M/kiti wa Chama cha wenye Kisukari Tanzania: Bora sukari iadimike tu

kudra hamidu

Senior Member
Jul 1, 2012
152
107
MWENYEKITI wa Chama cha wenye Kisukari Tanzania, Profesa Andrew Swai ametamani sukari iendelee kuadimika na bei yake kuwa juu ili matumizi yake yapungue kwa jamii kutoka na madhara ya bidhaa hiyo kwa mwili wa binadamu.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam wakati wa semina kwa waandishi wa habari iliyolenga kuelimisha juu ya magonjwa yasiyoambukizwa, Profesa Swai ambaye ni daktari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alisema matumizi ya sukari ni moja ya kichocheo cha magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari na shinikizo la damu.

“Kwa upande wa sekta ya afya, tunaona ni vizuri sukari kuadimika, na ndio maana nchi kama Uingereza inapandisha bei ya sukari kuanzia mwakani ili kudhibiti matumizi makubwa ya sukari. Hivyo kuongeza bei ni njia mojawapo ya kuzuia watu wasitumie,” alisema.

Hata hivyo, alisema anatambua kuadimika kwa sukari nchini hakutokani na sababu za kiafya, lakini ni vyema serikali kuiga hatua kama ya Uingereza na nchi zilizoendelea za kupandisha bei vitu vinavyochangia magonjwa yasiyoambukiza kama sukari, tumbaku na vileo.

“Ningependa liwepo ongezeko la bei kwa bidhaa kama sigara na vinywaji vilivyoongezewa sukari, ili kupunguza matumizi yake kwa jamii,” alisema. Magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni pamoja na moyo na shinikizo la damu, figo, saratani, kifua sugu, kisukari, magonjwa ya akili na mengine ya kurithi kama vile selimundu.

Chanzo: Habari leo
 
Hawa ndio madaktari wasiojielewa.
“Kwa upande wa sekta ya afya, tunaona ni vizuri sukari kuadimika, na ndio maana nchi kama Uingereza inapandisha bei ya sukari kuanzia mwakani ili kudhibiti matumizi makubwa ya sukari. Hivyo kuongeza bei ni njia mojawapo ya kuzuia watu wasitumie,” alisema.

Hivi utaifananishaje Taifa la Uingereza na nchi ya Tanzania ambapo mlo tu wa siku unasumbua, CCM na sirikali yake ikishindwa kuwapa hao watanzania masikini maisha bora wanayoyahubiri kila siku huku wao wakiota vitambi kwa ufisadi.?
SHAME dokta mwendokasi.
 
Prof umefanya utafiti kweli ujue watu wamehamia kwenye juice bandia ambazo ni hatari sana labda nazo ziadimike tule machungwa ya muheza
Au tule miwa mkuu.maana kila kitu kina madhara nowdays
 
Hawa ndio madaktari wasiojielewa.
“Kwa upande wa sekta ya afya, tunaona ni vizuri sukari kuadimika, na ndio maana nchi kama Uingereza inapandisha bei ya sukari kuanzia mwakani ili kudhibiti matumizi makubwa ya sukari. Hivyo kuongeza bei ni njia mojawapo ya kuzuia watu wasitumie,” alisema.

Hivi utaifananishaje Taifa la Uingereza na nchi ya Tanzania ambapo mlo tu wa siku unasumbua, CCM na sirikali yake ikishindwa kuwapa hao watanzania masikini maisha bora wanayoyahubiri kila siku huku wao wakiota vitambi kwa ufisadi.?
SHAME dokta mwendokasi.
Wewe hujui madhara ya kisukari wewe!
 
Hakuna anaeshinikiza kwamba sukari ni moja ya mahitaji muhimu, hebu soma vizuri huyo dk alichosema,..

Basi mgeni, hujui kama ukosefu wa sukari ni hoja ya wapinzani bungeni? Panua uwanja wa kufikiri sio kuzunguzia alichokisema Dr tu. Fikiria umplications and trends to the general public.
 
Sukari ni sumu. Anaeshinikiza kua sukari ni moja ya mahitaji muhimu anapotosha kwa makusudi. Maisha bila sukari yanawezekana.

We ndo unapotosha watu toka lini sukari ikawa Sumu au kwa vile una kisukari ndo useme maneno hayo,Tambua kuwa kama wewe hupendi kuna watu wanapenda kama wewe hutumii wapo watu wanatumia kwako inaweza kuwa sumu ila kwa wengine ni dawa
 
We ndo unapotosha watu toka lini sukari ikawa Sumu au kwa vile una kisukari ndo useme maneno hayo,Tambua kuwa kama wewe hupendi kuna watu wanapenda kama wewe hutumii wapo watu wanatumia kwako inaweza kuwa sumu ila kwa wengine ni dawa


Tuna safari ndefu sana watanzania. Magufuli na majaliwa endeleeni kudhibiti hii tamtam kiaina kuna wati wanabisha kua si sumu.
 
Basi mgeni, hujui kama ukosefu wa sukari ni hoja ya wapinzani bungeni? Panua uwanja wa kufikiri sio kuzunguzia alichokisema Dr tu. Fikiria umplications and trends to the general public.
Akili yako na wewe kama nyumbu tu, wewe umemskiliza nani kama si Drs wakisema kwamba sukari ni sumu. sasa hivi unajikana tena mwenyewe.
Ni upuuzi kukana kile unachokisema na kutaka kuniaminisha.
 
Akili yako na wewe kama nyumbu tu, wewe umemskiliza nani kama si Drs wakisema kwamba sukari ni sumu. sasa hivi unajikana tena mwenyewe.
Ni upuuzi kukana kile unachokisema na kutaka kuniaminisha.

Huu mchezo hautaki hasira... soma vizuri unaelewa. Maisha bila sukari yanawezekana, hatuhitaji sukari tunahitaji maendeleo meaning huduma bora ikiwapo ya afua na elimu na maarifa. You are a loving example of lack of education or knowledge or both. Do you know how sugar is processed in your body? Do you know its fate? Do you know its effects? Take a chill pill.
 
Huu mchezo hautaki hasira... soma vizuri unaelewa. Maisha bila sukari yanawezekana, hatuhitaji sukari tunahitaji maendeleo meaning huduma bora ikiwapo ya afua na elimu na maarifa. You are a loving example of lack of education or knowledge or both. Do you know how sugar is processed in your body? Do you know its fate? Do you know its effects? Take a chill pill.
Tunajua matumizi ya sukari yakizidi si nzuri kwa afya, so usinambie maisha bila sukari yanawezekana.
Na kuandika kiingereza siyo kwamba your so smart or intelligent or both.
 
Back
Top Bottom