Lowassa avamia mikutano ya CHADEMA Monduli

Lowassa avamia mikutano ya CHADEMA Monduli

THINKINGBEING

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2010
Posts
2,779
Reaction score
1,304
Katika hali ya kushangaza mbunge wa Monduli mh.Edward Lowassa ameingilia ratiba ya mikutano iliyopangwa kwa ajili ya kampeni za serikali za mitaa na kufanya mikutano ya chama chake maeneo ambayo CHADEMA ilipaswa ifanye mikutano.

Leo katika kijiji cha Losirwa kilichopo kata ya Eslalei vijana wa CHADEMA walishtushwa kuona CCM wakivamia na kuanza kufunga vyombo na vifaa vya kampeni kwenye eneo walilokuwa wakiliandaa kupigia kampeni kwa madai kwamba mbunge ndiye anayekuja kuhutubia huku wakijua fika kwamba ratiba haiwaruhusu.

Viongozi wa CHADEMA walipolifikisha suala hili kituo cha polisi Mto wa Mbu OCS wa kituo hicho alijaribu kuwasiliana na mtendaji wa kata na mtendaji wa kijiji ambao wote waligoma kutoa ushirikiano kwa madai kwamba wapo wilayani Monduli.Hata hivyo viongozi hao wa CHADEMA walishangazwa sana na kauli ya OCS huyo kwamba mbunge ana haki ya kufanya mikutano bila kujali ratiba.

Juzi pia mh. Lowassa aliingilia ratiba ya mkutano wa CHADEMA uliokuwa ufanyike Mto wa Mbu na hivyo CHADEMA kulazimika kutumia siku iliyofuata ambayo ilikuwa ndiyo ya CCM katika ratiba. Uongozi wa CHADEMA wilaya ya Monduli tayari umeshafikisha malalamiko katika ofisi ya mkuu wa wilaya leo kuonesha kutoridhishwa kwake na jinsi mbunge huyo anavyokandamiza demokrasia wilayani Monduli.

Mbunge huyo anahaha kukinusuru chama chake wilayani Monduli baada ya chama hicho kuzidiwa nguvu na CHADEMA wakati mbunge huyo alipokuwa nje ya nchi.

Wiki iliyopita pia uongozi wa CHADEMA wilaya ya Monduli uliiandikia ofisi ya mkuu wa wilaya barua inayoelezea njama na hujuma zinazopangwa juu ya viongozi na wagombea wa CHADEMA wakati huu wa uchaguzi wa serikali za mitaa.
 
Hili suala tutalishughulikia jumatatu,vuteni subira.
 
Jamani huyu Lowassa apumzike kwake pale Ngarash ajiangalie maradhi yake, anahangaika nini!
 
Kwa kwenda ofisi za serikali kushitaki mjue siku zote mtapotezewa ,wala hamna haja ya kuripoti makao makuu ya Chama ,ila kitu kimoja ni just kuweka taarifa ya kinachojiri huko ,polisi na hata makao makuu ya chama '

Iwapo mna uhakika kuwa siku ni yenu ya kufanya mkutano hapo na stakabazi zote mnazo basi kinachotakiwa ni kwa nyinyi nanyi kufunga vyombo vyenu ,tena mjizatiti kikwelikweli kwa liwalo na liwe ,mambo ya kwenda kushitaki yamepitwa na wakati ,ifike wakati wanaoshitaki wawe miccm na sio upinzani na wakati ni huu.Haki yenu haitaletwa na kupewa ndani ya sinia na sahani ,inatakiwa muilinde na muichukue kwa hali yeyote ile. Mlete habari kuwa mumefanikiwa kuilinda na sio mmekimbilia vyombo vya serikali,serikali ambayo ni miccm ,mpo ,kazeni buti mpaka kieleweke.
 
wangemkimbiza mtu mwenyewe hawezi kukimbia Lowassa amerudi lini kutoka kwenye matibabu ujerumani
 
Waacheni warukeruke tu kama maharage chunguni,wakiiva watatulia tu!
 
laki si pesa ni kibiko, yaani ana habari za Tz nzima.... hii inaonyesha huyu ni kibaraka tu mdaka tonge alie kwenye mitandao kutetea magamba hata kama hana data na hata kama taifa linafisadiwa.....

Monduli nakujua wewe kuanzia kisongo, duka bovu , lekisale, losimingori, waya , tma, chuo cha ualimu, huwezi kunidanganya dogo
 
Mwiba
usirogwe hata siku moja kwenda kuishitaki ccm polisi au kwenye ofisi yoyote ya umma, we wakikuchezea jipange kata mtu panga wao ndio wakashtaki wanabebwa sana kama mademu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom