Kwanini wanaume mnawaharibu watoto

Kwanini wanaume mnawaharibu watoto

kriche

New Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
3
Reaction score
2
Hivi inakuaje unaweka kabisa dhamira na kuitekeleza ili tu utimize haja zako huku ukimuachia mtoto kovu lisilofutika kabisa katika maisha yake hapa duniani?

Cha ajabu mmekuwa mkijinasibu kuwa na utaalamu mkubwa wa kuchakata wanawake. Hili mnalikiri hadharani. Ila kwa vitendo vinavyojitokeza inadhihirisha kabisa mnajinasibu pia kivitendo. Kwa nini muwaharibu watoto?

Tuwafiche wapi watoto? Na bahati mbaya zaidi viongozi wa dini wanafanya haya mambo, matajiri, wafanyabiashara, walimu ndo kabisaaa, waliooa na wanunua ngono pia!

Waoneeni huruma hawa watoto wana ndoto zao. Hebu fikiria ungekumbwa na maswahiba kama hayo leo hii ungekuwa katika hali gani?

Inaanza na wewe, Badili Fikra, Tanguliza Utu kwa watoto! Tuwapende
 
Back
Top Bottom