Maalim Seif: Muda ukifika nitazungumza

Maalim Seif: Muda ukifika nitazungumza

Maalim na watu wake wa Zanzibar wakihamia CHADEMA ni pigo kuu Takatifu kwa CCM maana misheni yao ya kuiua CUTF Zanzibar itafeli vibaya mno. Just imagine muungano wa CUF na CHADEMA via UKAWA ulivyoifanya Maalim na CUF yake kuishinda CCM kwa gapu kubwa sana haijawai kushinda kiasi hicho. Sasa fikiria Combination hiyo ndani ya Chama kimoja. Mwenyekiti Mbowe, Katibu Mkuu Maalim Seif, Mkamo mwenyekiti Juma Duni au Jussa hatari sana
Mwanangu hii itakuwa kama galacticos pale Real Madrid.
 
Julius Mtatiro ana siri nyingi sana za Maalim hata yule mganga wake ambae humsafishiaga nyota huko ungazija Komoro ameshajulikana .

Hapa ndio Mtatiro anapoingia ulingoni maalim anaweza asifikie uamuzi kwa sababu ya ulimi na mikono kuvimba.
Usituletee ramli hapa uchawi peleka Lumumba
 
Nadhani endapo Maalim Seif atahamia CDM basi naamini mpasuko mkubwa sana utakuwa ndani ya CDM kwanin nasema hivi chadema haijawa well organized hasa visiwani sasa kumleta Seif nadhani haitokuwa na tija sana huku bara na hata visiwani. Maalim atulie siasa ya bongo haiwezi kubadilika kwa maana mwenye maamuzi anaamua bila kujali matokeo yakoje.
Mpasuko ki vipi eleza, Chadema ni taasisi haiwezi kupasuliwa na mtu mmoja ingekuwa kupasuka ingepasuka wakati wa ujio wa Lowassa.
 
Sakaya hahakosea kuwa cdm wanamtaka Maalim ili wajiimarishe tu. Mana zenj hawana ushawishi. Ushauri ni maalim kuanzisha chama kipya akiona Cuf hakuna liwalo
Maalimu aanzishe chama kipya? Tanzania?
you are not serions.
 
Maalim Seif na wapambe wake kuhamia Chadema haitakuwa ajabu maana CUF Lipumba ndiyo inatambuliwa na Msajili na Tume, na kwa maana hiyo ndiyo wenye mamlaka ya kuamua mgombea gani asimame kwa tiketi ya CUF na kamwe (kwa kusudi maalumu), hawatathubutu kumpitisha Maalim na Wabunge wake kugombea Urais na Ubunge kwa tiketi ya CUF.

Kwa kuwa mgogoro wa CUF Lipumba na CUF Maalim uko mahakamani, ni wazi lazima upo upande utashinda kesi, iwapo CUF Lipumba watashinda, watawavua uanachama Seif na Wabunge wake uanachama na kwa siasa za Zanzibar, lazima Seif na wafuasi wake wagombee. Kwa hiyo hakuna namna. Lkn pia kwa mazingira ya sasa , bila wapinzani kuungana hawataweza ku-survive maana ni wazi kuna mkakati wa kuua upinzani, na ndani ya wapinzani kuna vibaraka wengi ambao sasa wanarudi CCM na kutoa fursa kwa wapinzani kubakiwa na wapinzani halisi ambao itawapasa kuunganisha nguvu ili waweze kupambana na dola na CCM.

Kwa maana hiyo, kuna uwezekano wa asilimia 75 kwa Maalim na wenzake kujiunga na Chadema ili waweze kusimama Zanzibar, ukizingatia kuwa Chadema haina msingi imara Zanzibar.

Kama upo mkakati wa makusudi kuisambaratisha CUF kutoka kwa dola na CCM, bila shaka watajuta sana iwapo Maalim na kundi lake wataenda Chadema. Ikumbukwe kuwa kwa siasa za Zanzibar, vyama vilivyopo ni kivuli cha vyama vikivyokuwepo kabla ya Mapinduzi ya 1964; ASP, ZPP, na ZNP, ni vyama vilevile vyenye majina mapya.

Vv
Hii inaitwa chenga ya mwili.
 
Maalimu aanzishe chama kipya? Tanzania?
you are not serions.
Kwan unafkr wazanzibari wanakipenda Cuf au wampenda Maalim? Akiingia leo ccm yule na dk Shein awe Cuf bas CCM itashind kihalali
 
Dalili ya mnvua ni mawingu, na akili ya kuambiwa ........
Sio tena kuzungumza kuhusu urais wake aliosema atapewa'soon'!!
Wajinga ndio waliwao sefu hapati urais wa zanzibar hata iweje,kwa hiyo hana haja ya kujiunga na chadema kuipa ruzuku,anaweza hata kujiunga na Tadea au chausta atapata wabunge,wawakilishi na na VP
 
Naunga mkono Maalim Seifu na Wana CUF Zanzibar, kutafuta Chama kipya cha kuungana nacho. CUF hivi sasa ni mateka wa CCM kwa usaliti wa Lipumba.

Jifunzeni Kenya, Chama hakijawahi kuwa kikwazo kwa ushindi wowote panapokuwa na political will.

Siasa ni agenda, sio chama. Waachieni CCM na Lipumba CUF yao, Songeni mbele, Hakuna mtakachopoteza zaidi ya huo umakamu wa kwanza na wizara mbili zisizo na tija kwenu.

CCM haiko tayari kwa vyovyote vile kuiona CUF Ikulu ya Zanzibar.

Kwa CCM, tatizo sio CUF bali ni Maalim Seif. Kwahiyo hata akiamua kuhamia CHADEMA, bado suala la kudhulumiwa ushindi wake liko pale pale. Labda tu kama atakuwa amejipanga kivingine kuhakikisha dhulma haifanikiwi. Kwa upande wa Wazanzibari wao wana angalia Seif yupo chama gani, na hicho chama kitaungwa mkono. Hivyo basi, hii hoja kwamba CHADEMA haina nguvu ZNZ haina mashiko, kwani hata Seif akiamua kuhamia CHAUMMA, bado atashinda urais. Swali linabaki je CCM watampa ushindi wake???
 
In politics you have to be flexible.kuwa na misimamo ambayo hauna followers Ni kupotea katika ulimwengu wa siasa,
 
Back
Top Bottom