DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Tarehe kama ya leo, Oktoba 29, 2025, inakumbukwa na Watanzania wengi kama siku ya maandamano makubwa yaliyotikisa taifa. Ni siku iliyobeba kumbukizi nzito kutokana na taarifa na madai kuhusu vifo na majeruhi wakati wa hatua za kukabiliana na waandamanaji. Leo tunawakumbuka wote waliopoteza maisha, pumzikeni kwa amani, na kwa majeruhi tunawaombea mpone haraka.