LOWASA KUHAMIA UKAWA ATAZUI GOLI LA MKONO:
Nadhani ni mwandishi wa kimarekani Cristoper Dikens kama sijakosea jina, wakati Marekani ikijiandaa kuishambulia Iraq ili kumuondoa Sadam madarakani mandishi huyu aliandika makala "The perils of victory" Kwa Kiswahili unaweza kusema hatari za ushindi. Kwenye makala hii alitahadharisha mambo ambayo yangetokea baada ya ushindi wa kijeshi wa marekani dhidi ya Sadam. Alitabiri karibu kila kilichotokea baadaye kuanzia the cilivil war hadi kugeuka kwa Iraq kuwa a save heaven kwa magaidi.
Si lengo langu kuijadili makala ile, nimechukua kichwa cha makala ile vile kinawiana sana na yanayoelekea kutokea kwenye siasa za Tanzania kwa sasa. Kuna fununu kwamba kada wa CCM Mh Edward Lowassa anaelekea ku hama chama chake na kujiunga na chama kikuu cha upinzani (CDM) na labda akapitishwa kugombea uraisi kupitia UKAWA.
Uchambuzi wangu kuntu unaniambia uwezekano wa Lowassa kushinda uraisi kupitia UKAWA ni mkubwa. Kwa nini! Wengi wanafikiria juu wa watu walioko nyuma yake lakini sidhani kama hilo ndilo lenye umuhimi wa kwanza. Kuna mambo kadhaa yanayompa Lowassa na UKAWA nafasi nzuri ya kuiangusha CCM.
CONNECTIONS ZA LOWASSA NDANI YA SYSTEM NA CHAMA Kushinda uchaguzi ni zaidi ya kuungwa mkono na watu, ni zaidi ya kupigiwa kura za kutosha. Uchaguzi ni kama vita na unapojipenyeza kwenye ngome ya adui yako na kujua anachopanga kufanya hakika una nafasi nzuri zaidi ya kushinda. Lowassa ana watu ndani ya system na CCM. Kuna watakaotoka naye iwapo atatoka (wana CCM) na kuna watakaobaki na kuendelea kumtumikia kichini chini wakiwa CCM, kuihujumu CCM toka ndani. Watu wake ndani ya system watasaidia sana kukabili juhudi wa system kuuhujumu upinzani. CCM na system iliyoko nyuma yake italazimika kupigana vita mbili kwa wakati mmoja, vita na upinzani wa wan je upande mmoja na upande wa pili itakuwa vita dhidi ya upinzani wa ndani. War on two fronts is the last thing strategist would wish for.
RASILIMALI FEDHA Ni wazi kuwa nyuma ya Lowassa kuna massive financial resources kulinganisha na kile ambacho CDM/UKAWA inaweza ku mobilize bila Lowasa. Rasilimali fedha ni muhimu sana kushinda uchaguzi, huu ni mchakato ghali sana ambapo uwezo wa kifedha una nafasi yake katika kuleta matokeo.
ORGANISATION Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni, 4u movement ilikuwa the best organised campaign within CCM, ilikuwa movement iliyoazima mbinu nyingi za kibiashara kufanya siasa, kosa kubwa lilikuwa ni kutokuweka msisitizo wa kutosha kwenye siasa yenyewe, siku nikiwa na nafasi nitalieleza hili kwa kina. Sasa organisation hii ikijumlishwa naya UKAWA itakuwa ni kikosi mahiri kabisa na tutaona mambo mapya kwenye kampeni za kisiasa. Sioni namna gani CCM inaweza kutengeneza timu ya kushindana na hii hapa.