Kweli usimdharau mtu.

Wakati naanza maisha kuna jamaa kazini tena juniors kwangu walikua wananitishia maisha sana "nakaa kwangu nimejenga" siku nimewatembelea makwao ndio nikaona haya maisha usijipe pressure zisizo na msingi!
Unakuta mtu nyumba madirisha ameziba mabati makuukuu,chumba chenye mlango ni chake tu,choo mlango gunia,umeme na maji hana uhakika wa kupata leo wala kesho,ila anakutishia kwa vile umepanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yupi,erick au

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo alizingua snaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngoja nijaribu kumtetea mleta maada.
Wakuu, iko hivi watu tunaojuana hua tumezoeana sana ama kidogo. Hivyo basi hua tunaheshimiana kulingana na hadhi zetu katika jamii tunayoishi. Hapa mwenye pesa, cheo, ushawishi (mfano mpigisha stori mzuri kwenye kahawa), taaluma n.k.

Utakuta mzee akisalimiana na kijana mwenye kauwezo flani, anakusanya mikono pamoja kuonyesha heshima wakati huohuo Huyo mzee akisalimiana na mwanae hakusanyi mikono wala kuonyesha unyenyekevu.

Ndugu zetu waliotuzidi umri tunawapa shikamoo, lakini tukikutana na tusiowajua wenye umri sawa na ndg zetu hua tunawaambia, "habari yako n.k"!

Hivyo sio ajabu kuona hatuheshimu tusiowajua (japo wapo wanaoheshimu kila mtu, namimi nimo
) maana hatujui wana nini, cheo, taaluma, hela, n.k.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni levo mkuu.... kwa mtazamo wako ukijilinganisha na ww huyo dogo katusua kukuzidi ww na kibarua chako....lkn kumbuka humu JF akina Gullam wamiliki wa viwanda wamo.....

Laiti angalijua wakati mwingine anajibiwa text na figures kubwa hatari na wakati mwingine anawatukana, we acha tu.... wakivaaga suti huwa wanaona wao ni kila kitu, haki ya nani!
 
Mkuu humo kwenye magodown na maviwanda kuna dili zinapigwa za kufa mtu huwezi jua kuna mmoja ni mfanyakazi wa kawaida kiwanda kimoja kipo mbezi beach ana nyumba 2 za maana ana gari mbili za kutembelea (ila kazini haendi nazo anapanda daladala) anasomesha mtoto shule ya bei m 2 kwa mwaka take home yake ni laki 6 na hajawahi kopa bank can you imagine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…