Secret Star
JF-Expert Member
- Jul 1, 2011
- 1,785
- 1,848
Kama wasomi na "Great Thinkers, sisi ni mabingwa wa kufanya Due Diligence ((upembuzi yakinifu). Ukitaka kununua kiwanja cha milioni tano Chanika, utaenda Wizara ya Ardhi, utaleta mpima ardhi wako, utahoji majirani, na utataka kuona hati halisi. Ukitaka kununua gari used la milioni 15, utaleta mafundi watatu tofauti wapime injini.
Lakini inapokuja kwenye kuingia ubia wa maisha (Ndoa/Mahusiano) na mtu ambaye atadhibiti 50% ya mali zako, asilimia 100 ya amani yako ya akili, na kuwa "Co-founder" wa watoto wakohapo ndipo wasomi tunapoweka akili pembeni na kutumia matope".
Hebu tuangalie makosa yetu ya kiuchambuzi kimkakati:
Nipo hapa kusikiliza mapovu yenu wakuu. Je, ni kweli upendo hauhitaji Risk Assessment? Uwanja ni wenu.
Lakini inapokuja kwenye kuingia ubia wa maisha (Ndoa/Mahusiano) na mtu ambaye atadhibiti 50% ya mali zako, asilimia 100 ya amani yako ya akili, na kuwa "Co-founder" wa watoto wakohapo ndipo wasomi tunapoweka akili pembeni na kutumia matope".
Hebu tuangalie makosa yetu ya kiuchambuzi kimkakati:
- Mchakato Feki wa 'Interview': Kampuni ikitaka kuajiri mtu wa kumlipa laki nane, itapitia CV yake, itampigisha usaili wa mdomo na maandishi, na itampigia simu mwajiri wake wa zamani (Background Check). Lakini msomi akitafuta mwenza, "interview" yake ni kwenda mgahawani, kunywa juisi, kumuuliza "unapenda rangi gani?", na jamaa akijibu kwa sauti ya upole au mdada akiwa na tabasamu zuri—BOOM! Interview imepasiwa. Mwajiri wa zamani (MaEx) hawaulizwi kwanini mkataba ulivunjwa!
- Kupuuza 'Rred Flags' (Auditing Failure): Wewe ni Mhasibu mzuri ofisini. Ukikuta hesabu hazibalansi, unakataa kusaini. Lakini kwenye mahusiano, unaona kabisa mtu ana Liability kubwa (hasira za karibu, mvivu, hajui kutafuta pesa, au anawasiliana na ma-ex wake saba). Badala ya kusitisha mkataba, msomi anasema, "Nitambadilisha kwa upendo wangu." Mkuu, huwezi kubadilisha Balance Sheet mbovu kwa kutumia upendo!
- Hasara ya Mtaji (Initial Investment ROI): Wasomi tuko tayari kuchukua mkopo wa benki kufanya sherehe ya harusi ya Milioni 30 ili kuwafurahisha watu 400 ambao 350 kati yao hata hatuna namba zao za simu. Kwenye uchumi, hii ni sawa na kununua Depreciating Asset kwa mkopo wenye riba kubwa. Siku ya pili baada ya harusi, mnaanza maisha na deni, mkiangaliana usoni huku "Return on Investment" (ROI) ikiwa ni picha za kwenye albamu pekee.
- Falsafa ya "At least ana hofu ya Mungu": Hii ndiyo Business Plan ya wengi. Tunatumia kigezo cha mtu kwenda ibadani kama kigezo cha yeye kuwa mwekezaji mzuri kwenye maisha. Tunasahau kuwa hata watu wanaofilisika kibiashara wana hofu ya Mungu. Kwenye ubia wa maisha, unahitaji mtu mwenye "Hofu ya Umaskini" na "Mikakati ya Kujenga Msingi," sio tu mtu wa ku-quote mistari ya vitabu vitakatifu huku bili ya umeme ikisomwa.
Nipo hapa kusikiliza mapovu yenu wakuu. Je, ni kweli upendo hauhitaji Risk Assessment? Uwanja ni wenu.