TAWA
JF-Expert Member
- Jun 23, 2013
- 3,674
- 1,572
Kwanza nitoe pongezi kwa mheshimiwa rais Dr. John Joseph Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kuamua siku ya leo iwe ni siku ya usafi nchi nzima. Lakini pia kwa watanzania ambao wamejitokeza kwa namna ya pekee katika kutekeleza agizo hilo la rais.
Kumekuwa na kasumba ya watanzania walio wengi kukwepa ukweli unaowaudhi wakubwa fulani ndani ya nchi, hasa kwa kulitamka neno TANGANYIKA. Imefika wakati watu wanaona dhambi kutamka Tanganyika. Hata viongozi wakubwa ndani ya nchi wanaishia kusema "Uhuru wa Tanzania bara". Lakini kimsingi hakuna nchi inayoitwa Tanzania bara iliyokabidhiwa uhuru. Mbona hatuhofii kusema Zanzibar au Unguja ama Pemba. Kwa nini midomo yetu inakuwa mizito kutamka Tanganyika?
Ukweli ni Tanganyika ndiyo ilipata uhuru 09/12/1961 na si Tanzania au Tanzania Bara kama wengi tunavyokaririshwa.
Kumekuwa na kasumba ya watanzania walio wengi kukwepa ukweli unaowaudhi wakubwa fulani ndani ya nchi, hasa kwa kulitamka neno TANGANYIKA. Imefika wakati watu wanaona dhambi kutamka Tanganyika. Hata viongozi wakubwa ndani ya nchi wanaishia kusema "Uhuru wa Tanzania bara". Lakini kimsingi hakuna nchi inayoitwa Tanzania bara iliyokabidhiwa uhuru. Mbona hatuhofii kusema Zanzibar au Unguja ama Pemba. Kwa nini midomo yetu inakuwa mizito kutamka Tanganyika?
Ukweli ni Tanganyika ndiyo ilipata uhuru 09/12/1961 na si Tanzania au Tanzania Bara kama wengi tunavyokaririshwa.