Hiyo ndio inaitwa "Coordination"...miguu haiwezi enda kama hakuna macho ya kuiongoza....vivyo hivyo kama yasingalikuwa macho labda yangalikuwa masikio yamesikia sauti nzuri ya kumtoa nyoka pangoni...
Uamuzi wa halali hukumu iso hatia, itakuwa ni muhali kimoja kukionea laumu vyote viwili usilaumu kimoja,,..
jicho ndilo la awali mashaka kukuletea, moyo ukawa wa pili mashakani kukutia adui hawa wawili walaumu wote pia
Bila Macho kuona Moyo ungependa vipi? Nafikiri Macho yaliona, Moyo ukapenda, Akili ikatamani hivyo unaweza kuilaumu tabia yako ya tamaa! Nasema hivi maana kazi ya Macho ni kuona, na kazi ya Moyo ni kupenda, lakini tamaa ni tabia ya mtu na waweza kuirekebisha kwa kuamua kuridhika!:becky: