Leo Katika Historia:PROTECTIVE TARRIF, Ni nini, ilianzaje na Inafaida gani kwetu

MSEZA MKULU

JF-Expert Member
Jul 22, 2011
3,763
5,605
staar-review-social-studies-2013-78-638.jpg


Ni nini?
Huu ni ushuru ambao unawekwa kwenye Bidhaa zinazoingia nchini ili bei zake zipande na kuwa angalau sawa na bidhaa zinazotengenezwa hapa nchini.

Mfano:
tyres.jpg

Unabiashara/kiwanda cha kutengeneza MATAIRI ya Gari na Kampuni nyingine iko MALASIA infanya biashara hiyohiyo. Lakini kutokana na kwao Malighafi na Gharama za uzalishaji kuwa chini wanaleta Matairi yao Tanzania Kwa bei rahisi kuliko yako. Na kampuni yako inaelekea kufirisika kwa kukosa wateja. Unaamua kwenda Serikalini kwa ajili ya msaada. Serikali/TRA wanaweka kodi kwa Kampuni ya malaysia kulinda biashara yako ili isife. Kama kodi ni kubwa kiasi cha kutosha, Matairi ya Malaysia itabidi yapande bei na Biashara yako Imelindwa.
Kodi hii ndio PROTECTIVE TARRIF.

MFANO HALISI KATIKA PICHA JINSI INAVYOFANYA KAZI,
slide_8.jpg


ILIANZAJE ANZAJE ?
220px-Alexander_Hamilton_portrait_by_John_Trumbull_1806.jpg

mmarekani Alexander Hamilton ndio mtu wa kwanza kupendekeza hii kitu ili kulinda viwanda na biashara ya ndani US. Baada ya vita vya 1822 marekani, Bidhaa kutoka UK zilifurika na kuanza kuua viwanda vya ndani na kutishia kabisa uwepo wa viwanda marekani kama kwetu sasa Bidhaa kutoka China. Bunge la Congress 1816 likapitisha.

SIKU HIZI HALI IKOJE?
2016-03-10-60a1d304_large.jpg

TUME YA KIMATAIFA YA BIASHARA INARIPOTI KUWA KUNA KODI ZAIDI YA 12000 KWA BIDHAA MBALIMBALI ZINAZOINGIA USA. Mfano karanga ambazo hazijapukuchuliwa zina hadi 163.3% ya kodi. Nyama kutoka ulaya, siagi na bidhaa mbalimbali zina hadi 100% ya kodi. Sekta zote za ndani zinategemea kodi hizi kuwepo kwao sokoni. Bila hii bidhaa za wamarekani zingepata wakati mgumu sana mbele ya macho ya wateja wao.

Kama nchi au mtu mmoja mmoja tuna mengi ya kujifunza kutoka katika historia mbalimbali duniani. Vitu hivi vikiingizwa kwa umakini bila upendeleo wala ubinafsi vitachechea maendeleo katika kila kona ya taifa.
 
Ili system hii ifanye kazi vizuri kwanza inatakiwa wafanyakazi katika idara husika kuwa na maadili mno ikiwa ni TRA, CUSTOMS na JESHI LA POLISI...ukiangalia bidhaa mingi zinazotoka nje kuingia hapa nchini zinauzwa bei ya chini sana kulinganisha na bidhaa zinazotengenezwa hapa mfano Mafuta ya kula, Sabuni , Sukar na list itaendelea...Shida ni kukosa maadili kuanzia wananchi wanaovusha bidhaa hizo kwenye mipaka isiyo rasmi lakini na maofisa wanao chukuwa rushwa na kupitisha bidhaa bila kulipiwa kodi..
 
Ili system hii ifanye kazi vizuri kwanza inatakiwa wafanyakazi katika idara husika kuwa na maadili mno ikiwa ni TRA, CUSTOMS na JESHI LA POLISI...ukiangalia bidhaa mingi zinazotoka nje kuingia hapa nchini zinauzwa bei ya chini sana kulinganisha na bidhaa zinazotengenezwa hapa mfano Mafuta ya kula, Sabuni , Sukar na list itaendelea...Shida ni kukosa maadili kuanzia wananchi wanaovusha bidhaa hizo kwenye mipaka isiyo rasmi lakini na maofisa wanao chukuwa rushwa na kupitisha bidhaa bila kulipiwa kodi..
uko sahihi chief. Hatuwezi kuingia kwenye mapinduzi ya viwanda na watu corrupt. katika planning za JPM lazima hii iingie kama changamoto na aje na corrective ation ambayo ni practical na long term
 
Back
Top Bottom