tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Mgombea wa Ubunge Jimbo la Bukene kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM )John Luhende, ameendelea na kampeni za kunadi sera kwenye jimbo hilo, akisema endapo atachaguliwa atatatua changamoto zinazoikabili sekta ya elimu, ikiwemo uhaba wa madawati mashuleni kwa kutumia rasilimali misitu inayopatikana katika Mkoa wa Tabora
Luhende ameyabainisha hayo wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Kata ya Itobo iliyopo Jimbo la Bukene, Wilayani Nzega Mkoani Tabora, akisema kuwa kutokana na uwepo wa Misitu Tabora atatumia fursa hiyo kuvuna magogo kwa mujibu wa sheria na kutengeneza madawati kwaajili ya wanafunzi.
Soma pia: John Luhende ashinda kura za maoni ubunge wa Jimbo la Bukene
"Na sisi hatuwezi kuwa tunahangaika madawati lakini jimbo letu la Bukene lina mapori ndani yake, nikiwa kiongozi naenda kuhakikisha hakuna Mwanafunzi anakaa chini ndani ya jimbo hili la Bukene" Luhende alisema .
Aidha, katika sekta ya nishati ya umeme, amesema kuwa licha ya serikali kusambaza umeme kwenye maeneo mengi Jimboni humo, kuna baadhi ya maeneo bado hajafikiwa na huduma hiyo hivyo atahakikisha anafikisha umeme ili wananchi waweze kunufaika katika shughuli mbalimbali za kiuchumi .
Luhende ameyabainisha hayo wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Kata ya Itobo iliyopo Jimbo la Bukene, Wilayani Nzega Mkoani Tabora, akisema kuwa kutokana na uwepo wa Misitu Tabora atatumia fursa hiyo kuvuna magogo kwa mujibu wa sheria na kutengeneza madawati kwaajili ya wanafunzi.
Soma pia: John Luhende ashinda kura za maoni ubunge wa Jimbo la Bukene
"Na sisi hatuwezi kuwa tunahangaika madawati lakini jimbo letu la Bukene lina mapori ndani yake, nikiwa kiongozi naenda kuhakikisha hakuna Mwanafunzi anakaa chini ndani ya jimbo hili la Bukene" Luhende alisema .
Aidha, katika sekta ya nishati ya umeme, amesema kuwa licha ya serikali kusambaza umeme kwenye maeneo mengi Jimboni humo, kuna baadhi ya maeneo bado hajafikiwa na huduma hiyo hivyo atahakikisha anafikisha umeme ili wananchi waweze kunufaika katika shughuli mbalimbali za kiuchumi .