Lema aache kumtishia amani DPP

Lema aache kumtishia amani DPP

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,931
Reaction score
7,828
Siasa anazofanya Lema, Mbunge wa Arusha kwa hakika ni za kijambazi. Katika clip ya video aliyorekodi punde utaona si anamtishia amani DPP tu bali viongozi wote wa awamu ya tano.

Wenye ufahamu wanajua aina ya uongozi wa nchi wanayopigania CHADEMA ni ile ya mwenye nacho anaongezewa na asiyenacho anazidi kuwa maskini. Tafsiri halisi ya demokrasia wanayopigania ni pale kuna ulaghai wa uhuru huku wenyenacho wananunua haki na kuuziwa haki kutokana na mfumo wa rushwa na ubinafsi kutawala.

Huko nyuma wahujumu uchumi na fisadi kumekuwa na kesi tu. Kila mwananchi anajua hujuma na ufisadi lakini hakuna anayekamatwa na akikamatwa anashinda kesi hafungwi maana haki inauzwa na wanasheria na wenye nacho wananunua haki.

Ndio maana baada ya tumbuatumbua ya majipu ya kifisadi fisadi wamejaa gerezani. Ni kweli kama anavyodai lema washutumiwa wa ufisadi na ndugu na marafiki zao wana hasira na kisasi. Ila si kama anavyotumaini Lema eti 'regime' hii itapita fisadi watarudi ulingoni na kulipa kisasi.

Kina Lema wajue Watanzania walifunzwa na Baba wa Taifa kudai haki na kupinga unyonyaji ndio maana Mwalimu Nyerere akaita chama alichokiongoza mwenyewe Chama cha Mapinduzi. CCM sio chama cha kiliberali kama CHADEMA kwa sababu kinapigania demokrasia na kupinga unyonyaji wa tabaka moja kulinyonya tabaka lingine.

Ningemshauri Lema atafakari badala ya kuwatisha watendaji na viongozi wa awamu ya tano kupitia kitisho kwa DPP. Ajue hakuna kurudi nyuma, mapinduzi ya uchumi Tanzania yataenda kwa kasi na kumfadisha kila raia.
 
Sa nani kamtisha nani...hilo liDPP lenu halijui kwamba lema alishakamatwa na kesi ipo singida? Yale matisho ya juzi yalikuwa na maana gani?

Limtu linasimamia sheria linajua kesi ipo mahakamni bado linatishia, hapo ndo utajua mamtu yapo ofcn but yanaendeshwa na mihemko..

lema yupo sahihi kabisa mwanaume lazima ujitete uwezi tishwa tishwa kindezi ukaa kimyaa...Namuunga mkono Mbunge wangu lema.
 
Umeandika hadithi ndefu sana lakini alicho sema Lema n ukweli . Amemtaka awache kutumia nafasi yake vibaya kwa kubambikia Watanzania kesi halafu wanakaa jela bila ya dhamana wala ushahidi hatimae ana wa black mail walipe ngawira.

DPD anachofanya kwa kushirikiana na serikali ni wozi wa mchana.

Waache

Lema was right


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Mh! Mimi napita tu ili wenye kutetea uvunjifu wa sheria za kuleta taharuki katika jamii, waendeleze mjadala huu.
 
Siasa anazofanya Lema, Mbunge wa Arusha kwa hakika ni za kijambazi. Katika clip ya video aliyorekodi punde utaona si anamtishia amani DPP tu bali viongozi wote wa awamu ya tano.

Wenye ufahamu wanajua aina ya uongozi wa nchi wanayopigania CHADEMA ni ile ya mwenye nacho anaongezewa na asiyenacho anazidi kuwa maskini. Tafsiri halisi ya demokrasia wanayopigania ni pale kuna ulaghai wa uhuru huku wenyenacho wananunua haki na kuuziwa haki kutokana na mfumo wa rushwa na ubinafsi kutawala.

Huko nyuma wahujumu uchumi na fisadi kumekuwa na kesi tu. Kila mwananchi anajua hujuma na ufisadi lakini hakuna anayekamatwa na akikamatwa anashinda kesi hafungwi maana haki inauzwa na wanasheria na wenye nacho wananunua haki.

Ndio maana baada ya tumbuatumbua ya majipu ya kifisadi fisadi wamejaa gerezani. Ni kweli kama anavyodai lema washutumiwa wa ufisadi na ndugu na marafiki zao wana hasira na kisasi. Ila si kama anavyotumaini Lema eti 'regime' hii itapita fisadi watarudi ulingoni na kulipa kisasi.

Kina Lema wajue Watanzania walifunzwa na Baba wa Taifa kudai haki na kupinga unyonyaji ndio maana Mwalimu Nyerere akaita chama alichokiongoza mwenyewe Chama cha Mapinduzi. CCM sio chama cha kiliberali kama CHADEMA kwa sababu kinapigania demokrasia na kupinga unyonyaji wa tabaka moja kulinyonya tabaka lingine.

Ningemshauri Lema atafakari badala ya kuwatisha watendaji na viongozi wa awamu ya tano kupitia kitisho kwa DPP. Ajue hakuna kurudi nyuma, mapinduzi ya uchumi Tanzania yataenda kwa kasi na kumfadisha kila raia.
Yawezekana una matatizo ambayo huyajui. Mbona unachoongelea hakishabihiani na maelezo ya Lema? Ni upungufu wa uelewa, ni uwezo mdogo wa akili au unajiondoa akili makusudi?
 
Tuwe professional kwenye vitu vyetu, tutakumbukwa kwa mazuri tukiviacha.
 
Watanzania na dunia inashuhudia yote na kwa taarifa yenu kadiri mnavyodhulumu watu mfano hizo fine 350M,Tzs, tunapoteza zaidi ya 350B bilion Tzs, support ya bajeti.Mpango na Dotto James wanawakati mgumu sana vikao na wahisani.Dunia inatoka gizani kwenda ktk nuru nyinyi mnaturudisha gizani.Lema na Watanzania wema ongezeni SAUTI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Atakuambia yeye ni waziri kivuli wa mambo ya ndani.
 
Sasa Lema na Huyo DPP nani aliyemtishia mwenzake? Lema hajamtisha kamwambia ukweli kwamba hamuogopi na akitaka ampe hukumu hata ya kumyonga na pia amemsisitiza kwamba awamu hii haingozwi na Mungu wala yesu hivyo itapita tu kama nyingine.
 
Back
Top Bottom