Teknolojia ni Yetu sote
JF-Expert Member
- Apr 28, 2020
- 1,221
- 2,425
Kuna app iko kwenye kila simu unayoijua wewe hapa Duniani, lakini watu wengi hawaijui vizuri na hawajawahi kuijaribu kuitumia Hata mara moja wengi wanaiogopa kabisa.
Unajua kwanini!!!๐๐ Je app hii inafanya kazi gani ? Kwanini ipo kwenye kila simu ?? Leo nitakujuza kabisa๐.
Sim Toolkit ni app ambayo inapatikana kwenye simu yako ambayo inakuja na kila line ya simu unayoweka kwenye simu yako ili kupiga simu na kutumia data.
Program hii mara nyingi hufupishwa kuwa STK utakutana nazo kwenye simu nyingi za Android.
Sim Toolkit inaunganisha simu yako na mtandao wa simu ( Airtel,Tigo, Vodacom,halotel,Ttcl au nyinginezo). Sim Toolkit inakusaidia kufanya mambo mbalimbali kwa urahisi kupitia simu yako kuanzia;
โก Kununua bando
โก Kutuma salio
โก Kubadilisha pin
โก Masuala ya kifedha
โก Kujiunga na promosheni mbalimbali nk.
Kila unachokifanya kwenye hii app ni Amri yako haiwezi kufanya chochote bila amri yako hivyo usijali kabisa haiwezi kusoma sms yako yoyote, kuchukua taarifa za app zinginezo nk.
Kubwa zaidi inafanya kazi bila mtandao (intaneti) kwani yenyewe inatumia USSD (unstructured supplimentary services data), unaweza nunua bando bila kuandika zile code za kununua bando.
Unaweza lipia bili, kutuma pesa, kununua kifurushi, kufuatilia Matumizi mbalimbali ya simu yako bila kuhitaji app kama vile mix by yas , Airtel app, m pesa nk.
Umeshawahi kutumia hii app ya STK kwenye simu yako au ulikua
unashangaa tu ??