GODZILLA
JF-Expert Member
- Dec 26, 2014
- 5,909
- 10,562
Wasalaam...
Mimi ni Kijana wa early 30's, nina urefu saizi ya kati, rangi ya maji ya kunde. Kwa asili mimi ni mtu mkimya SANA.
Nimekuwa niki experience namna ambavyo watu wanajawa hofu wakiwa karibu yangu... aidha watanisalimia kwa woga na kutetemeka, au wataonyesha ishara ya kunyong'onyea.
Watoto wadogo na vijana ndio balaa kabisa, wakiniona wanatetemeka sana huku wananiamkia haraka haraka.
Hii hali inanitesa sana maana hata kazini watu wananiogopa na wakiniona wanajisikia inferior sana. Nikianza kuzungumza kila mtu anaitikia kwa hofu. Wakati mwingine najaribu kukaa mbali na watu ili wasijisikie duni!
Ni nini hiki? Sidhani kama sura yangu inatisha maana mke wangu na baadhi ya wanawake huniambia mimi ni handsome! Kwahiyo naamini sura yangu haitishi!
What is this?
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi ni Kijana wa early 30's, nina urefu saizi ya kati, rangi ya maji ya kunde. Kwa asili mimi ni mtu mkimya SANA.
Nimekuwa niki experience namna ambavyo watu wanajawa hofu wakiwa karibu yangu... aidha watanisalimia kwa woga na kutetemeka, au wataonyesha ishara ya kunyong'onyea.
Watoto wadogo na vijana ndio balaa kabisa, wakiniona wanatetemeka sana huku wananiamkia haraka haraka.
Hii hali inanitesa sana maana hata kazini watu wananiogopa na wakiniona wanajisikia inferior sana. Nikianza kuzungumza kila mtu anaitikia kwa hofu. Wakati mwingine najaribu kukaa mbali na watu ili wasijisikie duni!
Ni nini hiki? Sidhani kama sura yangu inatisha maana mke wangu na baadhi ya wanawake huniambia mimi ni handsome! Kwahiyo naamini sura yangu haitishi!
What is this?
Sent using Jamii Forums mobile app