Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Maaskofu na Wachungaji wanaohudumu kupitia Kanisa la Glory Of Christ Tanzania Church(Ufufuo na Uzima) 'kanisa la Gwajima' wakiingia na kukaa katika chumba cha mahakama hapa katika Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Dodoma kwa ajili ya kufuatilia shauri la kanisa wanalohudumu ambalo limezuiwa kutoa huduma kuanzia juni 02, 2025.
Pia, Soma: Kesi ya Kanisa la Gwajima kufungiwa kunguruma leo Dodoma
Viongozi hawa wametoka maeneo mbalimbali nchini na kuja hapa Dodoma ili kujua hatma ya kanisa hilo lililopo chini ya Askofu Dkt. Josephat Gwajima ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Kawe, jijini Dar es Salaam.
Kesi hiyo inalenga kulinda hadhi ya usajili wa kanisa hilo huku rufaa dhidi ya zuio hilo ikiendelea kusikilizwa. Kanisa hilo linaongozwa na Askofu Josephat Gwajima, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kawe kupitia CCM.
Hivi karibuni, mamlaka za Serikali zilifunga kanisa hilo kwa madai kwamba linaendesha shughuli kinyume na masharti ya leseni ya usajili wake.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mamlaka, baadhi ya shughuli zinazofanyika ndani ya kanisa hilo zimeelezwa kuwa ni za ‘kisasa kupita kiasi’, na hazilingani na malengo ya asili ya taasisi hiyo kama ilivyosajiliwa.
Kupitia kwa wakili wake, Peter Kibatala, kanisa hilo limewasilisha shauri namba 13189 la mwaka 2025 dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Mwanasheria Mkuu wa Serikali, na Msajili wa Taasisi za Kiraia.
Katika shauri hilo, Glory of Christ Tanzania Church inaiomba mahakama kutoa amri ya muda itakayoruhusu kuendelea kwa ibada na shughuli nyingine za kidini, hadi pale rufaa iliyowasilishwa kupinga hatua ya serikali kufungia kanisa hilo itakaposikilizwa na kuamuliwa rasmi.
Pia, Soma: Kesi ya Kanisa la Gwajima kufungiwa kunguruma leo Dodoma
Viongozi hawa wametoka maeneo mbalimbali nchini na kuja hapa Dodoma ili kujua hatma ya kanisa hilo lililopo chini ya Askofu Dkt. Josephat Gwajima ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Kawe, jijini Dar es Salaam.
Kesi hiyo inalenga kulinda hadhi ya usajili wa kanisa hilo huku rufaa dhidi ya zuio hilo ikiendelea kusikilizwa. Kanisa hilo linaongozwa na Askofu Josephat Gwajima, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kawe kupitia CCM.
Hivi karibuni, mamlaka za Serikali zilifunga kanisa hilo kwa madai kwamba linaendesha shughuli kinyume na masharti ya leseni ya usajili wake.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mamlaka, baadhi ya shughuli zinazofanyika ndani ya kanisa hilo zimeelezwa kuwa ni za ‘kisasa kupita kiasi’, na hazilingani na malengo ya asili ya taasisi hiyo kama ilivyosajiliwa.
Kupitia kwa wakili wake, Peter Kibatala, kanisa hilo limewasilisha shauri namba 13189 la mwaka 2025 dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Mwanasheria Mkuu wa Serikali, na Msajili wa Taasisi za Kiraia.
Katika shauri hilo, Glory of Christ Tanzania Church inaiomba mahakama kutoa amri ya muda itakayoruhusu kuendelea kwa ibada na shughuli nyingine za kidini, hadi pale rufaa iliyowasilishwa kupinga hatua ya serikali kufungia kanisa hilo itakaposikilizwa na kuamuliwa rasmi.