sembo
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 4,350
- 3,451
Bado nikiwa katika viyunga vya hili jiji la Kigali, nimeona si mbaya nikishea nanyi hii stori niliyoipata huku.
Nadhani Meddie Kagere si jina geni nchini Tanzania.
Huyu jamaa alizaliwa katika mji wa Entebe uliopo nchini Uganda. Meddie Kagere alianza kusakata soka katika timu ya Mbale Heroes iliyopo Uganda kabla ya kuhamia nchini Rwanda, ambapo alicheza katika timu kadhaa kabla ya kutua katika miamba ya soka nchini humo, Rayon Sports ambapo historia iliandikwa.
Meddie Kagere alitandaza mpira mwingi saaana akiwa Rayon Sports. Ikumbukwe kipindi hiki alikua bado hajaitwa timu ya Taifa ya Uganda. Kwa soka alilokua akilitandaza alisababisha maandamano makubwa sana nchini kwake, si toka kwa mashabiki wa Rayon Sports tu bali hata wapinzani wao wakubwa APR wote wakishinikiza apewe uraia fasta ili aweze kuitumikia timu ya Taifa ya Rwanda (ingekua Bongo mashabiki wa Simba SC na Ndala tushinikize Asante Kwasi apewe uraia wa Tanzania).
Nasikia Rais Paul Kagame asingekua makini, haya maandamano yalikua yanamuondoa madarakani. Hatimae mwaka 2014 Meddie Kagere alikabidhiwa uraia wa Rwanda, na katika mechi ya kwanza jamaa alicheka na nyavu. Kilichofuata baada ya hapo ni historia.
Nikiripoti toka viyunga vya Kigali hapa Rwanda.. Ni Mimi sembo wa Simba TIIIIIIIIVIIIIIIIIIIIIIIIII (in George Malatu Voice)
Nadhani Meddie Kagere si jina geni nchini Tanzania.
Huyu jamaa alizaliwa katika mji wa Entebe uliopo nchini Uganda. Meddie Kagere alianza kusakata soka katika timu ya Mbale Heroes iliyopo Uganda kabla ya kuhamia nchini Rwanda, ambapo alicheza katika timu kadhaa kabla ya kutua katika miamba ya soka nchini humo, Rayon Sports ambapo historia iliandikwa.
Meddie Kagere alitandaza mpira mwingi saaana akiwa Rayon Sports. Ikumbukwe kipindi hiki alikua bado hajaitwa timu ya Taifa ya Uganda. Kwa soka alilokua akilitandaza alisababisha maandamano makubwa sana nchini kwake, si toka kwa mashabiki wa Rayon Sports tu bali hata wapinzani wao wakubwa APR wote wakishinikiza apewe uraia fasta ili aweze kuitumikia timu ya Taifa ya Rwanda (ingekua Bongo mashabiki wa Simba SC na Ndala tushinikize Asante Kwasi apewe uraia wa Tanzania).
Nasikia Rais Paul Kagame asingekua makini, haya maandamano yalikua yanamuondoa madarakani. Hatimae mwaka 2014 Meddie Kagere alikabidhiwa uraia wa Rwanda, na katika mechi ya kwanza jamaa alicheka na nyavu. Kilichofuata baada ya hapo ni historia.
Nikiripoti toka viyunga vya Kigali hapa Rwanda.. Ni Mimi sembo wa Simba TIIIIIIIIVIIIIIIIIIIIIIIIII (in George Malatu Voice)