Kwanini wasomi wetu na wanasiasa wanapenda title za elimu yao?

M_kara

JF-Expert Member
Jan 9, 2016
385
293
Mimi ni mtanzania ambaye nina elimu ya kawaida (Degree) toka nje ya nchi, na kwa kiasi kikubwa nimetumia muda mwingi wa maisha yangu kufanya kazi nchi mbali mbali ulaya na amerika.

Nilichokiona katika nchi zetu za kiafrika ni kutukuzana kwa kuitana majina (titles) kulingana na elimu hasa baada ya mtu kutunukiwa degree ya PhD.

Ni jambo la kawaida kabisa kusikia mtu akimwita Dr. X ndani ya bar au hata katika mazingira ya nyumbani. Mtu na mke, au na mdogo wake wanahitana hivyo hivyo.

Hali hii ni ya ajabu zaidi inapotokea kwamba huyo mwenye elimu yenye title ya Dr. au Professor ni mwanasiasa na ni engineer. Kwa maana hiyo jina lake sasa linakuwa 'Mh. Dr. Eng. Msomi' (kwa mfano).

Niwe mkweli kwamba elimu yangu haijafikia level hiyo, lakini kwa uzoefu wangu wa zaidi ya miaka 25 nje ya Tzn sijawhi kusikia watu wa aina hiyo wakiitana majina kulingana na usomi wao.

Cha ajabu, hata hizo tuzo za degree za kupewa (honorary) nao wanajiingiza kwenye upuuzi huu.

Utasikia kwenye kanisa la mama Lwakatare anaibuka mtu anasema "Mh. Mchungaji Dr. Lwakatare".

Kwanini sisi waafrika tunatukuza kitu hiki na hasa wasomi wa leo hii? Mwl. J. K. Nyerere aliweza kutunukiwa degree za honorary nyingi tu, lakini sikuwa kusikia akiitwa Ndg. Dr. Mwl. Nyerere.

Kwa wale wanaojua Rais wa Marekani Baraka Obama msomi wa sheria katika katiba (Professor in Constitutional Law) lakini sijawahi kusikia huko marekani akiitwa President Prof. B. Obama.

Siku zote anaitwa President Obama, na wakati mwingine ni Mr. Baracka Obama. Chancellor wa Ujerumani Angela Merkel ana PhD lakini kama walivyo wengine wengi katika nchi hizo sijawahi kusikia akiitwa Dr. A. Merkel ndani au nje ya bunge la Deutschland.

Sasa hapa kwetu mambo ndo hivo, Mh. Dr. Kikwete, Dr. Magufuli, Mh. Prof. Eng. S. Mhongo!! What's wrong mtu akaitwa tu Manji hapa kwetu Africa? Au wasomi wetu na wanasiasa wetu ni watu special?

Nawasilisha.
 
Kuna kitu kinaitwa ushamba, ndicho kinachowasumbua wasomi wetu. Obama ni profesa lakini huwezi kusikia akijinasibu kwa kutumia elimu yake. Bill Clinton ni profesa wa sheria, lakini huwezi kumsikia akijinasibu kwa sababu ya elimu yake. Kinachokera zaidi ni dharau walizonazo wasomi wetu, ambao baadhi yao hata hizo elimu walizonazo ni matunda ya mfumo wa "kuongea vizuri na waalimu wetu". Ziko zile elimu za underwear, ziko elimu za mtu kuwa mtoto wa baba yake mdogo wa mwalimu wa chuo kikuu.

Unakuta madaktari wetu ambao wanachemsha mara nyingi tu kikazi, na wao wanawaponda kina Mwaka, wakisema kuwa hakuna wanachokijua!!. Kila mtanzania anataka kuringia elimu yake aliyonayo. Lakini ukichunguza sana hakuna kizazi cha mtanzania ambacho miaka zaidi ya 100 iliyopita kilikuwa na mtu mwenye shahada angalau moja. Kina Issac Newton wamesoma karne nyingi zilizopita lakini huwezi kuwasikia wazungu wakijisifu kwa kutumia elimu. Waliosoma kwa miaka zaidi ya 300 iliyopita wala hawana mbwembwe za kutambia elimu, sisi ambao bado tunaendelea kujenga vyuo vikuu, kila kukicha mbwembwe mdomoni!!.
 
Elimu yetu ngumu sana na ina changamoto nyingi sana kwa sisi watoto wa masikini sasa tukitusua lazima tuonyeshe manjonjo yetu kuna msemo unasema maskini akipata makalio ulia mbwata
 
Mimi ni mtanzania ambaye nina elimu ya kawaida (Degree) toka nje ya nchi, na kwa kiasi kikubwa nimetumia muda mwingi wa maisha yangu kufanya kazi nchi mbali mbali ulaya na amerika.

Nilichokiona katika nchi zetu za kiafrika ni kutukuzana kwa kuitana majina (titles) kulingana na elimu hasa baada ya mtu kutunukiwa degree ya PhD.

Ni jambo la kawaida kabisa kusikia mtu akimwita Dr. X ndani ya bar au hata katika mazingira ya nyumbani. Mtu na mke, au na mdogo wake wanahitana hivyo hivyo.

Hali hii ni ya ajabu zaidi inapotokea kwamba huyo mwenye elimu yenye title ya Dr. au Professor ni mwanasiasa na ni engineer. Kwa maana hiyo jina lake sasa linakuwa 'Mh. Dr. Eng. Msomi' (kwa mfano).

Niwe mkweli kwamba elimu yangu haijafikia level hiyo, lakini kwa uzoefu wangu wa zaidi ya miaka 25 nje ya Tzn sijawhi kusikia watu wa aina hiyo wakiitana majina kulingana na usomi wao.

Cha ajabu, hata hizo tuzo za degree za kupewa (honorary) nao wanajiingiza kwenye upuuzi huu.

Utasikia kwenye kanisa la mama Lwakatare anaibuka mtu anasema "Mh. Mchungaji Dr. Lwakatare".

Kwanini sisi waafrika tunatukuza kitu hiki na hasa wasomi wa leo hii? Mwl. J. K. Nyerere aliweza kutunukiwa degree za honorary nyingi tu, lakini sikuwa kusikia akiitwa Ndg. Dr. Mwl. Nyerere.

Kwa wale wanaojua Rais wa Marekani Baraka Obama msomi wa sheria katika katiba (Professor in Constitutional Law) lakini sijawahi kusikia huko marekani akiitwa President Prof. B. Obama.

Siku zote anaitwa President Obama, na wakati mwingine ni Mr. Baracka Obama. Chancellor wa Ujerumani Angela Merkel ana PhD lakini kama walivyo wengine wengi katika nchi hizo sijawahi kusikia akiitwa Dr. A. Merkel ndani au nje ya bunge la Deutschland.

Sasa hapa kwetu mambo ndo hivo, Mh. Dr. Kikwete, Dr. Magufuli, Mh. Prof. Eng. S. Mhongo!! What's wrong mtu akaitwa tu Manji hapa kwetu Africa? Au wasomi wetu na wanasiasa wetu ni watu special?

Nawasilisha.
Ahsant Mkuu kwa Taarifa nilikuwa sijui kama hao uliowataja Clinton,Obama,Merkel kama ni Phd's...
Ni bora hata kuitana Dr...Prof..
Lakini sisi tumezidi utasikia Mtu na Kadegree kake kamoja utasikia Eng. Kimbori.....Advocate Saguda...Itabidi na watu wa Fani nyingine watafute Titles sasa/Utambulisho...Mfano HR.Igobe....IT.Seke....,Envir.Boko...,Accont...Jube...Mrk.Soni....nk
SIJUI IPIGWE MARUFUKU...AU TUACHE KAMA ILIVYO...AU TUPITISHE SHERIA...AU ULIMBUKENI....
 
Kutojiamini na kuwa na inferiority complex inafanya watu wa TZ tuwe na kujitangaza usomi wakati ukianza kuongeleshwa ulichokisoma unakuja na misemo ya changamoto, mikakati, mipasho nk. Nchi hii include me wote vilaza hatujasoma sababu hata tunayotenda aibu. Nchi nzima kuhamia kwa babu wa Loliondo kweli tulitoa taswira gani kwa nchi za nje na je madaktari wetu walijisikiaje???? Nchi hii msomi ni Prof. Maji marefu tu basi plus babu aliyeamua kukaa kimya baada ya kulamba mia tano mara millioni. Mtajiju.
 
Mimi ni mtanzania ambaye nina elimu ya kawaida (Degree) toka nje ya nchi, na kwa kiasi kikubwa nimetumia muda mwingi wa maisha yangu kufanya kazi nchi mbali mbali ulaya na amerika.

Nilichokiona katika nchi zetu za kiafrika ni kutukuzana kwa kuitana majina (titles) kulingana na elimu hasa baada ya mtu kutunukiwa degree ya PhD.

Ni jambo la kawaida kabisa kusikia mtu akimwita Dr. X ndani ya bar au hata katika mazingira ya nyumbani. Mtu na mke, au na mdogo wake wanahitana hivyo hivyo.

Hali hii ni ya ajabu zaidi inapotokea kwamba huyo mwenye elimu yenye title ya Dr. au Professor ni mwanasiasa na ni engineer. Kwa maana hiyo jina lake sasa linakuwa 'Mh. Dr. Eng. Msomi' (kwa mfano).

Niwe mkweli kwamba elimu yangu haijafikia level hiyo, lakini kwa uzoefu wangu wa zaidi ya miaka 25 nje ya Tzn sijawhi kusikia watu wa aina hiyo wakiitana majina kulingana na usomi wao.

Cha ajabu, hata hizo tuzo za degree za kupewa (honorary) nao wanajiingiza kwenye upuuzi huu.

Utasikia kwenye kanisa la mama Lwakatare anaibuka mtu anasema "Mh. Mchungaji Dr. Lwakatare".

Kwanini sisi waafrika tunatukuza kitu hiki na hasa wasomi wa leo hii? Mwl. J. K. Nyerere aliweza kutunukiwa degree za honorary nyingi tu, lakini sikuwa kusikia akiitwa Ndg. Dr. Mwl. Nyerere.

Kwa wale wanaojua Rais wa Marekani Baraka Obama msomi wa sheria katika katiba (Professor in Constitutional Law) lakini sijawahi kusikia huko marekani akiitwa President Prof. B. Obama.

Siku zote anaitwa President Obama, na wakati mwingine ni Mr. Baracka Obama. Chancellor wa Ujerumani Angela Merkel ana PhD lakini kama walivyo wengine wengi katika nchi hizo sijawahi kusikia akiitwa Dr. A. Merkel ndani au nje ya bunge la Deutschland.

Sasa hapa kwetu mambo ndo hivo, Mh. Dr. Kikwete, Dr. Magufuli, Mh. Prof. Eng. S. Mhongo!! What's wrong mtu akaitwa tu Manji hapa kwetu Africa? Au wasomi wetu na wanasiasa wetu ni watu special?

Nawasilisha.
they have nothing to show up zaidi ya hizo title zao. wangekuwa na cha kuonyesha jamii wasingekuwa na haja ya kuonyesha hizo title zao kwa jamii.
 
Huu ugonjwa tumeambukizwa na wale jamaa wa Ibadan. Manake kwao wao: "my broder, if you don't have a title you are a nobody-o!". Unakuta mtu mmoja anapigwa intro "Alhaji, Hon. Prince, Dr. Eng. ...". Enzi zetu shuleni tulikuwa tunashangaa jina la mtu kufanywa komedi na kuwaona washamba sana. Lakini leo hii tunawaiga kila ujinga wanaofanya.

Kuna ndugu yangu kasoma PhD ya "mtandao" usipomuita profesa hata katika mazungumzo ya kifamilia tu hakuelewi kabisa na kikao kinaishia hapo. Anadai kasota sana kuipata hiyo kitu ukubwani hivyo tusimfanyie mchezo!
 
kuna suala la utamaduni. Watanzania si watu pekee wanaopenda ama kutambulika kwa hierarchical order au kwa kiwango cha elimu walichofikia. ni chi nyingi Afrika na hata Asia wako hivyo. Katika masula ya international business hasa mnapokuwa mnafanya business meeting na watu wa culture tofauti hilo ni jambo la kuzingatia MNO wakati una adress watu .Kuna baadhi ya tamafuni mf. Wachina hupenda kutambulika kwa hierarchy zao yaani kama yeye ni mkurugenzi basi unapomtaja umtaje kwa cheo chake ili kumtofautisha na wengine na pia kama mtu ni Phd holder au ni Prof basi umtaje hivyo. Tamaduni huenda mbali zaidi kuna baadhi hutajwa kwa kuanza na surname(jina la ukoo) kisha ndio majina mengi. Haya yote ni mambo unayotakiwa kujifunza katika business culture ikiwa unafanya international consultancy/business. Hivyo ulaya na marekani isiwe ndio kigezo rejea (ref.point) kwa kila kitu. Utamaduni wa magharibi hauwezi kuwa sawa na wa Asia na hata Afrika. Na hata ndani ya Afrika yenyewe utamaduni wa Afrika mashariki mashariki hauwezi kuwa sawa na wa magharibi kwa mfano wakati sehemu za pwani ya Tanzania kiutamaduni watu hawanyimani maji ya kunywa mfano mikoa kama Tanga, Zanzibar,kilwa ,lindi na bagamoyo , huu ni utamaduni wa Afrika mashariki lakini Afrika magharibi katika Jamhuri ya kiislamu ya Mauritania kiutamaduni wao si tu hawanyimani MAZIWA lakini pia HAWAMUUZII MTU MAZIWA ikiwa ameomba kama ambavyo mtu wa pwani ya Tanzania aombavyo maji.
Kwa hiyo mimi naweza kuhitimisha kuwa hiyo ni desturi yetu watanzania na ni sehemu ya utamaduni wetu kuwa na watu hupenda kutajwa kwa nafasi zao au elimu zao, SIONI UBAYA wa hilo na tusilazimishe tufanane na ulaya na marekani kwa kila kitu.
 
Back
Top Bottom