Kwanini wanaopinga utumbuaji majipu si katika wale waliotumbuliwa?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,895
20,392
Wadau, amani iwe kwenu.

Tangu zoezi la utumbuaji majipu lilipoanza, tumeshuhudia watu kadhaa wakijitokeza na kupinga zoezi hilo. Mtu wa kwanza kulalamika ni aliyekuwa mgombea Urais wa CHADEMA na UKAWA kwenye uchaguzi wa Oktoba 2015, Edward Lowasa ambaye kwa upande wake alisema kuwa Rais Magufuli anawatumbua watu kwa itikadi za kisiasa kwa hisia kuwa waliunga mkono upinzani. Pia alisema kuwa Rais anatumbua watu ambao hakuwateua yeye na ndo maana hana huruma nao.

Mtu wa pili kupinga utumbuaji huo ni Freeman Aikael Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na Mbunge wa jimbo la Hai. Mbowe alitokwa na povu jingi kwa kusema kuwa utumbuaji huo haufuati katiba na sheria hasa haki ya kusikilizwa.

Baada ya makamanda hao wawili kuongea, tukaanza kusikia kelele nyingi kutoka kwa vibaraka wao wakiwemo wanaojifanya watetezi wa haki za binadamu. Pia kelele hizo tumeanza kuziona humu mitandaoni. Binafsi nimejiuliza sana. Hii huruma ya CHADEMA kwa wanaotumbuliwa imeanza lini? Nini maslahi yao kwa wanaotumbuliwa majipu? Je utumbuaji huu wa majipu unahatarisha nini kwa ustawi wa CHADEMA na UKAWA?

Swali kubwa zaidi ambalo limenifanya nije mbio kuomba ushauri kwa wadau ni hili. kama utumbuaji majipu unafanyika bila kufuata Katiba, Sheria na Kanuni, KWA NINI MPAKA SASA WANAOLALAMIKA NA KUPINGA UTUMBUAJI MAJIPU SI MIONGONI MWA WANAOTUMBULIWA? kuna nini hapa? Mpaka sasa hakuna hata mmoja aliyejitokeza hadharani kupinga kutumbuliwa kwake. Kama katiba na sheria zinakiukwa kama anavyosema Mbowe, iweje sasa hao wanaotumbuliwa hawataki kwenda Mahakamani kudai haki yao? Kuna nini hapa?
 
Mbona aliyenunua meli Chakavu, kuuza nyumba za serikali, kusababisha hasara kwa serikali kwa kulipa fidia wavuvi wa kigeni, kuhamisha mafungu ya fedha za serikali kinyume cha Sheria, bado hajatumbuliwa?
Bado na wewe unaendelea kuimba wimbo wa Mbowe. Kama mnaona kuwa sheria hazifuatwi, kwa nini hamkimbilii mahakamani kama mnavyofanyaga kwenye masuala mengine? Naona bado un aendelea kuzua maswali ambao hamuwezi kuyajibu
 
Bado na wewe unaendelea kuimba wimbo wa Mbowe. Kama mnaona kuwa sheria hazifuatwi, kwa nini hamkimbilii mahakamani kama mnavyofanyaga kwenye masuala mengine? Naona bado un aendelea kuzua maswali ambao hamuwezi kuyajibu
Kwa hiyo sheria zinavunjwa makusudi ili baadae Mahakama isaidie kuhalalisha. Sasa napata picha kwa nini, DPP na mawakili wa Serikali wanalazimishwa kushinda kesi.
 
Tuanzie hapo huenda utaanza kuelewa na utapata majibu ya maswali yako,kama bado niite nitarudi kukupa jingine.
 
Waliotumbuliwa nanajua kabisa kuwa walikosea ndomana hawana jinsi na hao wanaowasemea wanauchungu saana kwa kuwa ndo walikua vibaraka wao ndani ya utumishi waliwekwa kwa maslahi ya hao watetezi
Haiingii akilini uyasemee majibu kama sio mmoja wa washirika wao
 
Tuanzie hapo huenda utaanza kuelewa na utapata majibu ya maswali yako,kama bado niite nitarudi kukupa jingine.
Najua uwezo wako ni mdogo kuweza kujibu haya ama unafahamu ila unataka kuficha ukweli na hivyo kuungana na akina Mbowe. Huna msaada kwenye uzi huu
 
Waliotumbuliwa nanajua kabisa kuwa walikosea ndomana hawana jinsi na hao wanaowasemea wanauchungu saana kwa kuwa ndo walikua vibaraka wao ndani ya utumishi waliwekwa kwa maslahi ya hao watetezi
Haiingii akilini uyasemee majibu kama sio mmoja wa washirika wao
Sasa naanza kuelewa kwa nini walioanza kupiga kelele ni Mbowe na Lowasa. Ahsante sana Mkuu
 
Najua uwezo wako ni mdogo kuweza kujibu haya ama unafahamu ila unataka kuficha ukweli na hivyo kuungana na akina Mbowe. Huna msaada kwenye uzi huu
Huenda hujanielewa mkuu,wait,nilimaanisha hiki hapa
 

Attachments

  • 1462178432834.jpg
    1462178432834.jpg
    34.1 KB · Views: 49
Bado na wewe unaendelea kuimba wimbo wa Mbowe. Kama mnaona kuwa sheria hazifuatwi, kwa nini hamkimbilii mahakamani kama mnavyofanyaga kwenye masuala mengine? Naona bado un aendelea kuzua maswali ambao hamuwezi kuyajibu
vidagaa.

swissme
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Tangu zoezi la utumbuaji majipu lilipoanza, tumeshuhudia watu kadhaa wakijitokeza na kupinga zoezi hilo. Mtu wa kwanza kulalamika ni aliyekuwa mgombea Urais wa CHADEMA na UKAWA kwenye uchaguzi wa Oktoba 2015, Edward Lowasa ambaye kwa upande wake alisema kuwa Rais Magufuli anawatumbua watu kwa itikadi za kisiasa kwa hisia kuwa waliunga mkono upinzani. Pia alisema kuwa Rais anatumbua watu ambao hakuwateua yeye na ndo maana hana huruma nao.

Mtu wa pili kupinga utumbuaji huo ni Freeman Aikael Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na Mbunge wa jimbo la Hai. Mbowe alitokwa na povu jingi kwa kusema kuwa utumbuaji huo haufuati katiba na sheria hasa haki ya kusikilizwa.

Baada ya makamanda hao wawili kuongea, tukaanza kusikia kelele nyingi kutoka kwa vibaraka wao wakiwemo wanaojifanya watetezi wa haki za binadamu. Pia kelele hizo tumeanza kuziona humu mitandaoni. Binafsi nimejiuliza sana. Hii huruma ya CHADEMA kwa wanaotumbuliwa imeanza lini? Nini maslahi yao kwa wanaotumbuliwa majipu? Je utumbuaji huu wa majipu unahatarisha nini kwa ustawi wa CHADEMA na UKAWA?

Swali kubwa zaidi ambalo limenifanya nije mbio kuomba ushauri kwa wadau ni hili. kama utumbuaji majipu unafanyika bila kufuata Katiba, Sheria na Kanuni, KWA NINI MPAKA SASA WANAOLALAMIKA NA KUPINGA UTUMBUAJI MAJIPU SI MIONGONI MWA WANAOTUMBULIWA? kuna nini hapa? Mpaka sasa hakuna hata mmoja aliyejitokeza hadharani kupinga kutumbuliwa kwake. Kama katiba na sheria zinakiukwa kama anavyosema Mbowe, iweje sasa hao wanaotumbuliwa hawataki kwenda Mahakamani kudai haki yao? Kuna nini hapa?
Vipi Chenge wa Escrow na Rada akapewa na Uenyekiti wa Bunge.

Mhongo wa Escrow nae akapewa Uwaziri.

CCM kuna Kansa ya Rushwa na Ufisadi.
 
Waliotumbuliwa nanajua kabisa kuwa walikosea ndomana hawana jinsi na hao wanaowasemea wanauchungu saana kwa kuwa ndo walikua vibaraka wao ndani ya utumishi waliwekwa kwa maslahi ya hao watetezi
Haiingii akilini uyasemee majibu kama sio mmoja wa washirika wao
Sahihi kabisa mkuu lazima wezi walindane na kuteteana lakini watanyooka tu kwa magufuli.
 
Kwa usawa huu wa magufuli ukawa watasota sana majipu lazima yatumbuliwe tena kwa kasi tu hakuna kucheka na wezi.
Tusicheke nao kabisa kuanzia kwenye Meli Chakavu, Nyumba za Serikali, Richmond-Dowans, Escrow, Epa, Matumizi mabovu ya fedha Wizara ya Ujenzi kwa mujibu wa ripoti ya CAG, Hasara kwenye Fidia ya Meli ya Samaki.
 
Tatizo kubwa ni kwamba vijana wengi waliojiita wanamabadiliko ndilo lilikuwa genge la wizi na wakwepa kodi.

Wengi walikuwa wakiishi kwa kufadhiliwa na mafisadi,kundi hili linajumuisha wanahabari makanjanja ambao wapo kwenye payroll za mafisadi.
 
Bado na wewe unaendelea kuimba wimbo wa Mbowe. Kama mnaona kuwa sheria hazifuatwi, kwa nini hamkimbilii mahakamani kama mnavyofanyaga kwenye masuala mengine? Naona bado un aendelea kuzua maswali ambao hamuwezi kuyajibu
Takukuru yenyewe imesema mahakamani hamna haki, Rais mwenyewe amekiri. Naona wewe una mtazamo tofauti.
 
Kama hukumu ya kwa Mungu, kila nafsi inajua idadi ya dhambi zake, kipimo sahihi cha maovu siku zote si mahakama wala polisi bali nafsi yako mwenyewe. Wenye akili wameshaona zamu zao zinakuja wanajaribu kujihami. Usikate tamaa ya kujilinda na kujihami mpaka uone kama hakuna uwezekano kabisa, la sivyo pigana ujiokoe.
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Kama hukumu ya kwa Mungu, kila nafsi inajua idadi ya dhambi zake, kipimo sahihi cha maovu siku zote si mahakama wala polisi bali nafsi yako mwenyewe. Wenye akili wameshaona zamu zao zinakuja wanajaribu kujihami. Usikate tamaa ya kujilinda na kujihami mpaka uone kama hakuna uwezekano kabisa, la sivyo pigana ujiokoe.
kwikwikwikwikwikwiiiii. Kwa hiyo zamu ya Lowasa na Mbowe imo mbioni ama siyo?
 
Kama hukumu ya kwa Mungu, kila nafsi inajua idadi ya dhambi zake, kipimo sahihi cha maovu siku zote si mahakama wala polisi bali nafsi yako mwenyewe. Wenye akili wameshaona zamu zao zinakuja wanajaribu kujihami. Usikate tamaa ya kujilinda na kujihami mpaka uone kama hakuna uwezekano kabisa, la sivyo pigana ujiokoe.
kwikwikwikwikwikwiiiii. Kwa hiyo zamu ya Lowasa na Mbowe imo mbioni ama siyo?
 
Back
Top Bottom