Lowasa au zitto 2015

Lowasa au zitto 2015

Sassebossa

Member
Joined
Jan 13, 2013
Posts
27
Reaction score
3
Wanajamvi,
Leo nataka niwajadili viongozi wawili shupavu,wenye muono wasio na masikhara katika utendaji kazi wao!!

Kwanza ni mh. Edward Lowasa,mbunge wa Monduli na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania. Mzee huyu pamoja na kuhusishwa na scandle ya Richmond,bado anaonekana ndani ya CCM huyu ndiye angalau anaweza kupambana na mikikimikiki ya Urais. Kimsingi mpaka leo huwa najiuliza ni kwa nini vyama vya upinzani vilishadidia sakata la Richmond kwa Lowasa badala ya Kikwete mwenyewe! Ni nani asiyejua uhusika wa JK ktk Richmond?
Watanzania tuwe makini! Lowasa anakumbukwa kwa ushupavu wake ktk uongozi wake. Tumuunge mkono mzee wetu!

ZITTO KABWE: Kijana huyu hodari wa kufukunyua uozo na muonesha njia ya mabadiliko ktk uongozi,amekuwa muhanga wa siasa za udini na ukabila tangu alipotaka kugombea uenyekiti ndani ya chama chake cha CHADEMA. Kimsingi,kijana anauwezo wa hali ya juu sana wa kuliongoza taifa hili. Tofauti na katibu mkuu wake(SLAA) mwenye exposure ya kidini kwa kiasi kikubwa,ZITTO ZUBERI KABWE ni hodari katika mambo mbalimbali huku akitumia ujana wake kwenda nje kujifunza namna viongozi wa nchi mbalimbali walivyopambana kukwamua nchi zao ktk umasikini.
Kijana huyu,kama katiba ikimuruhusu,CHADEMA msitunyime haki watanzania ya kupata Rais ambaye sasa ndo mkombozi wetu!
Nahitimisha kwa kusema,kama Chadema wataendekeza ukabila wakati katiba imemruhusu ZITTO,na wakati huo huo CCM wakakumbuka kumkabidhi Lowasa bendera ya kijani,kwa mara ya kwanza CCM itachukua kura yangu.
 
Hivi bado kuna watu wanaamini kuwa Lowasa alionewa kama huyu mtoa post hii? Inashangaza! Na bado anaihusisha CDM na udini. Majitu kama haya yanayotulea tujadili udini hapa jamvini tuyaogope kama ukoama....
 
M23 at work, tulisha wasahau, hata huyo manye mtetea alisha wasahau siku nyingi sana
 
Duh! Hii ndio post yangu ya kwanza kuanza kusoma leo sijui ni balaa gani hili, ngoja nirudi kitandani ili nikiamka nianze siku upya tena maana hapa nishavuruga.
 
Hivi bado kuna watu wanaamini kuwa Lowasa alionewa kama huyu mtoa post hii? Inashangaza! Na bado anaihusisha CDM na udini. Majitu kama haya yanayotulea tujadili udini hapa jamvini tuyaogope kama ukoama....
Huyu ni mpiga debe njaa wa Lowasa. Na ndiye (Lowasa) amemshauri aje ampigie debe hapa. Si unajua tena njaa haijali umri
 
kwani lowasa anahusishwa na kashfa ya richmond pekee? zipo nyingine. katka ccm wapo watu safi wengi na wenye uwezo mzuri wa kuongoza. mbona tunaacha hao na kukomalia mtu ahusishwaye na madudu mengi? tukitaka tanzania dhaifu zaidi, chafu zaidi, shaghala baghala zaidi, kimeo zaidi, ya ovyo zaidi, etc tumpe uraisi mtu fisadi.
 
wanao sema hadharani "nautaka uraisi" "sigombei ubunge 2015".
inatakawa waliwe pesa zao alafu wafanyiwe 'surprise' kwenye kura za maoni za vyama vyao.
 
Wanajamvi,
Leo nataka niwajadili viongozi wawili shupavu,wenye muono wasio na masikhara katika utendaji kazi wao!!

Kwanza ni mh. Edward Lowasa,mbunge wa Monduli na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania. Mzee huyu pamoja na kuhusishwa na scandle ya Richmond,bado anaonekana ndani ya CCM huyu ndiye angalau anaweza kupambana na mikikimikiki ya Urais. Kimsingi mpaka leo huwa najiuliza ni kwa nini vyama vya upinzani vilishadidia sakata la Richmond kwa Lowasa badala ya Kikwete mwenyewe! Ni nani asiyejua uhusika wa JK ktk Richmond?
Watanzania tuwe makini! Lowasa anakumbukwa kwa ushupavu wake ktk uongozi wake. Tumuunge mkono mzee wetu!

ZITTO KABWE: Kijana huyu hodari wa kufukunyua uozo na muonesha njia ya mabadiliko ktk uongozi,amekuwa muhanga wa siasa za udini na ukabila tangu alipotaka kugombea uenyekiti ndani ya chama chake cha CHADEMA. Kimsingi,kijana anauwezo wa hali ya juu sana wa kuliongoza taifa hili. Tofauti na katibu mkuu wake(SLAA) mwenye exposure ya kidini kwa kiasi kikubwa,ZITTO ZUBERI KABWE ni hodari katika mambo mbalimbali huku akitumia ujana wake kwenda nje kujifunza namna viongozi wa nchi mbalimbali walivyopambana kukwamua nchi zao ktk umasikini.
Kijana huyu,kama katiba ikimuruhusu,CHADEMA msitunyime haki watanzania ya kupata Rais ambaye sasa ndo mkombozi wetu!
Nahitimisha kwa kusema,kama Chadema wataendekeza ukabila wakati katiba imemruhusu ZITTO,na wakati huo huo CCM wakakumbuka kumkabidhi Lowasa bendera ya kijani,kwa mara ya kwanza CCM itachukua kura yangu.

Wengine hatujui Kikwete alihusika je? Mbona Lowasa hajamtaja kama alihusika wakati aliulizwa kama siye amtaje mhusika na hakufanya hivyo! tuambie alihusikaje maana wengine hatujui!!
 
Mi ni cdm dam bt akipewa zito kupeperusha bendera kura yangu ntaigawa kwa yeyote.
 
Ukiona mtu anataka uraisi na anapita akitumia Pesa basi aogopwe Kama Ukoma(Julius Nyerere in Mbeya May Day 1993)
 
Back
Top Bottom