Leo ndio leo, jitu litavuliwa ubingwa

kilwakivinje

JF-Expert Member
Jan 4, 2014
5,999
9,089
Baada ya kula ng’ombe mzima katika mechi 26 zilizopita, leo ni fursa muhimu kwa Yanga kumalizia mkia utakaowapa rasmi ufalme wa Ligi Kuu msimu huu, watakapoikaribisha Coastal Union katika Uwanja wa Mkapa kuanzia saa 2:30 usiku.

Matokeo ya ushindi huo yataihakikishia Yanga ubingwa na kuhitimisha utawala wa misimu minne mfululizo ya watani wao, Simba ambao ndio walikuwa wababe wakitwaa mara nne mfululizo.

Kwa kuibuka na ushindi dhidi ya Coastal Union, Yanga itafikisha pointi 67 ambazo HAZITAFIKIWA na timu nyingine yoyote.
 
Baada ya kula ng’ombe mzima katika mechi 26 zilizopita, leo ni fursa muhimu kwa Yanga kumalizia mkia utakaowapa rasmi ufalme wa Ligi Kuu msimu huu, watakapoikaribisha Coastal Union katika Uwanja wa Mkapa kuanzia saa 2:30 usiku.

Matokeo ya ushindi huo yataihakikishia Yanga ubingwa na kuhitimisha utawala wa misimu minne mfululizo ya watani wao, Simba ambao ndio walikuwa wababe wakitwaa mara nne mfululizo.

Kwa kuibuka na ushindi dhidi ya Coastal Union, Yanga itafikisha pointi 67 ambazo HAZITAFIKIWA na timu nyingine yoyote.
Majaabu ya 8 ya dunia.

Tangu kuanza msimu wa NBC PL 2021 - 2022 ya TZ, MAKOLOKOLO FC hawajawahi kukaa kileleni mwa msimamo wa NBC PL hadi kuisha kwa ligi kuu.
 
Ngoja tusubiri tuone. Maana hii Coastal Union ya mwishoni mwa huu msimu, imechangamka kweli kweli! Azam na Simba wanaifahamu kweli kweli.

Halafu Mungu alivyo na majaribu, tutakutana tena kwenye fainali! Na pia kwenye Ngao ya Jamii msimu ujao!

Dah! Watakubali kweli kufungwa mara zote hizo na wananchi! Huyu Sopu wao ni hatari kweli kweli!!!
 
Back
Top Bottom