Lawrence Mafuru aibukia CRDB

Lawrence Mafuru aibukia CRDB

Hakeem makamba

Senior Member
Joined
Apr 15, 2011
Posts
123
Reaction score
41
Mkurugenzi wa Mtendaji wa zamani wa Benki ya NBC Bw.Lawrence Mafuru ameshinda kwa kura nyingi nafasi ya kuwa mjumbe huru wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB. Pamoja nae Waziri Mkuu mstaafu Bwana Fredrick Sumaye naye ametetea nafasi ya ujumbe wa bodi ys Benki hiyo. Source: Habari Mseto Blog
=================================




Mkurugenzi Huru wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Lawrence Mafuru akizungumza wakati wa kuomba kura kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 19 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB uliofanyika jijini Arusha. Mafuru alishinda nafasi aliyokuwa akiwania ya Mkurugenzi Huru wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB.

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Benki ya CRDB wakipewa karatasi za kupigia kura.

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Benki ya CRDB wakipewa karatasi za kupigia kura.

Kura kabla ya kuhesabiwa.

Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB akimpongeza Mkurugenzi Huru wa Bodi hiyo, Lawrence Mafuru baada ya kuchaguliwa wakati wa Mkutano Mkuu wa 19 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB uliofanyika jijini Arusha, mwishoni mwa wiki.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia), akimpongeza Mkurugenzi Huru wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Lawrence Mafuru baada ya kuchaguliwa wakati wa Mkutano Mkuu wa 19 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB uliofanyika jijini Arusha, mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja
 
Mkurugenzi wa Mtendaji wa zamani wa Benki ya NBC Bw.Lawrence Mafuru ameshinda kwa kura nyingi nafasi ya kuwa mjumbe huru wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB. Pamoja nae Waziri Mkuu mstaafu Bwana Fredrick Sumaye naye ametetea nafasi ya ujumbe wa bodi ys Benki hiyo. Source: Habari Mseto Blog

Nini majukumu ya mjumbe huru ndani ya bodi?
 
Corporate Governance - Kuisimamia management kwa niaba ya Shareholders
 
Heri yake. Lakini hawa watendaji wa mashirika ya umma kuna vitu vichafu wanaficha AMA wanashiriki kufanya...tatizo la NBC si la kawaida.
 
Bwana Mafuru ni hazina kubwa sana kwa nchi yetu katika masuala ya fedha ila nashangaa hapewi nafasi au jina lake halijakaa kama wale wenzetu.
mafuru ni mkurugezi wa idara mmoja wapo wa idara ofisi ya rais ufuatiliaji(presidential delivery buereu)
 
Bwana Mafuru ni hazina kubwa sana kwa nchi yetu katika masuala ya fedha ila nashangaa hapewi nafasi au jina lake halijakaa kama wale wenzetu.

Keshapewa nafasi mkuu, pale President's Delivery Bureau (PDB)- Ni Director
 
Bwana Mafuru ni hazina kubwa sana kwa nchi yetu katika masuala ya fedha ila nashangaa hapewi nafasi au jina lake halijakaa kama wale wenzetu.

Acha kuleta udini hapa ,mbona NBC iko hoi bin taaban ?
 
Acha kuleta udini hapa ,mbona NBC iko hoi bin taaban ?

NBC inaliwa na makaburu. We unajua kuwa faida inayopatikana bongo ndio inayolipa na mishahara ya wafanyakazi wa SA
 
Jiwe walilo likataa waashi sasa limekua jiwe kuu la pembeni...
Piga mzigo kaka!
 
Back
Top Bottom