ili uwe rais ni lazima uwe na degree, kumbe si kweli
 
Wewe ndio hujui, hao ni mabalozi wa serikali na wanagombea, sema watu wamekariri ni lazima wawe CCM.
kugombea ndicho kigezo? hao ni viongozi wa chama kufanya majukumu ya serikali siyo sawa.
 
Wewe ndio hujui, hao ni mabalozi wa serikali na wanagombea, sema watu wamekariri ni lazima wawe CCM.
Hapana, kwenye serikali za Mitaa, hawapo. Madaraka yanaanzia kwa m/kiti wa kitongoji sio balozi
 
Back
Top Bottom