Luis Figo amtaka Ifantino kujiuzulu

Luis Figo amtaka Ifantino kujiuzulu

Miss Halima

Senior Member
Joined
Aug 4, 2026
Posts
170
Reaction score
382
Gwiji wa soka duniani, Luis Figo, ametoa mashambulizi makali dhidi ya Rais wa Shirikisho la Soka la Duniani (FIFA), Gianni Infantino, akimtaka aondoke madarakani mara moja akidai uongozi wake umeathiri heshima ya taasisi hiyo kubwa ya soka. Mchezaji huyo wa zamani wa Ureno amedai Infantino amekuwa akifanya uamuzi unaolenga zaidi maslahi yake binafsi kuliko kulinda maslahi ya soka duniani.

1786014558842.png

Luis Figo

Figo amehoji kwa nini mipango mikubwa inayohusu mabadiliko ya kifedha ndani ya FIFA haikuwekwa wazi kwa wanachama wote kabla ya Fainali za Kombe la Dunia, akisema kama ilikuwa na manufaa makubwa ilipaswa kujadiliwa kwa uwazi.

1786013848774.png

Rais wa FIFA, Gianni Infantino
Soma
 
Bora hata ya Sepp Blater. Pamoja na mapungufu yake lakini alihakikisha FIFA kinakuwa ni chombo huru. Huyu Infantino ameigeuza FIFA kuwa chombo chenye double standard.

Mfano Urusi imefunguwa kushiriki mashinano yote ya FIFA baada kuivamia Ukraine mwaka 2022! Cha kushangaza Israel ilipoivamia Gaza 2023 na kusababisha mauaji ya watu zaidi ya elfu 70, FIFA hiyo hiyo imetulia kimya, kama haipo vile.
 
Back
Top Bottom