Lowassa kupigwa chini tena





Apigwe chini na watanzania wengi kwenye sanduku la kura na si watu wachache kujifungia kwenye kichumba na kuzuia ndoto ya mtu. Ndoto ya Lowassa ni kuwa siku moja awe Rais kwa ridhaa ya watanzania na alikuwa amejipanga hivyo.
Kujitoa ccm ambako ndoto hiyo ilitaka kuzuiwa ni ujasiri na fundisho kwa wanasiasa wachanga kuwa chama hakiwezi kuwa ndiyo msingi wa kuwa kiongozi wa watu.
CCM imezima ndoto nyingi sana za viongozi bora na badala yake wanatuletea watu ambao mwisho wa siku hawana kitu kichwana na kila wanapopewa madaraka hawawatumikii wananchi.
Lowassa ni jasiri na atabaki kuwa hivyo katika vitabu vya historia, na Mungu kama atamjalia kushinda itaandikwa historia mpya ya siasa za Tanzania na atastahili medali ya shujaa wa karne Tanzania aliyepitia magumu mengi ndani ya chama chake.
Lazima tukubali kuwa pamoja na wanachama wa ccm kutopendezwa na uamuzi wake lakini lolote linaweza kutokea ashinde au ashindwe anastahili kupongezwa na vijana kwa kuwa amekuwa mfano mzuri.
ccm si tiketi pekee ya kuwa kiongozi, vijana tafuteni uongozi kupitia vyama vingine kama CHADEMA, NCCR, CUF, ACT-Wazalendo na vingine badala ya kuwa wapiga debe wa ccm amabayo hata wakifanikiwa kushika madaraka mnasahaulika!
 
Hivi mbona ukiwa wanalia sana ccm kutumia logo yao ya M4C, mbona hao hao ukiwa waliiba wimbo wa ccm wa tunaimani na magufulii na sikusikia ccm hata mmoja akilalamika, by the way hiyo logo mlikatia hati miliki?
...Ila hizo ni dalili ya kukata tamaa kwa wana ukiwa
 
Umejiunga august ili kula Posho za bure kwa kila pumba unayoandika !!
 
hawa wakiwa wakiwa siju mikia vile....wakileta vurugu maji ya washa washa yapo!! Vikosi vya ulinzi na usalama vya tanzania vipo vizuri na makini....wako peace sana ila usivichokonoe!!! Fujo hakuna...ukiwa sasa hivi wameshakata tamaa!!!

duuuu akili hizi sijui ugumu wa maisha hata haki yako ww utaogopa kudai kisa polis na maji ya kuwasha mwanaume mwoga ni sawa na kuku anaeumwa mdondo
 
​ccm kweli mazuzu ndiyo maana hawaoni aibu kwa kuiga m4c
 
Zilipendwa hizi, wanaoamua sasa ni wananchi wapenda mabadiliko na si kamati
 
nimeipenda hiyo M4C ya sasa 'magufuli for change' wasilalamike huu wizi mzuri wao mbona wameiba vingi tu. aliselema mchakamchanga vitu mingi tu. ila makapi wachukue tu hatulalamiki.
 
Lowassa hawezi akawa rais,rais ni Magufuri

Huu ndo ukweli. Watu wanaomiminika kwenye kampeni za Lowasa hawafiki hata laki 3 kila mkoa na hao wote si wapiga kura wake. CCM wana wapiga kura hadi vijijini ambaklo upinzani hata haujulikani kabisa. Naongea na mtu wa Mwanga huko Kilimanjaro anasema huko ni CCM tu. Naongea na mtu wa Mpwapwa Dodoma nako ni CCM tu na Lowasa hakufika huko kufanya kampeni. Kwahiyo CCM wamewafikia wapiga kura karibu wote nchi nzima. Ushindi ni mweupee kwa Magufuli.
 

Mgomo umeisha na mmeshalipwa hela zenu?
 

WASHAANZA MAZOEZI; WATATUUA KAMA SERIKALI ISIPOWAZIBITHI
 


WASHABIKI; THUBUTU KUKUTWA
 
CCM Mtabaki mnasema lowasa ikifika cku ya uchaguz wakati wa kupiga kura utajikuta umeshampigia kura kwa kuwa mmezoea jina lake
 
Wakiwa bhana wanachekesha sana, yani kila mtu mwenye mtazamo tofauti na wao anakula posho😬😬 Mkishika dola si ndo mtafuta mfumo wa vyama vingi kabisa? Hii nchi kila mtu ana uhuru wa kukiunga mkono chama chochote cha siasa msitulazimishe wote kuwa manyumbu, kha...
 
hawa wakiwa wakiwa siju mikia vile....wakileta vurugu maji ya washa washa yapo!! Vikosi vya ulinzi na usalama vya tanzania vipo vizuri na makini....wako peace sana ila usivichokonoe!!! Fujo hakuna...ukiwa sasa hivi wameshakata tamaa!!!

Ningependa siku iyo nimuone lowasa mstari wa mbele kama alivyokua anafanya Dr slaa
 
Hivi tuwe wakweli nani anaye isoma namba ya mwenzake kati ya ccm na ukawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…