Leo navunja kibubu!

Leo navunja kibubu!

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
LEO NAVUNJA KIBUBU!
1
Leo navunja kibubu, pesa ninunue khanga,
Apendeze mahabubu, kama binti wa kitanga
Atokapo awe bubu, washindwe wano jigonga
Mniache nayajenga, mkome kunita zoba.
2
Sasa navunja kibubu, nipate nunua kanga,
Ale ashibe muhibu, kitoweo si mchunga,
Usiku tule kababu, uji pilipilimanga,
Mniache nayajenga, mkome kunita zoba.
3
Mimi navunja kibubu, nikagule kungumanga,
Nimpatie tabibu, mafusho toka Umanga,
Nimuenzi taratibu, niseme na zake nyonga
Mniache nayajenga, mkome kunita zoba.
3
Mie navunja kibubu, habibi apate shanga,
Mapambo yake dhahabu, vidoleni na kitanga,
Sawa nipate adhabu, apendeze wangu ninga,
Mniache nayajenga, mkome kunita zoba.
4
Njano navunja kibubu, lengo niweze kujenga,
Nyumba isiwe na tabu, mahaba yatie nanga,
Penzi lataka adabu, siwezi kulibananga,
Mniache nayajenga, mkome kunita zoba

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
0784845394/0762845394
mzalendo.njano5
Morogoro Tanzania

kwa mashairi mengine kama hayo waweza kujisomea katika blogu yangu, kwenye icon ya mashairi utabofya hapo kisha utayaona mashairi mengi nilitotunga

SASA HAMSINI RASI, HAMSINI MAJINUNI. | Kisima Cha Jangwani.
 
Hiyo ni yako akiba, ama ya ndugu uliiba,
Uliachiwa na baba, ama ya mama mahaba,
Hicho kibubu si haba, kiache kijaze kibaba,
Mapenzi upofu.

Hata boma ujengalo, kumbe kisa ni hidaya,
kakubana mpogolo, imeshakutoka haya,
utageuka kipolo, ukome maisha haya,
Mapenzi upofu.

Mapenzi kweli upofu, apendae hupofuka,
Akili upata ufu, kuelewa hufutika,
Mapenzi yakija kifu, wazimu unafumka,
Iko siku utajuta.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom