Mikono yenye Sugu
Senior Member
- Jul 1, 2020
- 133
- 215
Nakipenda chama changu (CCM), lakini kinaniangusha pale tunaposhindwa kuzijibu hoja za wapinzani wetu na badala yake tunawalazimisha kutusifu na kuonesha nyuso za ucheshi, bashasha na tabasamu ilhali mioyo yao inalia.
Nashauri tuzijibu hoja zao bila kejeli, hasira wala kuwatumia vyombo vya mabavu kuwanyamazisha. Naamini majibu tunayo na wenye kutafakari ukweli watatuelewa na kutupokea.
Upinzani sio hatia, usaliti wala dhambi, na kamwe upinzani hautamalizika kwani hata MWENYEZI MUNGU mwenyewe alimwacha shetani awepo ili wasiomkubali yeye nao wawe na kiongozi wao.
Ee chama changu, tusiwe chanzo cha Watanzania kugawanyika bali chanzo cha wao kuwa na mshikamano na umoja wa kitaifa. Hiyo ndio ilikuwa njozi ya Mwalimu Nyerere na wenzake walioliasisi taifa hili.
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE!
Nashauri tuzijibu hoja zao bila kejeli, hasira wala kuwatumia vyombo vya mabavu kuwanyamazisha. Naamini majibu tunayo na wenye kutafakari ukweli watatuelewa na kutupokea.
Upinzani sio hatia, usaliti wala dhambi, na kamwe upinzani hautamalizika kwani hata MWENYEZI MUNGU mwenyewe alimwacha shetani awepo ili wasiomkubali yeye nao wawe na kiongozi wao.
Ee chama changu, tusiwe chanzo cha Watanzania kugawanyika bali chanzo cha wao kuwa na mshikamano na umoja wa kitaifa. Hiyo ndio ilikuwa njozi ya Mwalimu Nyerere na wenzake walioliasisi taifa hili.
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE!