Mwangaza
Senior Member
- Feb 26, 2008
- 198
- 64
Wanabodi,
Wagombea wawili wa urais wamekuwa wakiahidi mabadiliko. Tunagalie kwa kina dhana halisi ya mabadiliko kwa hawa watu.
Lowassa ameahidi mabadiliko kwa kufanya yafuatayo:-
1.Kurudisha katiba ya warioba
2.Kutoa elimu bure mpaka chuo kikuu
3.Bima ya afya
4.Hospitali kila wilaya
5.Posho kwa wenyeviti vijiji/mitaa
Magufuli anahidi mabadiliko kwa kufanya yafuatayo:-
1. Kufungua mahakama ya mafisadi
2. Kutoa Elimu bure mpaka kidato cha nne
3. Kununua meli mpya 3
4. Kutoa millioni 50 kila kijiji
5. Kujenga mabarabara
Ukiangalia dhana hasa ya mabadiliko hakuna hata moja linaweza kufanikiwa kwa ufanisi hapo bila KUBADILISHA KATIBA KWANZA.
Katiba ikibadilishwa ikarudishwa katiba ya wananchi, ile ya tume ya Jaji Warioba, tutapata haya:-
1. Gharama za uendeshaji wa serikali zitapungua kwa zaidi ya 50%, kwa sababu mawaiziri, naibu na makatibu wao watapungua, wabunge watapungu, wajumbe wa baraza la wawakirishi watapungua, n.k.
2. Tutarudisha madaraka kwa wananchi-hivyo wataweza kuwawajibisha wabunge wazembe na mafisadi,watendaji wazembe na mafisadi,na hata mawaziri wazembe na mafisadi.
3. Tuongeza uhuru wa mahakama-maana jaji mkuu hatateuliwa na rais.
---Kufungua mahakama ya mafisadi wakati mahakama hazina uhuru,ni sawa na kuwa na TAKUKURU yenye kibogoyo kama hii.
4. Mawaziri, wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa..watakuwa watumishi wa wananchi sababu hawatakuwa wateule wa Rais.
5. Mgombea binafsi ataruhusiwa bila masharti magumu kama yalivyo kwenye katiba ya Chenge. Hii itaongeza demokrasia na kuhoji utendaji wa serikali.
6. N.k. n.k.
Tumeona nchi nyingi zimepata mabadiliko ya kimaendeleo baada ya kwanza kubadili katiba mbovu iliyopo, kwa mfano Kenya, Marekani, n.k.
HATUWEZI KULETA MABADILIKO BILA KWANZA KUBADILI KATIBA HII MBOVU.
Magufuli amedandia treni kwa mbele, mabadiliko anayosema HAYAWEZEKANI
NAUNGANA NA Mh LOWASSA AMBAYE ATALETA KATIBA YA WANANCHI... NDIPO TUTATAPATA MABADILIKO YA KWELI.
Wagombea wawili wa urais wamekuwa wakiahidi mabadiliko. Tunagalie kwa kina dhana halisi ya mabadiliko kwa hawa watu.
Lowassa ameahidi mabadiliko kwa kufanya yafuatayo:-
1.Kurudisha katiba ya warioba
2.Kutoa elimu bure mpaka chuo kikuu
3.Bima ya afya
4.Hospitali kila wilaya
5.Posho kwa wenyeviti vijiji/mitaa
Magufuli anahidi mabadiliko kwa kufanya yafuatayo:-
1. Kufungua mahakama ya mafisadi
2. Kutoa Elimu bure mpaka kidato cha nne
3. Kununua meli mpya 3
4. Kutoa millioni 50 kila kijiji
5. Kujenga mabarabara
Ukiangalia dhana hasa ya mabadiliko hakuna hata moja linaweza kufanikiwa kwa ufanisi hapo bila KUBADILISHA KATIBA KWANZA.
Katiba ikibadilishwa ikarudishwa katiba ya wananchi, ile ya tume ya Jaji Warioba, tutapata haya:-
1. Gharama za uendeshaji wa serikali zitapungua kwa zaidi ya 50%, kwa sababu mawaiziri, naibu na makatibu wao watapungua, wabunge watapungu, wajumbe wa baraza la wawakirishi watapungua, n.k.
2. Tutarudisha madaraka kwa wananchi-hivyo wataweza kuwawajibisha wabunge wazembe na mafisadi,watendaji wazembe na mafisadi,na hata mawaziri wazembe na mafisadi.
3. Tuongeza uhuru wa mahakama-maana jaji mkuu hatateuliwa na rais.
---Kufungua mahakama ya mafisadi wakati mahakama hazina uhuru,ni sawa na kuwa na TAKUKURU yenye kibogoyo kama hii.
4. Mawaziri, wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa..watakuwa watumishi wa wananchi sababu hawatakuwa wateule wa Rais.
5. Mgombea binafsi ataruhusiwa bila masharti magumu kama yalivyo kwenye katiba ya Chenge. Hii itaongeza demokrasia na kuhoji utendaji wa serikali.
6. N.k. n.k.
Tumeona nchi nyingi zimepata mabadiliko ya kimaendeleo baada ya kwanza kubadili katiba mbovu iliyopo, kwa mfano Kenya, Marekani, n.k.
HATUWEZI KULETA MABADILIKO BILA KWANZA KUBADILI KATIBA HII MBOVU.
Magufuli amedandia treni kwa mbele, mabadiliko anayosema HAYAWEZEKANI
NAUNGANA NA Mh LOWASSA AMBAYE ATALETA KATIBA YA WANANCHI... NDIPO TUTATAPATA MABADILIKO YA KWELI.