Lissu kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA

Lissu kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2018
Posts
439
Reaction score
742
KAMANDA CECIL DAVID MWAMBE (CDM) NA SAFU MPYA CHADEMA

Habari kutoka kwa watu wa karibu wa Mhe Cecil David Mwambe mbunge wa Ndanda na Mkt wa kanda ya kusini ni kwamba amedhamiria kuisuka upya CHADEMA ambapo inasemekana akiibuka mshindi basi Katibu Mkuu wake atakuwa Mhe Tundu Antipas Lissu Huku John Heche akiwa naibu wake.

Inasemekana wapo wanachama wengi wenye uwezo wa kutoa mchango wao kwa chama lakini makundi na siasa za kikanda yaliwaumiza sasa ni wakati wao kuingia kuthibitisha uwezo wao.

Nafasi za mafunzo kwa chama ndani na nje ya nchi zilikosa program inayoeleweka na uwazi kwa wanachama hususani vijana na wanawake. Mwambe amedhamiria kufanya mageuzi.

Mapato yote ya chama yanaweza kuajiri maafisa na watendaji kuanzia makao makuu hadi kwenye majimbo pamoja na upatikanaji wa vifaa muhimu vya kutendea kazi ikiwemo ofisi, baiskeli, pikipiki, magari, computer, bendera, kadi na sare za chama.

Siasa imebadilika sana lazima tuwajengee uwezo vijana wetu ili wamudu mabadiliko ya teknolojia na kutumia maarifa hayo katika kusukuma mbele gurudumu la chama chetu.

Zipo fursa lukuki za kimafunzo na ushiriki wa matukio mbalimbali kutoka vyama rafiki bahati mbaya sana zimekuwa zikiwanufaisha watu wale wale. Ni muda viongozi wa majimbo, wilaya, mikoa na kanda kuanza kunufaika na fursa hizi.

Twende na CDM CECIL DAVID MWAMBE...

#Miaka15MboweInatosha #TwendeNaCDM #SimonMkirene
IMG-20191126-WA0030.jpeg
 
Mbowe bado yupo sana tu ndani ya cdm labda kama wewe ni mpiga kura utamkataa wewe pekee yako
Tunapinga viongozi wa kiafrika kukaa madarakani muda mrefu wakati huo huo tunamtaka mbowe aendelee kukaa madarakani. Are we mentally okay ?
Screenshot_20191125-162412.jpeg
 
Huyo Mwambe hakuna wa kumpatia kura ya kuwa mwenyekiti
Mwambe aliingia CHADEMA mwaka gani? Asije kurubuniwa na CCM. Watu wa Kusini siwaamini. Hawana msimamo thabit. Tumeona mwaka jana ktk korosho.
 
Kila mwenye sifa basi akitaka na achukue form kura za wajumbe zitaongea ndio democracy yenyewe.
 
Mwambe aliingia CHADEMA mwaka gani? Asije kurubuniwa na CCM. Watu wa Kusini siwaamini. Hawana msimamo thabit. Tumeona mwaka jana ktk korosho.
Watu wa KIGOMA na ARUSHA wanafiki sana sana hawaaminiki hata chembe
 
Mkuu habari za Msamvu , tangu lini wewe ulikuwa Chadema ? umechoka rushwa unazopewa na Abood?
 
Huyo jamaa hatofafautiani na mwita waitara
 
Hivi tarehe ngapi vile anahitajika mahakamani? Yule Pilato kasema msimletee siasa daah Sina hela ya kiroba inabidi nigongee ugoro...
 
Back
Top Bottom