KERO Serikali ifanye utaratibu wa kupunguza Kodi na Ushuru kutusaidia Wafanyabiashara wa Pemba

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Sep 23, 2024
58
32
Asilimia kubwa ya sisi Wafanyabiashara Kisiwani Pemba tunapata wakati mgumu kuhusu suala la kodi na ushuru mkubwa tunaotozwa katika Bandari ya Unguja pamoja na Bandari ya Pemba

Hali hiyo imekuwa ikisababisha baadhi ya bidhaa kupanda bei tofauti na uhalisia kwa kuwa tunalazimika kufanya hivyo ili angalau turejeshe gharama tulizotumia kuzisafirisha.

Tunaponunua bidhaa kutoka Unguja tunalipa ushuru na kodi kwa mamlaka za kikodi, tukifika Pemba napo kuna gharama za kulipia.

Ushuru na kodi zinapokuwa rafiki zitasaidia bei ya bidhaa kuwa chini na pia itawarahisishia Wananchi kuzinunua kwa bei ya chini.

Hivi karibuni kwenye moja ya Kongamano Afisa Mdhamini Wizara ya Biashara, Ali Suleiman alisema endapo Kodi na Tozo zitakuwa rafiki kwa Wafanyabiashara itasaidia kuchangia ukuaji wa pato la Nchi, hiyo inamaanisha Mamlaka zenyewe zinajua kuna hiyo changamoto.
 
Asilimia kubwa ya sisi Wafanyabiashara Kisiwani Pemba tunapata wakati mgumu kuhusu suala la kodi na ushuru mkubwa tunaotozwa katika Bandari ya Unguja pamoja na Bandari ya Pemba

Hali hiyo imekuwa ikisababisha baadhi ya bidhaa kupanda bei tofauti na uhalisia kwa kuwa tunalazimika kufanya hivyo ili angalau turejeshe gharama tulizotumia kuzisafirisha.

Tunaponunua bidhaa kutoka Unguja tunalipa ushuru na kodi kwa mamlaka za kikodi, tukifika Pemba napo kuna gharama za kulipia.

Ushuru na kodi zinapokuwa rafiki zitasaidia bei ya bidhaa kuwa chini na pia itawarahisishia Wananchi kuzinunua kwa bei ya chini.

Hivi karibuni kwenye moja ya Kongamano Afisa Mdhamini Wizara ya Biashara, Ali Suleiman alisema endapo Kodi na ushuru zitakuwa rafiki kwa Wafanyabiashara itasaidia kuchangia ukuaji wa pato la Nchi, hiyo inamaanisha Mamlaka zenyewe zinajua kuna hiyo changamoto.
 
mkuu huku bala tnajua nyie nd mnafaid mema ya muungan huu! inaman na huko mambo magum? tumezoea kuambia vt kam cm tv na vngnevyo zenji bei chee mana kod zpo chin san!!
 
Serikali inahitaji kodi kujiendesha, sema serikkali iweke mfumo mwepesi wa kulipa kodi ili tuendelee kulipa.
 
Back
Top Bottom