Kweli wazanzibar wanakataa muungano?

WILSON MWIJAGE

JF-Expert Member
May 30, 2011
276
76
Jana (10.11.2011) katika kipindi cha Idhaa ya kiswahili ya BBC jioni kulikuwa na taarifa kwamba Wazanzibar wapatao 30 hivi wamewasilisha barua yao katika ofisi za umoja wa mataifa (Zanzibar) wakitaka Zanzibar kutokuwa katika Muungano na Tanzania Bara (Tanganyika). Katika barua hiyo wanamuomba Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (Mooon) kukubali na baadae kidogo kuitambua Zanzibar kama nchi inayojitegemea.

Hii sio mara ya kwanza kufanya hivyo japo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa huyo alishawakatalia. Sasa wanasema mara hii atumie busara zaidi kwasababu kuna Wazanzibar wengi nyuma yao wanaowaunga mkono.
 
ah waendezao hk kwani wanatusaidia nini? NYERERE ALIUNGANISHA TANGANYIKA NA ZANZIBAR KWA SBB ZA KIUSALAMA si vinginevyo hvy km wameamua tutengane powa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom