Lema ni Mwanasiasa wa Kawaida, Ila Chuki ya Watawala Imemfanya awe Shujaa

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
40,432
73,078
Mhe.Lema Mbunge wa Arusha ni mwanasiasa mahiri lakini wa viwango vya kawaida kwani wa aina yake bado wapo wengi tuu. Lakini ghafla ametokea kuwa maarufu mno na kuonekana shujaa mbele ya wananchi wa Arusha na Tanzania kwa ujumla. Hali iliyojitokeza Mjini Arusha leo ni uthibitisho kuwa hakuna wa kumzidi umaarufu wa kisiasa kwa sasa hapo Arusha.

Nini kimesababisha? Ukweli ni kuwa uonevu na wivu wa viongozi wa serikali ya CCM ndio karata yake iliyo mfanya aibuke shujaa wa aina yake. Viongozi hao akiwamo Mrisho Gambo RC wa Arusha wameonyesha wazi kuhusika na njama ambazo Majaji wa Mahakama ya Rufaa wameita 'unajisi wa sheria' dhidi ya Lema.

Safari ya kisiasa inajambo muhimu moja kuu nalo ni kupata uungwaji mkono, na hilo Lema amelimaliza sasa ni shujaa na anaungwa mkono hivyo watesi wake badala ya kumpunguzia umaarufu sasa ndio wamempa kiki zaidi kwa wao kushindwa kujua walilofanya ni kosa kubwa kimkakati kama walivyo dhani mwanzo
 
Mpeni cheo cha juu sasa, ushujaa uonekane kama upo nchi nzima.

Naona kufungwa kwake kawaida tu, sababu ana mdomo mrefu wa maneno mabaya na pia mgomvi hana uvumilivu. Hajui wapi na wapi atende majambo, hajiheshimu. Labda jela imemnyoosha, muda utaonyesha.
 
Godbless Jonathan Lema ni mpanganaji mashuhuri na Jasiri katika siasa za Tanzania
tmp_8141-16251842_377938042574415_2182147864036445963_o-182422605.jpg
 
CHARISMA..compelling attractiveness or charm that can inspire devotion in others....hii ndio silaha pekee kwenye siasa...Lema.Sugu.Msigwa.Mbowe.Mnyika.Lissu nk wote wanayo hii kitu....hata ukimdharau Lema ni sawa na kujitekenya na kucheka mwenyewe...unafikiri CCM hawalitaki jimbo LA Arusha mjini...kama unaweza kamtoe 2020 ..aarrgg
 
CHARISMA..compelling attractiveness or charm that can inspire devotion in others....hii ndio silaha pekee kwenye siasa...Lema.Sugu.Msigwa.Mbowe.Mnyika.Lissu nk wote wanayo hii kitu....hata ukimdharau Lema ni sawa na kujitekenya na kucheka mwenyewe...unafikiri CCM hawalitaki jimbo LA Arusha mjini...kama unaweza kamtoe 2020 ..aarrgg
Mkuu umeongea kweli kabisa.
 
Kuna watu wana mawazo ya kizamani (kikoloni). Wanadhani ukiwa kiongozi wa serikali hutakiwi kuhojiwa, kukosolewa na hata kubezwa unapofanya kinyume na utaratibu. Huo ni upuuzi na ni ya kizamani sana.

Katika sakata hili Lema ni mshindi kwa sababu amesababisha hukumu imetoka kwa ajili ya wananchi waliokuwa wakionewa na upungufu huo wa kisheria hawataonewa tena kwa sababu ya hiyo ruling, hivyo Lema ni shujaa .
 
CHARISMA..compelling attractiveness or charm that can inspire devotion in others....hii ndio silaha pekee kwenye siasa...Lema.Sugu.Msigwa.Mbowe.Mnyika.Lissu nk wote wanayo hii kitu....hata ukimdharau Lema ni sawa na kujitekenya na kucheka mwenyewe...unafikiri CCM hawalitaki jimbo LA Arusha mjini...kama unaweza kamtoe 2020 ..aarrgg
Mbona Lowassa hayumo kwenye list yako mkuu? Mafuriko yale na mapenzi mahaba watu walikuwa wanafuata nini? Wanaume wazima walideki barabara kibao tena mchana kweupee...I am just curious!
 
Ama kweli baadhi yetu watz tumeshikiwa akili zetu ss sijui ni kwa muda gani-kwani sijaona ushujaa ambao Lema anapewa
 
Mpeni cheo cha juu sasa, ushujaa uonekane kama upo nchi nzima.

Naona kufungwa kwake kawaida tu, sababu ana mdomo mrefu wa maneno mabaya na pia mgomvi hana uvumilivu. Hajui wapi na wapi atende majambo, hajiheshimu. Labda jela imemnyoosha, muda utaonyesha.
Naona uelewa wako si mzuri kwa hoja iliyoko mezani mkuu, yaani kuna viongozi walioweka hila asote jela asipate dhamana na wakati alikuwa na haki kisheria.

Hawa hawana tofauti na makaburu wa Mandela ie

"KABURU NI KABURU TU, HATA AKIWA MZAWA, HATUKUWACHUKIA MAKABURU KWA RANGI YAO BALI KWA VITENDO VYAO VYA UKANDAMIZAJI NA UBAGUZI"
By mwl J.K.Nyerere

Bado hujaelewa?
 
Kuna watu wana mawazo ya kizamani (kikoloni). Wanadhani ukiwa kiongozi wa serikali hutakiwi kuhojiwa, kukosolewa na hata kubezwa unapofanya kinyume na utaratibu. Huo ni upuuzi na ni ya kizamani sana.

Katika sakata hili Lema ni mshindi kwa sababu amesababisha hukumu imetoka kwa ajili ya wananchi waliokuwa wakionewa na upungufu huo wa kisheria hawataonewa tena kwa sababu ya hiyo ruling, hivyo Lema ni shujaa .
"Tunahitaji vijana wenye ujasiri mkubwa wa kuhoji"
By mwl Nyerere
 
Back
Top Bottom