LIVE: Tamasha la Matumaini

LIVE: Tamasha la Matumaini

Governor of Bettors-GB

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2013
Posts
10,768
Reaction score
9,942
Mie binafsi napenda sana kuwashkuru AZAM Tv kwa kurusha Live Tamasha la Matumaini.
Ni matangazo ya ubora wa hali ya juu sana.
Mechi zimeisha Za Bongo movie na maswahiba zao,wabunge wa Simba na Yanga,Sasahivi tunaona AZAM FC ambapo wachezaji wengi ni Timu B maana A wapo Rwanda wanacheza na Mtibwa Sugar hawa watatumia all 90 minutes.

Kabla ya Mechi hiyo Sir Nature alifunika na bado kuna wasanii kibaoo nimeona kwenye Screen wakiwa Sehem yao wakisubiria zamu zao za makamuzi.

Wapenzi wa Ngumi nikwamba Thomas Mashali anazicha na Mada Maugo .Hapa ndio silali mpaka nione hawa jamaa leo inakuwaje maana wanatambiana sana.

Sijui kama AZAM isingekuwepo Tamasha kubwa kama hili Africa Mashariki lingeoneshwa na nani.Lakini hapa sie tuliombali tunaona kila kitu kwa murua kabisa.

Nitaendelea au tutaendelea kuwapa Updates wale ambao hawatumii AZAM Decorders.

JAZAKALLAHU KHAIRAN BAKRESSA and All Staffs wameohusika katika kufanikisha Tamasha hili ili na sie wa mbali tuone.
 
Mussa Hassan Mgosi na Mwaikimba ndani.Wapenzi mnaweza kujikumbusha na kuangalia ubora wa wakongwe hao
 
Hayaa,katika soka la Sasa
Musa Hassan Mgosi Dakika ya 31 kipindi cha kwanza anaipatia Mtibwa bao la kwanza.
Mtibwa 1 - Azam 0
 
Duh mnaturusha roho wenye ving'amuzi vya serikali
 
Mpira ni mapumziko.
MAdee anakamua katika kipindi hiki timu zipi vyumbani.
Bonge la Shoo
 
Nilikuepo ndani ya uwanja nikashudia game ya Bongo Movie vs Bongo flavor, Bongo flavor wakaibuka na ushindi wa goli moja kupitia kwa Ali kiba. Sio Mbaya japo haikunifurahisha kama ya waheshimiwa wabunge.

Maana ilikua bonge la burudani kwa waheshimiwa kulishana kanzu tobo na magori mazuri,
Burudani zaidi ni baada ya kipyenga cha mwisho matokea kusomeka Yanga 3-2 Simba. Hongera sana kwa wanayanga wote.

Kilichoniuma sana kukuona Juma Nature akiwa vile alivyo pamoja na historia kubwa aliyonayo kwenye tasnia ya mziki Bongo..........
 
endeleeni kutupa updates za hilo tamasha kwani nasubiri habari za Simba ASIYEFUGIKA {mashali} vs Tembo {maugo}.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom