Maandamano ni ushamba

Maandamano ni ushamba

Bahimba

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2013
Posts
510
Reaction score
346
Zikiwa zimebaki takribani saa kazaa tu kuwasili kwa kiongozi wa taifa la Marekani bwana Barack Obama, mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, amesema kuandamana na kubeba mabango ni ushamba.

ameyasema hayo katika kipindi maalum kilichokua kikirushwa na TBC, akaenda mbali zaidi kwa kusema maandamano yeyote yale kimsingi hua hayana maana yeyote ile, kwa sababu hata kama ukiandamana haitakusaidia zaidi ya kupoteza muda wako tu.

Nimejiuliza maswali mengi sn juu ya maelezo ya mkuu wa mkoa na tafsili zake juu ya hoja nzima ya maandamano, zipo sababu nyingi ambazo zinapelekea watu kuandama, hata huko anakotokea Obama kuna baadhi ya watu tumeona waliandamana kupinga ujio wa Obama nchini mwao, sasa kwa mujibu wa kauli za mkuu wa mkoa kwa niaba ya serikali anataka atulazimishe watanzania wote tukubaliane na matakwa ya serikali hata kama ni mabaya.

NAWASILISHA.
 
Hivi mkuu wa mkoa kazi yake ni nini?

Naona Pinda amewafundisha watu wa serikalini wote kuhalifu sheria bila woga. Kwahiyo katiba ya Tanzania ni Ushamba!...my hairs!

Kulewa madaraka huku, na kujiona kuwa proletariet class haina maana na ni ya KUPIGWA TU!

WAPIGWE TU!
 
Zikiwa zimebaki takribani
saa kazaa tu kuwasili kwa kiongozi wa taifa la Marekani bwana Barack
Obama, mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, amesema kuandamana na kubeba
mabango ni ushamba,
ameyasema hayo katika kipindi maalum kilichokua kikirushwa na TBC,
akaenda mbali zaidi kwa kusema maandamano yeyote yale kimsingi hua
hayana maana yeyote ile, kwa sababu hata kama ukiandamana haitakusaidia
zaidi ya kupoteza muda wako tu,
Nimejiuliza maswali mengi sn juu ya maelezo ya mkuu wa mkoa na
tafsili zake juu ya hoja nzima ya maandamano, zipo sababu nyingi ambazo
zinapelekea watu kuandama, hata huko anakotokea Obama kuna baadhi ya
watu tumeona waliandamana kupinga ujio wa Obama nchini mwao, sasa kwa
mujibu wa kauli za mkuu wa mkoa kwa niaba ya serikali anataka
atulazimishe watanzania wote tukubaliane na matakwa ya serikali hata
kama ni mabaya.NAWASILISHA.
cdm imekula kwenu
 
Akili Ndogo, Kuongoza AKILI kubwa.
Mpotezeee!
Na wewe unafanya nini TBC saa hizi, watu wote wako MARACANA saa hizi. Closing ceremony imeanza.
 
Maandamano ni ushamba hivyo watu wenye kutaka kufikisha ujumbe wajikusanye mahali moja au "WAFIKISHAJE UJUMBE"???Au anaishi dunia nyingine nini??Teh,teh,teh!hela za kigamboni tam.
 
Zikiwa zimebaki takribani saa kazaa tu kuwasili kwa kiongozi wa taifa la Marekani bwana Barack Obama, mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, amesema kuandamana na kubeba mabango ni ushamba,
ameyasema hayo katika kipindi maalum kilichokua kikirushwa na TBC,
akaenda mbali zaidi kwa kusema maandamano yeyote yale kimsingi hua hayana maana yeyote ile, kwa sababu hata kama ukiandamana haitakusaidia zaidi ya kupoteza muda wako tu,
Nimejiuliza maswali mengi sn juu ya maelezo ya mkuu wa mkoa na tafsili zake juu ya hoja nzima ya maandamano, zipo sababu nyingi ambazo zinapelekea watu kuandama, hata huko anakotokea Obama kuna baadhi ya watu tumeona waliandamana kupinga ujio wa Obama nchini mwao, sasa kwa mujibu wa kauli za mkuu wa mkoa kwa niaba ya serikali anataka atulazimishe watanzania wote tukubaliane na matakwa ya serikali hata kama ni mabaya.NAWASILISHA.

Mwambie akawaambie Wamisri hayo maneno kama atarudi salama.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
UKINUNULIWA KWA BUKU 7 za mwigulu IPO SIKU UTAUZWA KWA BUKU 2. Uzalendo ni natural heritage.
 
Mwambie akawaambie Wamisri hayo maneno kama atarudi salama.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

Siyo kwamba mshamba ni yeye RC? OBAMA mwenyewe anajua ambavyo hata nchini mwake huwa wanaandamana sembuse Tanzania? Au na RC ni MLIBERALI nini?
 
Siyo kwamba mshamba ni yeye RC? OBAMA mwenyewe anajua ambavyo hata nchini mwake huwa wanaandamana sembuse Tanzania? Au na RC ni MLIBERALI nini?

Viongozi wa Tanzania huwa wana-take advantage ya ujinga wa Watanzania kuhusu haki zao za msingi.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
February, 2013 wakuu wake wote waliandamana akiwemo JK, Kinana na Mangula ktk kuazimisha kuzaliwa kwa CHAMA chao kule Kigoma... Kama na hawa ni washamba basi na yeye ni mshamba.
 
mimi nimemskia jana akitamka kuwa kwanza maandamano ni ushamba...mpaka nikashtuka hv huyu bwana ajui maandano ni njia nzuri ya kufikisha ujumbe' ? aoni mataifa mengine yanatumia nafasi ya kiongozi yeyote wa kitaifa anapo wasili mahali au kwenye nchi nyingine basi hapo hapo wananchi utumia haki yao ya msingi kwa kuandamana kufikisha ujumbe..alafu huyu mzee anasema ni ushamba.
 
We haupo duniani maandamano si ushamba wablazil washamba,misri nao,turkey. Labda ww
 
Viongozi wa Tanzania huwa wana-take advantage ya ujinga wa Watanzania kuhusu haki zao za msingi.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
watz sio wajinga labda ww peke yako. haki zao za msingi wanapata labda za sekondari
 
Maandamano ya Chadema ni ushamba.

Usimtetee, hakusema maandamano ya CHADEMA, bali amesema maandamano kwa ujumla wake, kwa hiyo hata yale ya ccm wanayofanya asubuhisubuhi nchi nzima wenyewe mkiyaita ya mshikamano ni ushamba mtupu! (Rc wenu wenyewe huyo!)
 
Ha ha haaa, dah, yani hizi kauli saa ingine inabidi ucheke tu, Eti kuandamana ni ushamba!
 
Back
Top Bottom