Leo nimerudia kuzisikiliza Msinitenge, Ni Kazeze, Kosa la Marehemu, Bush Party na Homa Dunia

Hiyo inaitwa Narrative lyrical styles huwezi kuipata kwa vijana wa Sasa hivi..
Kote East Africa..
Jiulize kipindi hicho Hawa K sal walikuwa wakenya ila Usingeweza kuwatofautisha na Watanzania waru akama Hardmad na wengine..

Nakuomba Rudi kasikilize Mkiwa ya Ksal feat Ferouz...
Uone watu walivyokuwa wakitunga halafu ukisikiliza kiswahili Rudi niambie yule alikuwa Mkenya au Mtanzania...
K sal ni mkenya? Usije ukawa unachanganya na K South ambaye ni marehemu.
 
Yeah…
Yeah…
Hakuna S bila O
L bila O
Mwingine aitwe’ Thang bila Solo
Shupavu’ awajibike kama Apollo
Jay, Afande!
Ni ukuta’ wapi uchochoro?
Hakuna S bila O
L bila O
Mwingine aitwe’ Thang bila Solo
Shupavu’ awajibike kama Apollo
Jay, Afande!
Ni ukuta’ wapi uchochoro?
Yo Naghani’ ni mtazamo wa fani
Ile dhana ni uhuni wameleta hawa katuni
Kuna ku-rap na kumbwata
Ma-reaper na ma-rapper
Katuni, Tungo tata
Wapi ulipo we jaku?
Unakuwa mtumwa ili upewe promo kuuza
Au kama ni binti’ ukalale kwa prodyuza
Ma-Promoter wana uma tu’ hawajui na kupuliza
Na siku wakipuliza jua kidonda kishaoza
Natamani kuwa huru mnyonyaji asinidhuru
Wanaitwa “ma-Emcee” hawajui mitindo huru
Huu mtazamo wangu’ naona vingi vioja
Yaani watangazaji sasa’ ndo ma meneja
Vidato sita nlivyopitia
Ndivyo vinavyonisaidia
Mbunifu ukiizingatia
Hata wakinibania
Ni kipaji tu
Ni mtazamo tu
Msikasirike wash’kaji
Haya mawazo tu
Ulamaa…
 
Yeah…
Yeah…
Hakuna S bila O
L bila O
Mwingine aitwe’ Thang bila Solo
Shupavu’ awajibike kama Apollo
Jay, Afande!
Ni ukuta’ wapi uchochoro?
Hakuna S bila O
L bila O
Mwingine aitwe’ Thang bila Solo
Shupavu’ awajibike kama Apollo
Jay, Afande!
Ni ukuta’ wapi uchochoro?
Yo Naghani’ ni mtazamo wa fani
Ile dhana ni uhuni wameleta hawa katuni
Kuna ku-rap na kumbwata
Ma-reaper na ma-rapper
Katuni, Tungo tata
Wapi ulipo we jaku?
Unakuwa mtumwa ili upewe promo kuuza
Au kama ni binti’ ukalale kwa prodyuza
Ma-Promoter wana uma tu’ hawajui na kupuliza
Na siku wakipuliza jua kidonda kishaoza
Natamani kuwa huru mnyonyaji asinidhuru
Wanaitwa “ma-Emcee” hawajui mitindo huru
Huu mtazamo wangu’ naona vingi vioja
Yaani watangazaji sasa’ ndo ma meneja
Vidato sita nlivyopitia
Ndivyo vinavyonisaidia
Mbunifu ukiizingatia
Hata wakinibania
Ni kipaji tu
Ni mtazamo tu
Msikasirike wash’kaji
Haya mawazo tu
Ulamaa…
Solo Thang alifunika wote hapo
 
Hiyo inaitwa Narrative lyrical styles huwezi kuipata kwa vijana wa Sasa hivi..
Kote East Africa..
Jiulize kipindi hicho Hawa K sal walikuwa wakenya ila Usingeweza kuwatofautisha na Watanzania waru akama Hardmad na wengine..

Nakuomba Rudi kasikilize Mkiwa ya Ksal feat Ferouz...
Uone watu walivyokuwa wakitunga halafu ukisikiliza kiswahili Rudi niambie yule alikuwa Mkenya au Mtanzania...
Ushawahi sikiliza ngoma ya Boss kaimba Ferooz ft Solo Thang &Juma Kiroboto Nature???
Kama unaangalia movie vile
 
Baada ya kumaliza kumshukuru Maanani Muumba Mbingu na ardhi. Nikapata kikombe cha kahawa, nikatafakari yale yangu ya siku na ratiba za hapa na pale lakini akili ikanisukuma kusikiliza kidogo music.

Katika kuchakura makabrasha mkono ukaangukia kwenye kazi ya kizazi cha kati cha muziki wa vijana wa miaka ile ya 90's, walioweka heshima na kuchonga barabara. Ambayo kizazi hiki hawaumizi kichwa wanaserereka tu.

Ghafla nikaona jina Msinitenge Profesa J, nikaona Ni kazeze wa OCG, nikakutana na kosa la marehemu uswahili ni matola nikaugusa bush party Sold ground family na homa ya dunia Solo thang na ingekuwa vipi Mwana FA.

Nikasema hizi zinatosha kuisikiliza kwa kweli nikiri kile nilichokisikia nikarudia nikagundua baki ya beat nzito na mistari.

Jamaa walikuwa ni wabunifu na waliumiza vichwa nina hakika kizazi hiki hata wakusanyane wote hawawezi kufikia ule uwezo, ni vile tu zilikuwa zama za kale za giza ila hawa wakongwe wanastahili kujengewa minara.

Nilipomaliza kusikiliza nikaingia kwenye vokswageni beatle yangu mgongo wa chura nikajikata kwenye mishe zangu!

Kweli ya kale ni dhahabu nini mnataka mazee!
Machozi yanatoka ishara homa ya dunia
Binadamu wanyama ndege wote mbona mnalia
Parapanda italia
Mito milima mabonde vyote vitaangamia
Madaktari waganga ujuzi washautumia
Wamemzunguuka mgonjwa homa ya dunia
Waumini wamemsalia
Na bado mikononi akawafia...
 
Kwenye Party/Party by KR MULLA nadhani hii nyimbo ilikuwa ndio foundation ya mziki wa sasa. Mdundo wa hii nyimbo iliuwahi muda.
 
Machozi yanatoka ishara homa ya dunia
Binadamu wanyama ndege wote mbona mnalia
Parapanda italia
Mito milima mabonde vyote vitaangamia
Madaktari waganga ujuzi washautumia
Wamemzunguuka mgonjwa homa ya dunia
Waumini wamemsalia
Na bado mikononi akawafia...
Ukipima hiyo mistari na uzito wake hakika solo ni mnyama sana!
 
Naomba kuuliza kwa wataalam wa muziki. Hivi singeli Ina vina na mizani?? Au huyu muimba singeli akiwa studio neno linalomjia kichwani ndio anatamka tu?
 
Back
Top Bottom