Ma DC bungeni, conflict of interest

Taso

JF-Expert Member
Jun 12, 2010
2,445
2,268
Mwenyekiti wa Bunge, Jenista Mhagama, mapema leo amekataa kusomwa na kujibiwa maswali ya wabunge wawili ambao wamechaguliwa kuwa Wakuu wa Wilaya hivi karibuni. Amesema, haiwezekani Mkuu wa Wilaya ambae ni sehemu ya serikali kuihoji serikali hiyo hiyo ambayo yeye ni sehemu yake.

Maoni yangu: Kwanza namsifu Mwenyekiti Mhagama kwa kutambua hilo, kwa sababu amesema kwa kweli hakuna kanuni inayoongelea ni nani anaruhusiwa kuuliza swali bungeni, amesema ana mamlaka ya kuamua kukataa au kukubali swali la mtu yeyote, (hata la Taso wa JamiiForums?!) . Pili ni bahati mbaya sana Rais Kikwete ana hulka ya kulimbikiza vyeo kwa watu ambao wanaishia kuwa kwenye mihimili zaidi ya mmoja. Sasa wewe ni Mbunge na ni mwana serikali, unawajibika kwa bunge kama serikali au unaisimamia Serikali kama mbunge?

Hayo maswali yaliyokataliwa, ina maana duku duku za wananchi zilizobebwa na maswali hayo hayataweza kupatiwa msaada au majibu, hivyo wananchi wamekosa uwakilishi kwa namna moja ama nyingine. Lini tunakuwa na utengano kamili wa mihimili ya nchi?
 
Mwenyekiti wa Bunge, Jenista Mhagama, mapema leo amekataa kusomwa na kujibiwa maswali ya wabunge wawili ambao wamechaguliwa kuwa Wakuu wa Wilaya hivi karibuni. Amesema, haiwezekani Mkuu wa Wilaya ambae ni sehemu ya serikali kuihoji serikali hiyo hiyo ambayo yeye ni sehemu yake......

Mbona leo Martha Umbulla, Mbunge wa Viti Maalum na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa karuhusiwa kuuliza swali?
 
Taso zaidi ya robo ya wabunge wote hawawezi kuhoji chochote serikalin kwa vile ni mawaziri wakuu wa mikoa na wilaya!
 
Last edited by a moderator:
Taso
umeleta lugha gongana ya muhimu sana.
Sema kweli hii nchi kuna watu wanaiba ila wizi wao unafunikwa wingu la baraka za viongozi feki.
Kuna faida gani kumchagua kuwa mkuu wa wilaya mtu ambaye tayarui ni Mbunge????
Kwa maoni yangu naona Mamlaka inayomchagua nayo si Makini.
How can you save two Masters at Once?? HUU NI WIZI.
Kuna Kundi linatuibia-Full stop
 
Heri turejee miiko ya uongozi enzi za Azimio la Arusha, panaposema - "Kiongozi asiwe na mishahara miwili".
 
Siku zote nimekuwa nikiiamini Jenista Muhagama angefaa kuwa Spika kuliko Anne Makinda.
 
Hapa kwetu kuna muingiliano mkubwa sana baina ya serikali na bunge, kiasi cha kuwa ninadhani hata Wabunge wenyewe hawalielewi hilo

Siku Rais akimchagua Mbunge mmoja kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ninadhani ndipo watakaposhtuka. Sasa hivi wamejisahau wakidhani kuwa bunge na serikali ni kitu kimoja.
 
Nchi hii ina mambo ya AJABU sana. Mtu ukiwa DC halafu ukataka kugombea UBUNGE unajiuzulu hicho cheo cha u-DC. Hali kadhalika ukiwa mtumishi wa serikali ukataka kugombea ubunge inabidi ujiuzulu utumishi wa umma.

Maajabu kama sio UJINGA ni pale eti umeshakuwa MBUNGE mtu mmoja anayeitwa RAIS anaweza kukuteua tena kuwa DC au RC? Kulikuwa na mantiki gani basi ya kumlazimisha DC kujiuzulu cheo chake kabla ya kugombea ubunge kama Rais anaweza kumteua kuwa DC baada ya kupata UBUNGE?!.

Mimi ninaisubiri tume ya katiba kwa hamu kuondoa huu UPUMMBAVU
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom