Emmaloy
JF-Expert Member
- May 14, 2017
- 216
- 231
Kiufupi nianze tu kwa kusema watu wengi sio waumini saaaana wa aina ya muziki anaoufanya msanii Lavalava. Kwa muda mrefu sasa style yake ya uimbaji imekuwa haiendani kabisa na aina ya muziki unaofanywa na wasanii wenzie walio katika record label moja. Katika tamasha kubwa la burudani la Wasafi Festival lililopita mikoa kadhaa kabla ya jana kufikia tamati jijini Dsm huyu jamaa perfomance yake steijini imekuwa ya kiwango cha chini saaaana hakuna cha maana anachofanya zaidi ya kutuambia tu watazamaji kuwa hatusikii kwahiyo tuimbe wote..”Nasema siwasikii tuimbe wote tena..”
Ninachokiamini huyu jamaa ile nafasi yake pale WCB haikupaswa kuwa yake ila ni zali tu limemdondokea akajikuta keshasainiwa, tunahitaji watu wenye uweledi wa hali ya juu katika kufanya muziki na sio kila siku kuwa na aina ileile ya uimbaji na mbaya zaidi ni kwamba sijawahi muona akifanya show yake binafsi mbali na kudandia Festival tofauti na msanii Mbosso Khan ambaye hana muda mrefu saaana tangu asainiwe lakini kazi anayoifanya imeonekana
NB: Lavalava kashikilia nafasi ya mtu WCB
Ninachokiamini huyu jamaa ile nafasi yake pale WCB haikupaswa kuwa yake ila ni zali tu limemdondokea akajikuta keshasainiwa, tunahitaji watu wenye uweledi wa hali ya juu katika kufanya muziki na sio kila siku kuwa na aina ileile ya uimbaji na mbaya zaidi ni kwamba sijawahi muona akifanya show yake binafsi mbali na kudandia Festival tofauti na msanii Mbosso Khan ambaye hana muda mrefu saaana tangu asainiwe lakini kazi anayoifanya imeonekana
NB: Lavalava kashikilia nafasi ya mtu WCB