Lowasa hazina ya CCM 2015

Lowasa hana jipya, anataka aingie madarakani ili wajilinde mafisadi... Asubiri tu kuning'inizwa na Rais ajae. Alipewa nafasi ameshindwa kuitumia....ni hivi anavyoutafuta kwa nguvu atakuwa kama swahiba wake tu. Ila hii nafasi hataipata kamwe.


"Ukiona mtu anaogelea baharini usiku ujue ana ajenda na vibwengo"
 
Huo ndio ukweli. Lowassa ni Kagame wetu 2015.God bless EL.
Kwa kipi cha kumfananisha, bado mnafikria 2naishi kama miaka hiyo, we are watching the movie prety soon u will c the changes!
 
hiyo mashine ya ukweli sana ila watu waliofanya madudu ndani ya chama ndo hawataki wnataka wabaki wao na baba zao
 
Sitegemei kama anaweza kufika uko kote, kwa sasa Jamaa wamembana sana, but also Umri umemtupa mkono.
kunamambo mengi yamejifisha nyuma yake na yeyemwenye anajua. but siwezi kusema nisije kula burn apa.
 
Huo uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi ameupata wapi? Tatizo letu ni kukubali kununuliwa!!!!!
 

Duuu!! Watu mnakazi kweli, hivi ni kiasi gani cha fedha mnalipwa kwa kazi hii?

Watanzania hawaishi nje ya tanzania wanafahamu sana kama EL anafaa au la, alihusika na ufisadi au la, ni msafi au laa. kwa nini mnajisumbua kiasi hicho wandugu wapendwa.

Mimi ningekuwa EL ningewambia wote wanaofanya kazi hii waache maana watamfanya sasa watz washtuke na wamchukie bure. kama anafaa jamani si tunamfahamu...? Mtu aliyeshika nafasi kubwa kama yeye kuna ambaye hamfahamu.. Hapa ni sawa na kuwaambia watz kuwa uchumi wa tz unapaa wakati wote tunaishi tz tunachopata tunajua km uchumi unapaa au ni bora au la, kila mmoja unamgusa kivyake... mambo haya yanachosha sana...
 
Hazina ya baba yako, acha kusababisha watu kubaniwa hapa
 
Najua bado mna matumaini ya kuwa watanzania ni wajinga kiasi kwamba unaweza ukawaletea limao na ukawashawishi ni chungwa wakakubali, well labda kweli mtawapata watu wa dizaini hiyo, lakini nikuhakikishie mnachofanya ni kusababisha Lowasa achukiwe zaidi, moja ni kwa sababu anawafanya watanzania ni wajinga, anafikiri anaweza kutumia ujinga wao katika kupata urais.

Lowasa ana ufisadi mwingi utakaomfanya ashindwe kufanya hayo maamuzi magumu iwapo atakuwa rais, wewe unafikiri ni kwa nini Kikwete anashindwa kuwashugulikia mafisadi Lowasa akiwemo, ni kwa sababu na yeye anahusika kwenye huo ufisadi, anaogopa akimshugulikia yeyote kati ya hao mafisadi watamuumbua na yeye. Tukiweka rais kama Lowasa itakuwa mwendelezo wa hayohayo.
 

Ni mtaji na ni hazina yako wewe. Sababu ni moja tu, na wewe ni fisadi mwenza.
 
Mungu atatoa jibu dkk ya 90!Zngne hapa ni mbwembwe tu
 
kwani kageme ndo unaona raisi wakumfananisha na maraisi duniani??
LOWASA ni jambazi tuuu!


Mkuu ukiangalia hao watu wote wanaomsifia Lowassa utaona wamejiunga mwaka huu au mwaka jana, na ukiangalia kwa undani utaona ni mtu mmoja. Ukiwauliza swali ni kwanini lazima Lowassa awe rais 2015? ana nini cha kuifanyia Tanzania? kwa kipi alichoifanyia Tanzania? utaona wanavyojikanyaga.
 

acha ujinga wewe ni mawazo yake hayo!

kwani wewe umenunuliwa na nani kusema haya uliyoyaandika?
 

Du, hata pumba za nguruwe zina afadhali, yaani mtu mzima na akili zako unaandika utumbo!
 
Lowasa sio rais 2012. Dhambi yake ipo mbele za mungu na 41m watanzania wanahaha kwa sababu yake pesa zake mwisho uwaziri mkuu. Pole sana.
 
LOWASA mm cmkubali,anataka urais akijua uovu wake utatambuliwa nayeye kufilisiwa, kama alishindwa ujanana na cheo kidngo kama kile ataweza urais?
 
Duh kweli rais hatuna yaani 2012 watu wanahoji ya 2015 my gosh we should hav to focus on geting the perfect 1 ili mda kama huu tunakua tunapeana raha tu jamvini kutokana na deliverties za mr president.....
 
Kwani tuna watendaji wengi wazuri wapo na sio LOWASA peke yake, Kiongozi ni wajibu wako kusimamia na kuongoza walio nyuma yako. Ukishindwa kufanya hivyo, wewe sio Kiongozi bora kwani ndiyo= Lowasa alishindwa kusimamia mali ya serikari chini ya uongozi wake kama Waziri Mkuu. Nchi na Wananchi wamepoteza Fedha na mali nyingi kwa wachache akiwemo yeye mwenyewe kwa kupitisha mikataba hewa.Huyo sio Kiongozi mzuri wakuweza kupewa Nchi, atauza Nchi na Wanachi wake akijali manufaa yake mwenyewe na familia yake.
Pili, hao Viongozi wa dini wanao muunga mkono! Nashindwa kuwaelewa kwani kazi yao kubwa ni kuhakikisha kuwa Wanadamu wapatiwa haki na mahitaji yao ya kibinaadamu. Inapofikia hatua ya Viongozi wa dini kupokea fedha kutoka kwa wanyonyaji wa jamii ambao ni waumini wao, hii inaonyesha hata dini siyo dini tena ila ni vituo vya kisiasa vinavyo tumikia Wezi wa Jamii kama akina Lowasa na RA. Wewe unayemtaka Lowasa kugombea, amisha kununua kwa kiasi gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…