Boramaisha
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 820
- 18
Mkuu,
Nashukuru kwa hii habari ambayo imejaa mengi ambayo nimekuwa nikiandika leo hii. Wengine walisema nina majungu ila wewe umeiweka vizuri sana na kuwa NEUTRAL.
Hao Task Force nimewasikia habari zao. Wametembeza UBABE wa waziwazi na kibaya ni kuwa vyombo vya DOLA viliwaangalia tu wakitesa na utemi wao. Nashindwa kuamini kama kweli Kyela wamechagua au mtu kawachagulia.
Maadamu wao wenyewe wanakiri kuwa Mwakalinga kawaletea vitu vingi vya maendeleo na Mwakyembe hakuleta ila tu kasaidia Kuwafanya kuwa MAARUFU Tanzania, basi nawarudisha kwenye wimbo wa Marehemu Maneti na Mwalimu wangu Msasa pale Mazengo alishawahi kuutumia katika mfano kama huu akisema "....... Najuta umaarufu umeniponza............ amejenga nyumba kwao, mimi kwangu midabwada".
Mkataa pema................. Kila la kheri wana Kyela na umaarufu wenu.
Mwakalinga nilikuambia hamia Sikonge, ukakataa. Watani zako tungeliheshimu kazi yako.
Mwanamtama, naona hii ya Lipstick umeipenda sana tangu nikushushie juzi, heheheeee 🙂
.Mkuu nilikuwa sijagundua kumbe ukijumlisha George na Elias Mwakalinga, Mwanjala na dada Mwamunyange jumla yao ni 4501 bado wanashindwa na Dr Harrison M, labda kama wangechukua na zile kadi 10,000 hahahahahahahahaahhhh
Nyie watu wa Kyela mnataka kufanya sisi wengine hatuna majimbo wala wabunge? Kila kukicha Kyela tu kwa lipi hasa? Kwanza mmetuyeyusha kwa ubishi humu na matokeo tumeyaona. Tafuteni kitu badala inayovuta macho na masikio sasa siyo kila kukicha Kyela tu. Kyela yenyewe ni chovu mno kimaendeleo ukilinganisha na Wilaya zote za Mbeya na huu ni muda muafaka wa kuwashawishi wakina Mwakalinga mpange namna ya kuindeleza na siyo kujadili politics tu. Na hii tabia ya kusema kila mwaka kuwa Wanakyela ni wagumu hawayumbishwi, sijui Abdul Jumbe alitolewa jasho; haina tija hata kidogo kwenu iwapo mbazi kuwa wachovu mbofu kabisa kila mwaka. Ni muda wa kubadilika huu. Mkajenge kwenu badala ya kung'ang'ania Mbeya mjini na Dar es Salaam. Chukua ujumbe huo wape na wenzenu
Hizi kura 15,336 mhhhh!!!! Ngoja wazihakiki akina Mwakalinga maana naanza kuogopa kuwa Kyela nzima ilipiga kura na kuwa jimbo lenye wana CCM waaminifu sana. Sitashangaa wakiibua majina hadi ya akina Marehemu Mwaka............
Kitu gani wakati mmemshinda? Binadamu tuna tabia mbaya sana. Rafiki yako akishindwa au kufeli maisha, mtihani, uchaguzi basi unamkimbia. Mimi hilo sifanyi hata kidogo. . Kupanga ni kuchagua. Uamuzi wa Wanakyela uheshimiwe.
.Mkuu Sikonge,
Rafiki yako Mwakalinga WanaKyela wamemuingiza mjini ama wamemkaribisha nkayani. Kabla hata hajakuwa Mbunge, kuamua kujenga ghorofa, kuanzisha kituo cha radio na kugawa jezi zilizoandikwa Kyela FM aliona ndio maendeleo, hiyo si rushwa outright?! Angelifanya hayo bila ya kuwa na agenda yoyote behind tungelimwita ni mpenda maendeleo ya Kyela lakini kujenga na kugawa vitu halafu kutaka Ubunge in return ni rushwa tu.
Mwakyembe ni moto wa kuotea mbali! Hata kama angelikuwa anapigiwa kura za maoni na Watanzania wote angepeta tu bila ya kutoa jasho kujinadi. Kama walikuwepo wapambe wa Mwakyembe ni katika kulinda haki za chaguo lao asidhulumiwe wala kuhujumiwa kwa sababu tunaambiwa tayari 'Mmasai" mmoja alishasema kama Mwakyembe akirudi kwenye ubunge basi yeye si Mmasai! Tunasubiri wamuengue Dr. Mwakyembe waone kitakachotokea. Nawapa tano ndugu zangu wa Kyela kwa kuonyesha ushujaa dhidi ya Mwakipesile na genge lake. Tunataka Mkoa wa Mbeya na Tanzania isiyo na majungu wala visasi.
Mbona mwanzishaji habari hii hajaeleza jinsi ambavyo katika kampeni mahasimu wa Mwakyembe walijaribu kutumia ujanja wa kutaka Dr. Mwakyembe aanze kuzungumza ili watakapozungumza akina wagombea 'wao' wampiku. Matokeo yake, baada ya kuzungumza Dr. Mwakyembe watu walikuwa wakitawanyika wakidai tayari shughuli imekwisha na wagombea wengine kuachwa wakihutubia mashabiki wao tu! Ilipodhihirika hivyo, Dr. Mwakyembe akawa anawekwa kuzungumza mwisho ili watu wasiondoke. Haikufua dafu, baada ya kuzungumza wananchi walisema waziwazi kwamba tumeishakupitisha MBUNGE WETU Mwakyembe! Pia, sehemu zingine Dr. Mwakyembe alikuwa anazuiwa na wazee kuzunguza wakidai kwamba hana haja ya kuzungumza kwa sababu tayari keshapita!
Mkuu Sikonge,
Kama tunaitakia nchi hii mema kwa dhati tuwashabikie watu wa aina ya Dr. Mwakyembe warudi bungeni kuleta changamoto waliyokwisha kuionyesha kwa kung'oa visiki kwa maslahi ya Taifa. Naamini kabisa kama Dr. Slaa atafanikiwa kuupata urais, watu wenye msimamo kama Dr. Mwakyembe watampa support kubwa katika masuala yanayohusu maslahi ya taifa. Kwa maana nyingine msimamo utakuwa TAIFA MBELE, vyama nyuma!
.
Masanilo.
Karibu tena nyumbani jf.Ulipotelea wapi?.Nilifikiri umekuja Mwanza kutafuta ubunge.Badala yake sikukusikia wala sikukuona .
Karibu sana hapa Nyakato-mwanza
.Mwa Njelwa, sasa mbona unakuwa mbaguzi?Kyela si iko TZ?wengine wame oa/kuolewa na wachaga,wapare,wahaya,etc lakini in any case hii ni wilaya iko TZ kama inabidi kusaidiwa(kimawazo na kiuchumi) sio lazima ifanywe na wana Kyela kwa sababu hata kama ingekuwa ina dhabhabu isingeliwa na wana Kyela tu.
Nadhani una habari kuwa mchele 1st class TZ nzima unatoka katika maeneo mengi lakini Kyela iko No. 1 au 2?na wa TZ wote wanaula na kuishi.
Kwa hiyo jukumu la kuizungumzia sio lao tu.
Shukuru mungu wilaya yako haina baya ndio maana haizungumziwi kama inalo ilete hapa-si ndio penye jamii?:tape:
.Teh teh teh nilikuwa kwenye kura za Maoni mkubwa! Nilienda mkoa mmoja wapo wa pembezoni nilikofanyia kazi nimeambulia aibu tu
Ila mkuu naogopa sana memba wapya usije kuwa ni yule mwenye IDs mingi kama Mkulima, Muheza ama Buc.... ukachafua hali ya hewa Lol
jilala
Join Date Mon Aug 2010
Posts 6
Thanks : 0
Thanked 1 Time in 1 Post
.
No.Mimi ninaitwa magoli kwa jina lingine.Lakini bahati mbaya mods walifuta kutokana na sababu zilizonje ya uwezo wao.Kwa hiyo nimerudi na ID nyingine na nimeamua kuwajulisha hili jambo.Wakinifuta tena,basi nita seti mambo mengine kwenye internet.
Nyumbu,
Kila ukiandika hapa kwa kuwa NEUTRAL, wanakuita uko kambi ya Mwakalinga na unaandika KUJIPOZA. Mwakalinga akirudi hapa, kuna moto utawaka maana kuna watu wana ugomvi naye wa siku nyingi na wako tayari hata kusikia Mwakyembe kauwa watu ili ashinde. Hata kama watakuwa wameuawa ndugu zao, watafurahi tu kisa Mwakalinga kashindwa. Sintashangaa wengine walienda hadi kuloga.
Kuna mijitu ni kama Mipare vile. Iko tayari KUUZA ngo'ombe ili ashinde kesi ya KUKU.
Nilikuwa nafikiria achukue fomu za CHADEMA ingawa kwa lengo zaidi ya kusaidia na kulinda kura za Dr. Slaa huko Kyela. Sijui atakuwa na uamuzi gani kwa sasa. Akifanya hivyo basi atakuwa anasaidia zaidi Watanzania na si Kyela peke yake. Na pia hapa Umafia waliomchezea hautakuwepo tena. Ukweli halisi wa KURA utaonekana na hiyo ndiyo itakuwa Final Say. Mtu akitoa HONGO basi afahamu kesi haiendi kwa Makamba ila itakwenda MAHAKAMANI.
KATABAZ: Nakubaliana na maneno yako. Naweza kusema wazi kuwa wewe na Nyumbu kweli mlikuwa Kyela na hawa wengine wote akina Kasyabone, Malafyale, Afande Samuel na wengine wote wanaobishana hapa ni wapiga story za kijiwe na hawako KYELA. Mie nakiri kabisa wala sijafika Kyela. Ila cha kushangaza, pamoja na kuwa hawapo Kyela, wanataka Kutuaminisha habari kama vile walikuwepo. UChaguzi umeisha na Mwakyembe wenu kashinda, KUWENI WAKWELI BASI HATA SIKU MOJA.
Masaiti,
Usinihukumu bure hapa JF ndugu yangu. Nikiandika kuhusu Kyela, ninakuwa kati ya UKWELI na UTANI. Wanyakyusa ni watani wangu na hiyo huwa inanipa eneo kubwa sana la KUJIDAI kila ninapoandika.
Wanakyela wameamua kuchagua UMAARUFU, let it be.
Mkuu,
Tatizo lako unamentality ya Wanyamwezi ya kuwa nyoronyoro/upole usio na tija ambao umefanya RA ameweza kuwarubuni kwa pesa hadi wakamuangusha mpambanaji Selelii badala ya Wanyamwezi hao kuona fahari ya kuwa na Mnyamwezi kama huyo shujaa aliyetetea maslahi ya Taifa wakati wa sakata la Richmonduli! Wanyakyusa hawako hivyo, wakishakudharau basi hata uje na majisenti huambulii kitu midhali wao wameishaamua wanachokitaka. Hili liwe fundisho kwa hata wanasiasa wanaowania urais.
Pia hata kama Mwakalinga atahamia CHADEMA haitamsaidia Dr. Slaa kwa sababu Mwakalinga atakosa. Wanyakyusa walishaamua Mwakyembe wao apite atapita tu.
Wewew lazima unatoka Ileje.....
Kyela sasa ni halmashauri ya mji....hupewi hadhi hiyo bila kufikia vigezo kadhaa......
Kwa maana nyingine, Kyela inafanana na Njombe , Rungwe nk
Ongea kwa point siyo kukurupuka.
.
Katabazi.
Kwa utafiti wako wa harakaharaka, hivi populations ya kyela ni ngapi?.
Kinachonishangaza hapa ni hiyo idadi ya wana ccm waliojitokeza kupiga kura ni 20,000 na je ambao hawakupiga?
Nani aliyekwambia kuwa ukiwa na halmashauri maana yake mmeendelea? Inawezekana Mwakalinga akawa anachangia mapato ya halmashauri kiasi kikubwa sana kuiwezesha ku-qualify kuwa halmashauri huku wengine mkiwa choka mbaya kama hali halisi ilivyo! Ukinisoma vema, nina maana ni muda muafaka kwa wana Kyela sasa kuanza kufikiria maendeleo yenu kama wananchi na si kukimbilia kujenga Mbeya na Dar na mikoa mingine.
Chagueni mada za kuendeleza Kyela na si ubishi wa Mwakalinga, Mwakyembe na wengine....
Mwingine anaongelea mchele,,, du! Hiyo nayo kali zaidi.
Ningemshauri ndugu yangu Mwakalinga asiende CHADEMA maana koti la Rostam na Lowassa atakuwa bado analo, litakuwa kosa kubwa kama CHADEMA watampokea. Chama kinachomfaa ni CUF maana wanaendana sera!