Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,268
- 33,040
Waonya kukithiri kwa ubinafsi wa viongozi
Watahadharisha utasababisha machafuko
Watamani Azimio la Arusha lirejeshwe
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Polycarp Kardinali Pengo, akiongoza sala ya Krismas katika Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam jana.
Viongozi wa madhehebu ya dini ya Kikristo nchini, wameonya tabia ya ubinafsi na ya kujilimbikizia mali inayofanywa na baadhi ya viongozi wa umma nchini na kutahadharisha kwamba kama hali hiyo itaachwa iendelee inaweza kuliingiza taifa katika machafuko.
Pia viongozi hao wametaka Azimio la Arusha kuhusu maadili ya viongozi kurejeshwa haraka ili kufanikisha vita dhidi ya rushwa na ufisadi miongoni mwa watendaji serikalini.
Walitoa onyo hilo wakati wakihubiri ibada ya sikukuu ya Krismasi ambapo kitaifa ilifanyika katika Kanisa la Mtakatifu Theresia mjini Tabora jana.
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tabora, Mhashamu Paul Ruzoka, amewataka viongozi wa umma nchini, kuacha tabia ya tamaa na kujilimbikizia mali kwa sababu tabia hyo inaweza kuliingiza taifa katika machafuko.
Alisema tabia hiyo imekuwa ikiwafanya wananchi wakate tamaa, kwa sababu inawasababisha viongozi wenye tamaa kushindwa kufuata maadili ya utumishi wa umma na hivyo kugeuka kama maadui wao kwa kuwa wanashindwa kutenda haki.
Askofu Ruzoka, alisema ni vyema sasa wakarejea katika misingi ya maadili aliyoianzisha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, ambayo ilijenga taifa lenye umoja na usawa na kuwafanya Watanzania kujiona kama watu kutoka sehemu moja.
Hata hivyo, alilaumu kuondolewa kwa Azimio la Arusha ambalo alisema uwepo wake ungesaidia kuimarika kwa maadili ya viongozi na
kupunguza tamaa na ushindani wa viongozi kumiliki mali na kuwasahau wananchi.
Askofu Ruzoka, pia aliwataka viongozi kuhakikisha kuwa utekelezaji wa sera ya Kilimo Kwanza nchini, hauiathiri wananchi na kuwaacha bila ya kuwa na ardhi.
Alisema sera hiyo sasa inahimiza uwepo wa wawekezaji na hivyo kuwepo kwa hatari ya Watanzania kuwa watumwa katika ardhi yao au kutumikishwa katika mfumo wa manamba, na kuhoji: "Wakishachukua ardhi kuna nini tena kitakachobakia?.
Aliwataka viongozi kuamka na kuanza kuwawezesha Watanzania ili watekeleze sera ya Kilimo Kwanza kwa vitendo na kujikwamua kiuchumi.
Alisema dhana ya Kilimo Kwanza msingi wake ni ardhi na kama ardhi haitakuwepo basi ni vigumu kutekelezeka na kuwasaidia Watanzania kuboresha maisha yao.
Akizungumzia athari za kutokuwepo kwa Azimio la Arusha, alisema ni pamoja na kuwepo kwa mbio za utajiri baina ya viongozi, kutofuatwa kwa maadili ya uongozi, kutokuwa na miiko, kuongezeka kwa posho katika vikao vingi na kuibuka kwa suala la mrahaba katika kazi mbalimbali za kiserikali na kukithiri kwa tamaa.
Akitoa mfano alisema ardhi ni rasilimali muhimu na inaweza kumuondoa mtu yeyote katika umaskini, hivyo kutoa mfano wa Mwalimu Nyerere, alipotembelea wilaya ya Urambo, alimkuta mkulima mmoja aliyepata Sh. 82,000 kwa mauzo ya tumbaku ambapo ni sawa na paundi 4,800.
Alisema kipato hicho kwa wakati huo kilikuwa ni sawa na mara 20 kwa mshahara wa Rais, ambacho kilimshawishi Mwalimu kutamani kuacha urais, lakini alisema alilazimika kuendelea kuwatumikia wananchi.
Alisema ni muhimu basi viongozi wa umma wakaendelea kufuata falsafa za Mwalimu Nyerere, kwa sababu zimelenga kuleta umoja wa kitaifa, haki, usawa, amani na utulivu huku akiamini kwamba pale ambapo pamekosewa, ni vyema kujisahihisha.
Alisisitiza kwamba hata Biblia Takatifu katika kitabu cha Yakobo, kinasisitiza kwamba "Tunda la uadilifu hupandwa katika amani" hivyo alionya kama misingi ya haki ikipuuzwa, amani hutoweka na uadilifu utabaki katika masimulizi pekee.
Alimsifu hayati Mwalimu Nyerere, kutokana na tabia yake ya kuiasa jamii na yeye mwenyewe kuishi sawa na misingi aliyoiamini kitu ambacho kilimfanya aishi bila ya kuwa na tamaa ya kujitajirisha, na kueleza kuwa kilikuwa mtihani mkubwa sana kwa viongozi wa zama hizo.
Ibada ya Krismas ilifanyika katika Kanisa la Mtakatifu Theresia mjini hapa, ambalo lina umri wa miaka 133 toka lilipojengwa na wamisionari wa kizungu.
Kwa upande wao, Mchungaji Michael Hafidh wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Zanzibar, Askofu Dickson Kaganga wa Kanisa la TAG Kariakoo na Askofu wa Kanisa Katoliki Zanzibar, Augustine Ndeliakyama Shao wametaka Azimio la Arusha kuhusu maadili ya viongozi
kurejeshwa haraka ili kufanikisha vita dhidi ya rushwa na ufisadi miongoni mwa watendaji serikalini.
Walitoa tamko hilo kwa nyakati tofauti wakati wa maadhimisho ya mkesha wa ibada ya Krismasi ambao ulifanyika katika makanisa mbalimbali mjini Zanzibar jana.
Askofu Kaganga alisema wakati huu wa kuelekea katika mjadala wa Katiba mpya, serikali lazima ifikirie kurejesha Azimio la Arusha litakalowabana vigogo wanaojihusisha na ufisadi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Alisema kutokana na kushamiri kwa vitendo vya rushwa na ufisadi, huduma za jamii zimeendelea kudorora huku baadhi ya viongozi wakijilimbikizia mali kutokana na kuweka mbele maslahi binafsi badala ya taifa.
Askofu huyo alisema pamoja na Tanzania kuwa na rasilimali kama za madini na bahari bado wananchi wake wameendelea kuishi katika mazingira ya umaskini kutokana na usimamizi mbovu wa rasilimali za taifa.
Alisema misingi ya maadili ya viongozi iliyowekwa na Baba wa taifa Mwalimu Nyerere na Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Sheikhe Abeid Karume imetupwa na kubakia historia. Leo hii kuna viongozi wanamiliki mali za kutisha bila kueleweka chanzo cha kipato chao.alisema Askofu Kaganga.
Alisema kwamba ndani ya azimio la Arusha yamo mambo mazuri ambayo yanaweza kusaidia taifa ikiwemo suala la viongozi kutojishirikisha na biashara wakiwa katika utumishi wa serikali.
Hata hivyo, alisema katika kuelekea mjadala wa katiba mpya ni jambo la busara kwa Watanzania kujiepusha na vitendo vya udini na ukabila ili kulinda misingi ya umoja wa kitaifa.
Naye Mchungaji Hafidh wa Kanisa Aglikana Dayosisi ya Zanzibar, alisema Watanzania imefika wakati kupambana kwa vitendo katika kupiga vita vitendo vya ufisadi unaofanywa na baadhi ya viongozi wake.
Katika Azimio la Arusha yapo mambo lazima yarejeshwe haraka kwa maslahi ya taifa kama suala la maadili kwa viongozi wetu wa serikali na hatua hiyo itasaidia kuondoa wimbi la ufisadi nchini, alisema Mchungaji Hafidh.
Alisema katika kusheherekea sikukuu ya Krismasi, ni vizuri kwa serikali kutafutia ufumbuzi migomo na maadamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu kwa malengo ya kudumisha umoja wa Watanzania.
Upande wake, Askofu Shao alisema rushwa na ufisadi utaondoka Tanzania iwapo viongozi wote wa serikali watakuwa tayari kukemea vitendo hivyo.
Ni lazima kuwe na nguvu za ziada kutoka kwa viongozi wa ngazi zote kukemea na kuwawajibisha wala rushwa hususani kwenye taasisi za uongozi.alisema askofu Shao katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Shangani mjini Zanzibar.
Alisema Watanzania hivi sasa wanaishi katika hali ngumu ya maisha kutokana na tatizo la mfumuko wa bei unaoendelea kujitokeza na kuwaumiza wananchi wengi masikini.
Wimbo kwamba Tanzania ni kisiwa cha amani kwa sababu hakuna vita ya silaha ni mwavuli wa siasa wa kuficha shida na maovu ya serikali zetu. alisema Askofu Shao.
Hata hivyo, alisema wakati Watanzania wameweka matumaini ya kuwa na maisha bora kupitia taasisi zilizokabidhiwa dhamana ya maendeleo ya nchi bahati mbaya taasisi hizo ndio zinaongoza kwa vitendo vya ufisadi na rushwa.
Mwananchi akimbilie wapi kama haki imekuwa ni bidhaa katika mahakama zetu. alisema Askofu Shao.
Alisema kutokana kushamiri kwa vitendo vya rushwa sekta ya elimu Tanzania imeendelea kuanguka na kushika nafasi ya mwisho katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Aliongeza kuwa tatizo la kununua mitihani limekuwa likichangia kwa kiwango kikubwa kuanguka kwa ubora wa elimu hapa nchini.
Aidha, alisema tatizo la mikopo ya elimu ya juu limekuwa giza kuu kwa taifa kutokana na watoto wengi wanaonufaika na mikopo hiyo kuwa ni wa viongozi na kuwaacha wanyonge.
Askofu Shao alisema mikopo ya elimu ya juu imekuwa ikiwanufaisha watoto wa viongozi wa serikali wakiwemo makatibu wakuu, mawaziri na wafanyabiashara na kuwanyima wananchi wanyonge.
Mkulima anayeishi chini ya Sh. 1,000 kwa siku hapati mkopo, tunapenda kuwaasa wahusika katika hili watende haki, alisema.
Kuhusu mfumo wa vyama vingi vya siasa alisema vimeleta mwanga wa kufichua maovu na udhaifu wa serikali.
Hata hivyo, alisema migogoro inayoendeleea kujitokeza katika vyama vya siasa inatokana na ubinafsi na uchu wa madaraka wa viongozi wa vyama hivyo.
Sikukuu ya Krismas Zanzibar imefanyika ikiwa imezorota tofauti na miaka ya nyuma kutokana na hali ngumu ya maisha baada ya soko la ndani la vyakula kuathiriwa na mfumuko mkubwa wa bei kuanzia Januari, mwaka huu.
Hata hivyo, zimefanyika katika mazingira ya amani na utulivu ambapo askari polisi walionekana kuimarisha doria katika makanisa mbalimbali ya Zanzibar.
ASKOFU LAISER ALILIA AMANI
Wilayani Monduli mkoani Arusha, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati, Dk. Thomas Laiser, ameonya kuwa amani iliyopo nchini ikitoweka hakuna Mtanzania atakayenusurika.
Kutokana na hali hiyo amewataka Watanzania kujihadhari na mambo yanayoweza kuondoa amani ambayo taifa imejipatia katika kipindi cha miaka 50 tangu kupata uhuru.
Alisema iwapo amani iliyopo itatoweka kwa sababu ya malumbano yoyote yale, hakuna Mtanzania atakayenusurika, hivyo, wanapaswa kumwomba Mungu asaidie katika hilo.
Alisema hayo katika mahubiri yake wakati wa ibada ya misa ya Krismasi iliyofanyika katika Usharika wa Monduli jana.
Leo hii tunapoadhimisha Krimasi yetu ya mwaka huu, miaka 50 baada ya uhuru, Kristo mleta amani atuletee amani kati yetu yapo mambo
ndugu zangu ambayo yatatuondolea amani hii aliyotuletea Yesu aliyezaliwa, alisema.
Alibainisha kuwa Watanzania kwa miaka mingi wamekuwa na umoja na wamekuwa wamoja licha ya kuwepo kwa makabila mengi na lugha nyingi lakini wameunganishwa na lugha moja ya taifa ambayo ni Kiswahili.
Tunazo imani zetu, tupo Waislamu, Wakristo na wafuatao imani za dini za asili, hivyo Wakristo wapende wasipende Waislamu watakuwepo na
Waislamu wapende wasipende Wakristo watakuwepo, alisema na kuhoji, malumbano ya nini?
Sisi ni taifa moja lenye amani ambalo mfano wake haupo katika Bara la Afrika tuheshimiane, tushikamane, tupendane na tusaidiane, kwani amani
yetu ikitoweka kwa sababu ya malumbano yoyote yale hakuna kati yetu atakayenusurika.
Akizungumzia dhana ya kutafuta ukweli, alitaka watu kuiga mfano wa Mamajusi wa Mashariki ambao hawakuwa tu watu wema, watakatifu au wenye
hekima bali walikuwa pia watu waliokazana kutafuta ukweli kuhusu kuzaliwa kwa Yesu wakiongozwa na nyota.
Alisema, Biblia inasema, Mamajusi wa Mashariki walifika Yerusalemu wakisema yuko wapi yeye aliyezaliwa Mfalme wa Wayahudi, maana tuliona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.
Alisema haishangazi kujua kwa nini hawa watu wa Mungu Mamajusi wa Mashariki walitafiti kujua ukweli huu wa kuzaliwa kwa Yesu Kristo, Ulimwengu wote ulikuwa na matazamio ya kuja kwa Masiha, hivyo ilikuwa ni lazima watafiti kujua ni yeye au ni mwingine. Kutokana na hali
hiyo, Watanzania hawana budi kutafuta ukweli wa jambo kabla ya kulizungumza ili kuepuka kuwa wazushi.
Ulimi wa kuropoka mambo katika familia, kwa jirani, mahali pa kazi, kanisani na hata katika nchi mara nyingi ndugu umeleta madhara makubwa jambo lisilo kweli likasemekana ni kweli baadaye ni vigumu kulifanya hilo lionekane sio kweli, alisema na kunukuu kitabu cha
Mithali 12:19 inayosema, Mdomo wa kweli utathibitishwa milele bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
PENGO NA DAWA ZA KULEVYA
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amewaasa Watanzania kuyasikiliza na kuyafuata maagizo ya Mwenyezi Mungu anayoyatoa kupitia kwa manabii wake ili waondokane na maisha ya shida na mifarakano wanayoendelea
kukumbana nayo; huku akiitaka serikali ichukue hatua madhubuti kudhibiti biashara haramu ya dawa za kulevya.
Kardinali Pengo, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa mahubiri kwenye Ibada ya Misa kusherehekea kuzaliwa kwa Bwana Yesu Kristo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph.
Alisema Mwenyezi Mungu anaendelea kuwaongoza wanadamu kuishi maisha ya kumpendeza kupitia kwa manabii wake na kwamba wanaposhindwa kuwasikiliza wanayoyasema na kuyaonya ni sawa na kumuona Mwenyezi Mungu ni muongo kama alivyofanya shetani pale alipowadanganya Adamu na Hawa.
Ni mambo mengi mabaya yaliyotokea na yanayoendelea kutokea katika jamii yetu ambapo manabii wameyasemea; kwa mfano walisema kuhusu biashara ya dawa za kulevya kuwa zinahatarisha maisha ya wananchi wetu, lakini badala ya kusikilizwa ikasemwa kuwa manabii hawa nao wanashiriki kwenye biashara hiyo, alisema.
Alisema kitendo kama hicho hakiisaidii jamii badala yake kinaendelea kuiweka katika mazingira yenye matatizo na shida mbalimbali za kimaisha kama zinazoendelea kutokea katika nchi yetu, ikiwa ni matokeo ya kutofanyia kazi maelekezo anayoyatoa Mwenyezi Mungu.
Kardinali Pengo alisema sherehe ya kuzaliwa kwa Bwana Yesu Kristo inaashiria mwanzo wa maisha mapya na alitoa rai kwa wananchi wote kuangalia hatua walizopiga kwa mwaka mzima tangu Krismas ya mwaka jana na endapo kutakuwa na mapungufu yaliyojitokeza waitumie Krismasi hii kumgeukia Muumba.
Suala la dawa za kulevya limekuwa ni tatizo ambalo viongozi wengi wa dini wamekuwa wakilipigia kelele wakiitaka serikali iwachukulie hatua watu wote wanaohusika na biashara hiyo kwa hoja kwamba inahatarisha maisha ya wananchi na hasa vijana.
Hata hivyo, suala hilo lilileta sintofahamu kubwa pale Rais Jakaya Kikwete, alipowatuhumu baadhi ya viongozi wa dini kuhusika na biashara hiyo
kwenye sherehe za kupewa daraja la Uaskofu na kusimikwa kwa Mhashamu John Ndimbo, kuwa Askofu mzalendo wa pili wa Jimbo la Mbinga.
Kwenye sherehe hizo zilizofanyika Juni 5, mwaka huu, Rais Kikwete, aliwataka viongozi wa dini kuacha kushiriki kwenye biashara ya kuuza dawa za kulevya, kauli ambayo ilipingwa vikali na viongozi wa dini wakiitaka serikali yake iwachukulie hatua za kisheria viongozi hao wanaojihusisha na biashara.
Viongozi hao walisema kwamba kauli ya Rais iliashiria kuwajua viongozi wa dini wanaojihusisha na biashara hiyo na hivyo wakashangaa kwa nini haiwakamati kwa kuwa kufanya biashara hiyo ni kosa la jinai na sheria haiangalii mtu.
DK. MALASUSA
Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa na Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, amewataka Wakristo wote nchini kusherehekea sikukuu cha Krismasi kitakatifu ikiwemo kusaidia waliopatwa na janga la mafuriko badala ya kufanya mambo yasiyompendeza Mungu.
Aidha, aliwataka Watanzania wote waliopateza ndugu zao na waliopatwa na janga la mafuriko yaliyotokea jijini Dar es Salaam mapema wiki iliyopita kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu kuelekea mwisho wa mwaka na mwanzo wa mwaka mpya wa 2012.
Dk. Malasusa alisema mwaka 2011 umekuwa na majanga mengi ya kitaifa ikiwemo lile la kuzama kwa meli ya Mv Spice Islanders ambalo mzee
mmoja wa kanisa hilo alipoteza maisha na mafuriko yaliyotokea na kusababisha baadhi ya Watanzania kupoteza maisha na makazi.
"Wakristo wenzangu nitumie nafasi hii kutoa pole kwa wenzetu waliopatwa na shida na janga la mafuriko yaliyotokea wiki iliyopita wawe na subira katika kipindi hiki kigumu...Wakristo watumie nafasi hii kuwasaidia wenzetu wanaohitaji msaada wetu na waache kusheherekea siku hii
kwa kutenda yale ambayo hayampendezi Mungu katika maadhimisho ya kuzaliwa Yesu Kristo," alisema.
Alisema Yesu Kristo alizaliwa katika hali duni na umaskini na kwamba Mungu habagui maskini wala matajiri hivyo Watanzania wote watumie nafasi hiyo kutafakari maadhimisho ya sikukuu ya Krismas.
"Tudumishe amani na kuomba kwa ajili ya majanga yanayotokea hapa nchini ili yasiweze kutokea tena," alisema askofu Malasusa.
Imeandikwa na Lucas Raphael, Tabora, Raphael Kibiriti na Hellen Mwango (Dar), John Ngunge (Monduli) na Mwinyi Sadallah (Zanzibar).
CHANZO: NIPASHE
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Polycarp Kardinali Pengo, akiongoza sala ya Krismas katika Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam jana.
Viongozi wa madhehebu ya dini ya Kikristo nchini, wameonya tabia ya ubinafsi na ya kujilimbikizia mali inayofanywa na baadhi ya viongozi wa umma nchini na kutahadharisha kwamba kama hali hiyo itaachwa iendelee inaweza kuliingiza taifa katika machafuko.
Pia viongozi hao wametaka Azimio la Arusha kuhusu maadili ya viongozi kurejeshwa haraka ili kufanikisha vita dhidi ya rushwa na ufisadi miongoni mwa watendaji serikalini.
Walitoa onyo hilo wakati wakihubiri ibada ya sikukuu ya Krismasi ambapo kitaifa ilifanyika katika Kanisa la Mtakatifu Theresia mjini Tabora jana.
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tabora, Mhashamu Paul Ruzoka, amewataka viongozi wa umma nchini, kuacha tabia ya tamaa na kujilimbikizia mali kwa sababu tabia hyo inaweza kuliingiza taifa katika machafuko.
Alisema tabia hiyo imekuwa ikiwafanya wananchi wakate tamaa, kwa sababu inawasababisha viongozi wenye tamaa kushindwa kufuata maadili ya utumishi wa umma na hivyo kugeuka kama maadui wao kwa kuwa wanashindwa kutenda haki.
Askofu Ruzoka, alisema ni vyema sasa wakarejea katika misingi ya maadili aliyoianzisha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, ambayo ilijenga taifa lenye umoja na usawa na kuwafanya Watanzania kujiona kama watu kutoka sehemu moja.
Hata hivyo, alilaumu kuondolewa kwa Azimio la Arusha ambalo alisema uwepo wake ungesaidia kuimarika kwa maadili ya viongozi na
kupunguza tamaa na ushindani wa viongozi kumiliki mali na kuwasahau wananchi.
Askofu Ruzoka, pia aliwataka viongozi kuhakikisha kuwa utekelezaji wa sera ya Kilimo Kwanza nchini, hauiathiri wananchi na kuwaacha bila ya kuwa na ardhi.
Alisema sera hiyo sasa inahimiza uwepo wa wawekezaji na hivyo kuwepo kwa hatari ya Watanzania kuwa watumwa katika ardhi yao au kutumikishwa katika mfumo wa manamba, na kuhoji: "Wakishachukua ardhi kuna nini tena kitakachobakia?.
Aliwataka viongozi kuamka na kuanza kuwawezesha Watanzania ili watekeleze sera ya Kilimo Kwanza kwa vitendo na kujikwamua kiuchumi.
Alisema dhana ya Kilimo Kwanza msingi wake ni ardhi na kama ardhi haitakuwepo basi ni vigumu kutekelezeka na kuwasaidia Watanzania kuboresha maisha yao.
Akizungumzia athari za kutokuwepo kwa Azimio la Arusha, alisema ni pamoja na kuwepo kwa mbio za utajiri baina ya viongozi, kutofuatwa kwa maadili ya uongozi, kutokuwa na miiko, kuongezeka kwa posho katika vikao vingi na kuibuka kwa suala la mrahaba katika kazi mbalimbali za kiserikali na kukithiri kwa tamaa.
Akitoa mfano alisema ardhi ni rasilimali muhimu na inaweza kumuondoa mtu yeyote katika umaskini, hivyo kutoa mfano wa Mwalimu Nyerere, alipotembelea wilaya ya Urambo, alimkuta mkulima mmoja aliyepata Sh. 82,000 kwa mauzo ya tumbaku ambapo ni sawa na paundi 4,800.
Alisema kipato hicho kwa wakati huo kilikuwa ni sawa na mara 20 kwa mshahara wa Rais, ambacho kilimshawishi Mwalimu kutamani kuacha urais, lakini alisema alilazimika kuendelea kuwatumikia wananchi.
Alisema ni muhimu basi viongozi wa umma wakaendelea kufuata falsafa za Mwalimu Nyerere, kwa sababu zimelenga kuleta umoja wa kitaifa, haki, usawa, amani na utulivu huku akiamini kwamba pale ambapo pamekosewa, ni vyema kujisahihisha.
Alisisitiza kwamba hata Biblia Takatifu katika kitabu cha Yakobo, kinasisitiza kwamba "Tunda la uadilifu hupandwa katika amani" hivyo alionya kama misingi ya haki ikipuuzwa, amani hutoweka na uadilifu utabaki katika masimulizi pekee.
Alimsifu hayati Mwalimu Nyerere, kutokana na tabia yake ya kuiasa jamii na yeye mwenyewe kuishi sawa na misingi aliyoiamini kitu ambacho kilimfanya aishi bila ya kuwa na tamaa ya kujitajirisha, na kueleza kuwa kilikuwa mtihani mkubwa sana kwa viongozi wa zama hizo.
Ibada ya Krismas ilifanyika katika Kanisa la Mtakatifu Theresia mjini hapa, ambalo lina umri wa miaka 133 toka lilipojengwa na wamisionari wa kizungu.
Kwa upande wao, Mchungaji Michael Hafidh wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Zanzibar, Askofu Dickson Kaganga wa Kanisa la TAG Kariakoo na Askofu wa Kanisa Katoliki Zanzibar, Augustine Ndeliakyama Shao wametaka Azimio la Arusha kuhusu maadili ya viongozi
kurejeshwa haraka ili kufanikisha vita dhidi ya rushwa na ufisadi miongoni mwa watendaji serikalini.
Walitoa tamko hilo kwa nyakati tofauti wakati wa maadhimisho ya mkesha wa ibada ya Krismasi ambao ulifanyika katika makanisa mbalimbali mjini Zanzibar jana.
Askofu Kaganga alisema wakati huu wa kuelekea katika mjadala wa Katiba mpya, serikali lazima ifikirie kurejesha Azimio la Arusha litakalowabana vigogo wanaojihusisha na ufisadi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Alisema kutokana na kushamiri kwa vitendo vya rushwa na ufisadi, huduma za jamii zimeendelea kudorora huku baadhi ya viongozi wakijilimbikizia mali kutokana na kuweka mbele maslahi binafsi badala ya taifa.
Askofu huyo alisema pamoja na Tanzania kuwa na rasilimali kama za madini na bahari bado wananchi wake wameendelea kuishi katika mazingira ya umaskini kutokana na usimamizi mbovu wa rasilimali za taifa.
Alisema misingi ya maadili ya viongozi iliyowekwa na Baba wa taifa Mwalimu Nyerere na Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Sheikhe Abeid Karume imetupwa na kubakia historia. Leo hii kuna viongozi wanamiliki mali za kutisha bila kueleweka chanzo cha kipato chao.alisema Askofu Kaganga.
Alisema kwamba ndani ya azimio la Arusha yamo mambo mazuri ambayo yanaweza kusaidia taifa ikiwemo suala la viongozi kutojishirikisha na biashara wakiwa katika utumishi wa serikali.
Hata hivyo, alisema katika kuelekea mjadala wa katiba mpya ni jambo la busara kwa Watanzania kujiepusha na vitendo vya udini na ukabila ili kulinda misingi ya umoja wa kitaifa.
Naye Mchungaji Hafidh wa Kanisa Aglikana Dayosisi ya Zanzibar, alisema Watanzania imefika wakati kupambana kwa vitendo katika kupiga vita vitendo vya ufisadi unaofanywa na baadhi ya viongozi wake.
Katika Azimio la Arusha yapo mambo lazima yarejeshwe haraka kwa maslahi ya taifa kama suala la maadili kwa viongozi wetu wa serikali na hatua hiyo itasaidia kuondoa wimbi la ufisadi nchini, alisema Mchungaji Hafidh.
Alisema katika kusheherekea sikukuu ya Krismasi, ni vizuri kwa serikali kutafutia ufumbuzi migomo na maadamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu kwa malengo ya kudumisha umoja wa Watanzania.
Upande wake, Askofu Shao alisema rushwa na ufisadi utaondoka Tanzania iwapo viongozi wote wa serikali watakuwa tayari kukemea vitendo hivyo.
Ni lazima kuwe na nguvu za ziada kutoka kwa viongozi wa ngazi zote kukemea na kuwawajibisha wala rushwa hususani kwenye taasisi za uongozi.alisema askofu Shao katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Shangani mjini Zanzibar.
Alisema Watanzania hivi sasa wanaishi katika hali ngumu ya maisha kutokana na tatizo la mfumuko wa bei unaoendelea kujitokeza na kuwaumiza wananchi wengi masikini.
Wimbo kwamba Tanzania ni kisiwa cha amani kwa sababu hakuna vita ya silaha ni mwavuli wa siasa wa kuficha shida na maovu ya serikali zetu. alisema Askofu Shao.
Hata hivyo, alisema wakati Watanzania wameweka matumaini ya kuwa na maisha bora kupitia taasisi zilizokabidhiwa dhamana ya maendeleo ya nchi bahati mbaya taasisi hizo ndio zinaongoza kwa vitendo vya ufisadi na rushwa.
Mwananchi akimbilie wapi kama haki imekuwa ni bidhaa katika mahakama zetu. alisema Askofu Shao.
Alisema kutokana kushamiri kwa vitendo vya rushwa sekta ya elimu Tanzania imeendelea kuanguka na kushika nafasi ya mwisho katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Aliongeza kuwa tatizo la kununua mitihani limekuwa likichangia kwa kiwango kikubwa kuanguka kwa ubora wa elimu hapa nchini.
Aidha, alisema tatizo la mikopo ya elimu ya juu limekuwa giza kuu kwa taifa kutokana na watoto wengi wanaonufaika na mikopo hiyo kuwa ni wa viongozi na kuwaacha wanyonge.
Askofu Shao alisema mikopo ya elimu ya juu imekuwa ikiwanufaisha watoto wa viongozi wa serikali wakiwemo makatibu wakuu, mawaziri na wafanyabiashara na kuwanyima wananchi wanyonge.
Mkulima anayeishi chini ya Sh. 1,000 kwa siku hapati mkopo, tunapenda kuwaasa wahusika katika hili watende haki, alisema.
Kuhusu mfumo wa vyama vingi vya siasa alisema vimeleta mwanga wa kufichua maovu na udhaifu wa serikali.
Hata hivyo, alisema migogoro inayoendeleea kujitokeza katika vyama vya siasa inatokana na ubinafsi na uchu wa madaraka wa viongozi wa vyama hivyo.
Sikukuu ya Krismas Zanzibar imefanyika ikiwa imezorota tofauti na miaka ya nyuma kutokana na hali ngumu ya maisha baada ya soko la ndani la vyakula kuathiriwa na mfumuko mkubwa wa bei kuanzia Januari, mwaka huu.
Hata hivyo, zimefanyika katika mazingira ya amani na utulivu ambapo askari polisi walionekana kuimarisha doria katika makanisa mbalimbali ya Zanzibar.
ASKOFU LAISER ALILIA AMANI
Wilayani Monduli mkoani Arusha, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati, Dk. Thomas Laiser, ameonya kuwa amani iliyopo nchini ikitoweka hakuna Mtanzania atakayenusurika.
Kutokana na hali hiyo amewataka Watanzania kujihadhari na mambo yanayoweza kuondoa amani ambayo taifa imejipatia katika kipindi cha miaka 50 tangu kupata uhuru.
Alisema iwapo amani iliyopo itatoweka kwa sababu ya malumbano yoyote yale, hakuna Mtanzania atakayenusurika, hivyo, wanapaswa kumwomba Mungu asaidie katika hilo.
Alisema hayo katika mahubiri yake wakati wa ibada ya misa ya Krismasi iliyofanyika katika Usharika wa Monduli jana.
Leo hii tunapoadhimisha Krimasi yetu ya mwaka huu, miaka 50 baada ya uhuru, Kristo mleta amani atuletee amani kati yetu yapo mambo
ndugu zangu ambayo yatatuondolea amani hii aliyotuletea Yesu aliyezaliwa, alisema.
Alibainisha kuwa Watanzania kwa miaka mingi wamekuwa na umoja na wamekuwa wamoja licha ya kuwepo kwa makabila mengi na lugha nyingi lakini wameunganishwa na lugha moja ya taifa ambayo ni Kiswahili.
Tunazo imani zetu, tupo Waislamu, Wakristo na wafuatao imani za dini za asili, hivyo Wakristo wapende wasipende Waislamu watakuwepo na
Waislamu wapende wasipende Wakristo watakuwepo, alisema na kuhoji, malumbano ya nini?
Sisi ni taifa moja lenye amani ambalo mfano wake haupo katika Bara la Afrika tuheshimiane, tushikamane, tupendane na tusaidiane, kwani amani
yetu ikitoweka kwa sababu ya malumbano yoyote yale hakuna kati yetu atakayenusurika.
Akizungumzia dhana ya kutafuta ukweli, alitaka watu kuiga mfano wa Mamajusi wa Mashariki ambao hawakuwa tu watu wema, watakatifu au wenye
hekima bali walikuwa pia watu waliokazana kutafuta ukweli kuhusu kuzaliwa kwa Yesu wakiongozwa na nyota.
Alisema, Biblia inasema, Mamajusi wa Mashariki walifika Yerusalemu wakisema yuko wapi yeye aliyezaliwa Mfalme wa Wayahudi, maana tuliona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.
Alisema haishangazi kujua kwa nini hawa watu wa Mungu Mamajusi wa Mashariki walitafiti kujua ukweli huu wa kuzaliwa kwa Yesu Kristo, Ulimwengu wote ulikuwa na matazamio ya kuja kwa Masiha, hivyo ilikuwa ni lazima watafiti kujua ni yeye au ni mwingine. Kutokana na hali
hiyo, Watanzania hawana budi kutafuta ukweli wa jambo kabla ya kulizungumza ili kuepuka kuwa wazushi.
Ulimi wa kuropoka mambo katika familia, kwa jirani, mahali pa kazi, kanisani na hata katika nchi mara nyingi ndugu umeleta madhara makubwa jambo lisilo kweli likasemekana ni kweli baadaye ni vigumu kulifanya hilo lionekane sio kweli, alisema na kunukuu kitabu cha
Mithali 12:19 inayosema, Mdomo wa kweli utathibitishwa milele bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
PENGO NA DAWA ZA KULEVYA
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amewaasa Watanzania kuyasikiliza na kuyafuata maagizo ya Mwenyezi Mungu anayoyatoa kupitia kwa manabii wake ili waondokane na maisha ya shida na mifarakano wanayoendelea
kukumbana nayo; huku akiitaka serikali ichukue hatua madhubuti kudhibiti biashara haramu ya dawa za kulevya.
Kardinali Pengo, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa mahubiri kwenye Ibada ya Misa kusherehekea kuzaliwa kwa Bwana Yesu Kristo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph.
Alisema Mwenyezi Mungu anaendelea kuwaongoza wanadamu kuishi maisha ya kumpendeza kupitia kwa manabii wake na kwamba wanaposhindwa kuwasikiliza wanayoyasema na kuyaonya ni sawa na kumuona Mwenyezi Mungu ni muongo kama alivyofanya shetani pale alipowadanganya Adamu na Hawa.
Ni mambo mengi mabaya yaliyotokea na yanayoendelea kutokea katika jamii yetu ambapo manabii wameyasemea; kwa mfano walisema kuhusu biashara ya dawa za kulevya kuwa zinahatarisha maisha ya wananchi wetu, lakini badala ya kusikilizwa ikasemwa kuwa manabii hawa nao wanashiriki kwenye biashara hiyo, alisema.
Alisema kitendo kama hicho hakiisaidii jamii badala yake kinaendelea kuiweka katika mazingira yenye matatizo na shida mbalimbali za kimaisha kama zinazoendelea kutokea katika nchi yetu, ikiwa ni matokeo ya kutofanyia kazi maelekezo anayoyatoa Mwenyezi Mungu.
Kardinali Pengo alisema sherehe ya kuzaliwa kwa Bwana Yesu Kristo inaashiria mwanzo wa maisha mapya na alitoa rai kwa wananchi wote kuangalia hatua walizopiga kwa mwaka mzima tangu Krismas ya mwaka jana na endapo kutakuwa na mapungufu yaliyojitokeza waitumie Krismasi hii kumgeukia Muumba.
Suala la dawa za kulevya limekuwa ni tatizo ambalo viongozi wengi wa dini wamekuwa wakilipigia kelele wakiitaka serikali iwachukulie hatua watu wote wanaohusika na biashara hiyo kwa hoja kwamba inahatarisha maisha ya wananchi na hasa vijana.
Hata hivyo, suala hilo lilileta sintofahamu kubwa pale Rais Jakaya Kikwete, alipowatuhumu baadhi ya viongozi wa dini kuhusika na biashara hiyo
kwenye sherehe za kupewa daraja la Uaskofu na kusimikwa kwa Mhashamu John Ndimbo, kuwa Askofu mzalendo wa pili wa Jimbo la Mbinga.
Kwenye sherehe hizo zilizofanyika Juni 5, mwaka huu, Rais Kikwete, aliwataka viongozi wa dini kuacha kushiriki kwenye biashara ya kuuza dawa za kulevya, kauli ambayo ilipingwa vikali na viongozi wa dini wakiitaka serikali yake iwachukulie hatua za kisheria viongozi hao wanaojihusisha na biashara.
Viongozi hao walisema kwamba kauli ya Rais iliashiria kuwajua viongozi wa dini wanaojihusisha na biashara hiyo na hivyo wakashangaa kwa nini haiwakamati kwa kuwa kufanya biashara hiyo ni kosa la jinai na sheria haiangalii mtu.
DK. MALASUSA
Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa na Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, amewataka Wakristo wote nchini kusherehekea sikukuu cha Krismasi kitakatifu ikiwemo kusaidia waliopatwa na janga la mafuriko badala ya kufanya mambo yasiyompendeza Mungu.
Aidha, aliwataka Watanzania wote waliopateza ndugu zao na waliopatwa na janga la mafuriko yaliyotokea jijini Dar es Salaam mapema wiki iliyopita kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu kuelekea mwisho wa mwaka na mwanzo wa mwaka mpya wa 2012.
Dk. Malasusa alisema mwaka 2011 umekuwa na majanga mengi ya kitaifa ikiwemo lile la kuzama kwa meli ya Mv Spice Islanders ambalo mzee
mmoja wa kanisa hilo alipoteza maisha na mafuriko yaliyotokea na kusababisha baadhi ya Watanzania kupoteza maisha na makazi.
"Wakristo wenzangu nitumie nafasi hii kutoa pole kwa wenzetu waliopatwa na shida na janga la mafuriko yaliyotokea wiki iliyopita wawe na subira katika kipindi hiki kigumu...Wakristo watumie nafasi hii kuwasaidia wenzetu wanaohitaji msaada wetu na waache kusheherekea siku hii
kwa kutenda yale ambayo hayampendezi Mungu katika maadhimisho ya kuzaliwa Yesu Kristo," alisema.
Alisema Yesu Kristo alizaliwa katika hali duni na umaskini na kwamba Mungu habagui maskini wala matajiri hivyo Watanzania wote watumie nafasi hiyo kutafakari maadhimisho ya sikukuu ya Krismas.
"Tudumishe amani na kuomba kwa ajili ya majanga yanayotokea hapa nchini ili yasiweze kutokea tena," alisema askofu Malasusa.
Imeandikwa na Lucas Raphael, Tabora, Raphael Kibiriti na Hellen Mwango (Dar), John Ngunge (Monduli) na Mwinyi Sadallah (Zanzibar).
CHANZO: NIPASHE