BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Lipumba: Ufisadi ni matokeo ya utawala mbovu
2008-08-29 09:31:45
Na Dunstan Bahai
Matukio ya rushwa, ufisadi na nyufa mbalimbali zilizojitokeza kwenye Muungano, ni matokeo ya kuwa na viongozi wasio waadilifu, hekima na busara.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, kwenye kongamano lililoandaliwa na chama hicho jijini Dar es Salaam likiwa na lengo la kujadili ukosefu wa uongozi na hatma ya Tanzania.
Alisema uongozi usio adilifu na usio na dira wala kujiamini, hujenga matabaka kama ya mitandao.
Alisema matabaka hayo ndiyo yanayojikuta yakiishikilia nchi katika nyadhifa mbalimbali na hata mmoja wao akifanya madudu ni vigumu kumuengua, kwani kwa kufanya hivyo ni kukiuka makubaliano yaliyomo kwenye mtandao huo.
Kwa mujibu wa Profesa Lipumba, wanamtandao hao ndiyo chanzo cha matokeo mabaya ya utawala wowote duniani kwani maamuzi yao hawawashirikishi wananchi.
``Katika nchi inayokabiliwa na dimbwi la umaskini, na inataka kujenga demokrasia ya kweli, uadilifu ndiyo unapaswa kuwa msingi wa siasa, msingi wa maongozi ya siasa.
``Kuzungumzia uongozi na uadilifu katika siasa si jambo jepesi. Hisia na mitazamo ya watu wa kawaida kuhusiana na siasa, imekuwa ya kuihusisha fani hiyo na tamaa, ubinafsi, uroho, unafiki, ulaghai, upotovu, uovu, fitina, hiyana na hata hujuma. Tena si watu wa kawaida tu bali hata baadhi ya wasomi wetu wanaonekana kuiona hivyo,`` alisema Profesa Lipumba.
Alisema kutokana na hali hiyo, imechukua muda Watanzania kuamini kama mabadiliko yanawezekana hapa nchini ingawa alisema sasa wameamka na kuunga mkono jitihada za kuwepo kwa mabadiliko hayo.Profesa Lipumba, aliainisha mabadiliko 11 ambayo alidai Watanzania wanayahitaji.
Mabadiliko hayo ni yale yatakayowapa uongozi wa namna bora ya kutumia neema ya rasilimali zilizopo, yatakayomhakikishia kila Mtanzania anamiliki alau milo mitatu iliyotimia kwa siku na kuongeza kipato chake kupitia kazi halali na jasho lake na kuhakikisha gharama za maisha hazipandi kiholela.
Mengine alidai kuwa ni mabadiliko ya kupata huduma za msingi za afya zilizo bora na watoto kupata elimu bora ya msingi na sekondari, kupata maji safi na salama na miundombinu ya umeme na barabara iliyo imara na yatakayosafisha uozo wa ufisadi na rushwa na yatakayoleta uwajibikaji na utawala wa sheria.
Profesa Lipumba, alianisha mabadiliko mengine kuwa ni ya kujenga misingi imara ya umoja, udugu na mapenzi kati ya wananchi wenye imani tofauti za kidini, wa makabila, rangi na jinsia tofauti.
Mabadiliko mengine ni ya kutoa uhai mpya kwa Muungano na kuuimarisha uweze kukabiliana na changamoto mpya kwa kuhakikisha haki na usawa kati ya Tanganyika na Zanzibar na hivyo kuvutia nchi nyingine kujiunga.
Mwenyekiti huyo wa CUF alisema mabadiliko mengine ni yale yatakayowapa dira na mwelekeo mpya utakaolipeleka Taifa katika jamii itakayozingatia haki sawa kwa wote na yenye uchumi imara unaotoa ajira na tija kwa wananchi wote, uongozi makini, thabiti na wenye uzalendo wa kweli kwa Taifa lao.
Wakichangia kwenye kongamano hilo, Profesa Abdallah Safari, alisema maliasili zilizopo nchini haziwanufaishi wananchi wala Taifa kwa ujumla.Alisema hayo ni matokeo ya mikataba mibovu na kwamba upo wakati vijana watavamia kwenye migodi na maeneo mengine ya rasilimali zilizopo ili kunufaika nazo.
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Bw. Augustine Mrema, alisema hali kuwa mbaya nchini, ni ishara kwamba uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) umefikia kikomo kwa vile umeshindwa kuwafikisha Watanzania katika maisha bora waliyoahidiwa.
Alihoji sababu za Tanzania Bara kuing`ang`ania Zanzibar wakati ipo Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ambayo wanaweza kuungana nayo.
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw. James Mbatia, aliwataka Watanzania kufikiria kwa kina hali inayoikabili nchi hivi sasa kwani ikisambaratika hakuna atakayepona na akawataka pia watafute mbadala kwa madai kwamba walioko madarakani wameshindwa kuongoza nchi.
Mhadhiri wa Msikiti wa Idrisa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, Maalim Ali Bassaleh, alihoji taarifa zinazotolewa na serikali kwamba watu waliochota fedha katika Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wanazirejesha wakati hawakukopa wala kuwekesha amana.
``Hawa ni wezi. Wakamatwe na wafikishwe mahakamani,`` alisema Maalim Bassaleh.
Awali, akielezea madhumuni ya kongamano hilo, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, alisema walilazimika kuliandaa ili kutafakari na kuona nini la kufanya ili kuikwamua nchi ambayo alidai inapita katika kipindi kigumu kinachohatarisha hatma ya Watanzania.
Kongamano hilo lilihudhuriwa na wawakilishi kutoka balozi za Ufaransa na Marekani, taasisi za kijamii, vyuo vikuu, wabunge wa Jamhuri ya Muungano, Baraza la Wawakilishi na makundi ya watu wenye ulemavu.
SOURCE: Nipashe
2008-08-29 09:31:45
Na Dunstan Bahai
Matukio ya rushwa, ufisadi na nyufa mbalimbali zilizojitokeza kwenye Muungano, ni matokeo ya kuwa na viongozi wasio waadilifu, hekima na busara.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, kwenye kongamano lililoandaliwa na chama hicho jijini Dar es Salaam likiwa na lengo la kujadili ukosefu wa uongozi na hatma ya Tanzania.
Alisema uongozi usio adilifu na usio na dira wala kujiamini, hujenga matabaka kama ya mitandao.
Alisema matabaka hayo ndiyo yanayojikuta yakiishikilia nchi katika nyadhifa mbalimbali na hata mmoja wao akifanya madudu ni vigumu kumuengua, kwani kwa kufanya hivyo ni kukiuka makubaliano yaliyomo kwenye mtandao huo.
Kwa mujibu wa Profesa Lipumba, wanamtandao hao ndiyo chanzo cha matokeo mabaya ya utawala wowote duniani kwani maamuzi yao hawawashirikishi wananchi.
``Katika nchi inayokabiliwa na dimbwi la umaskini, na inataka kujenga demokrasia ya kweli, uadilifu ndiyo unapaswa kuwa msingi wa siasa, msingi wa maongozi ya siasa.
``Kuzungumzia uongozi na uadilifu katika siasa si jambo jepesi. Hisia na mitazamo ya watu wa kawaida kuhusiana na siasa, imekuwa ya kuihusisha fani hiyo na tamaa, ubinafsi, uroho, unafiki, ulaghai, upotovu, uovu, fitina, hiyana na hata hujuma. Tena si watu wa kawaida tu bali hata baadhi ya wasomi wetu wanaonekana kuiona hivyo,`` alisema Profesa Lipumba.
Alisema kutokana na hali hiyo, imechukua muda Watanzania kuamini kama mabadiliko yanawezekana hapa nchini ingawa alisema sasa wameamka na kuunga mkono jitihada za kuwepo kwa mabadiliko hayo.Profesa Lipumba, aliainisha mabadiliko 11 ambayo alidai Watanzania wanayahitaji.
Mabadiliko hayo ni yale yatakayowapa uongozi wa namna bora ya kutumia neema ya rasilimali zilizopo, yatakayomhakikishia kila Mtanzania anamiliki alau milo mitatu iliyotimia kwa siku na kuongeza kipato chake kupitia kazi halali na jasho lake na kuhakikisha gharama za maisha hazipandi kiholela.
Mengine alidai kuwa ni mabadiliko ya kupata huduma za msingi za afya zilizo bora na watoto kupata elimu bora ya msingi na sekondari, kupata maji safi na salama na miundombinu ya umeme na barabara iliyo imara na yatakayosafisha uozo wa ufisadi na rushwa na yatakayoleta uwajibikaji na utawala wa sheria.
Profesa Lipumba, alianisha mabadiliko mengine kuwa ni ya kujenga misingi imara ya umoja, udugu na mapenzi kati ya wananchi wenye imani tofauti za kidini, wa makabila, rangi na jinsia tofauti.
Mabadiliko mengine ni ya kutoa uhai mpya kwa Muungano na kuuimarisha uweze kukabiliana na changamoto mpya kwa kuhakikisha haki na usawa kati ya Tanganyika na Zanzibar na hivyo kuvutia nchi nyingine kujiunga.
Mwenyekiti huyo wa CUF alisema mabadiliko mengine ni yale yatakayowapa dira na mwelekeo mpya utakaolipeleka Taifa katika jamii itakayozingatia haki sawa kwa wote na yenye uchumi imara unaotoa ajira na tija kwa wananchi wote, uongozi makini, thabiti na wenye uzalendo wa kweli kwa Taifa lao.
Wakichangia kwenye kongamano hilo, Profesa Abdallah Safari, alisema maliasili zilizopo nchini haziwanufaishi wananchi wala Taifa kwa ujumla.Alisema hayo ni matokeo ya mikataba mibovu na kwamba upo wakati vijana watavamia kwenye migodi na maeneo mengine ya rasilimali zilizopo ili kunufaika nazo.
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Bw. Augustine Mrema, alisema hali kuwa mbaya nchini, ni ishara kwamba uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) umefikia kikomo kwa vile umeshindwa kuwafikisha Watanzania katika maisha bora waliyoahidiwa.
Alihoji sababu za Tanzania Bara kuing`ang`ania Zanzibar wakati ipo Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ambayo wanaweza kuungana nayo.
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw. James Mbatia, aliwataka Watanzania kufikiria kwa kina hali inayoikabili nchi hivi sasa kwani ikisambaratika hakuna atakayepona na akawataka pia watafute mbadala kwa madai kwamba walioko madarakani wameshindwa kuongoza nchi.
Mhadhiri wa Msikiti wa Idrisa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, Maalim Ali Bassaleh, alihoji taarifa zinazotolewa na serikali kwamba watu waliochota fedha katika Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wanazirejesha wakati hawakukopa wala kuwekesha amana.
``Hawa ni wezi. Wakamatwe na wafikishwe mahakamani,`` alisema Maalim Bassaleh.
Awali, akielezea madhumuni ya kongamano hilo, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, alisema walilazimika kuliandaa ili kutafakari na kuona nini la kufanya ili kuikwamua nchi ambayo alidai inapita katika kipindi kigumu kinachohatarisha hatma ya Watanzania.
Kongamano hilo lilihudhuriwa na wawakilishi kutoka balozi za Ufaransa na Marekani, taasisi za kijamii, vyuo vikuu, wabunge wa Jamhuri ya Muungano, Baraza la Wawakilishi na makundi ya watu wenye ulemavu.
SOURCE: Nipashe