Yaani katika purukushani za migomo ya walimu na wafanyakazi,harakati za kuandika katiba mpya,mfumuko wa bei, Wanavyuo wanaokosa mikopo licha ya kuwa na vigezo, usafirishaji haramu wa nyara za serikali, mafuriko ya jangwani, wizi kwenye nguzo za umeme, polisi kutumia nguvu kubwa kutekeleza sheria, kuongezeka kwa vyakula, dawa na bidhaa feki sokoni,
Mgogoro wa Tanzania Vs Malawi, benki kuwa na riba kubwa isiyowanufaisha masikini, miundombinu hovyo vijijini,mabadiliko ya hali ya hewa, usiri katika mikataba ya madini n.k
Ukiona mbunge wako ana machache ya kuihoji serikali kati ya makubwa niliyoyataja hapo juu, basi ujue pengine ni mgonjwa kama Mwandosya, au ulimchagua kwa kuwa alikuhonga kanga/t-shirt au kofia au alipita kwa kuchakachua!