Kwanini wa Kigoma wanasumbuliwa kupata Passport?

Kwanini wa Kigoma wanasumbuliwa kupata Passport?

chankele kigoma

Senior Member
Joined
Jan 12, 2017
Posts
199
Reaction score
121
Habari zenu bandugu, Hivi kwanini sisi watu wa kigoma tuna nyanyapaliwa sana na maafsa uhamiaji pale tunapo kwenda katika office zao ?

Ukienda kuomba hati ya kusafiri (passport) ukataja wewe ni from kigoma mara utasikia mkimbizi wewe, ukiwa na passport ukiwa unatoka nje ya mpaka ukitoa tu hati hiyo ukaonekana from KIGOMA utaulizwa mwaswali mengi ikiwemo mpaka ulivo ipata hati hiyo

Sasa najiuliza kwa nini iwe kwa wazawa wa kigoma? Tanzani inamikoa mingi iliyo mipakani lakin watu wake unyanyapaaji huo hauwahusu hata ukiwa naye utasumbuliwa wewe yeye aka.

Sasa naomba kuelezwa nikwanini hii hali au kuna siri gani imejificha katika mkoa wa kigoma mpaka sisi tunaozaliwa huko tunajikuta tuananyanyasika kisa tumezaliwa KIGOMA inawezekana kuna historia siijui hivo naomba kwa mwenyekulijuwa hili anijuze ili kama kigoma haiko Tanzania basi nijuzwe mimi ni raia wa nchi gani

Tena napenda kama wahusika wapo mnipe ufafanuzi kwa hilo

Karibuni sana
 
Kuna wakimbizi wazamiaji sana kigoma kuliko mikoa yyte Tanzania
 
Haf mnanifanyaga mna swaga za kikongo sana nyinyi.. kifupi mnazipenda nchi jirani kuliko Tz acha tu uhamiaji wa deal na nyinyi perpendicular
 
Sasa kama hawana imani na mkoa wa kigoma basi serikali iufute mkoa wa kigoma lijulikane moja ili tujitawale tukitaka kuingia mikoa mingine tujitambulishe kama wananchi wa kigoma.
Mpaka inakela sana
 
Tatizo mmechanganyikana sana na Warundi hadi inakua tabu kuwatofautisha.
 
Habari zenu bandugu, Hivi kwanini sisi watu wa kigoma tuna nyanyapaliwa sana na maafsa uhamiaji pale tunapo kwenda katika office zao ?

Ukienda kuomba hati ya kusafiri (passport) ukataja wewe ni from kigoma mara utasikia mkimbizi wewe, ukiwa na passport ukiwa unatoka nje ya mpaka ukitoa tu hati hiyo ukaonekana from KIGOMA utaulizwa mwaswali mengi ikiwemo mpaka ulivo ipata hati hiyo

Sasa najiuliza kwa nini iwe kwa wazawa wa kigoma? Tanzani inamikoa mingi iliyo mipakani lakin watu wake unyanyapaaji huo hauwahusu hata ukiwa naye utasumbuliwa wewe yeye aka.

Sasa naomba kuelezwa nikwanini hii hali au kuna siri gani imejificha katika mkoa wa kigoma mpaka sisi tunaozaliwa huko tunajikuta tuananyanyasika kisa tumezaliwa KIGOMA inawezekana kuna historia siijui hivo naomba kwa mwenyekulijuwa hili anijuze ili kama kigoma haiko Tanzania basi nijuzwe mimi ni raia wa nchi gani

Tena napenda kama wahusika wapo mnipe ufafanuzi kwa hilo

Karibuni sana
Mkuu cyo hilo tuu hata ujenzi wa rami kutoka nyakanazi kigoma unasuasua na hakuna hata mkandarasi mmoja alotikiswa au kufukizwa kazi kama kwingine mpaka nafikiri kampuni inayojenga ni ya mtumbuaji ambaye hawezi kujitumbua mwenyewe
 
chankele kigoma ,
Mkuu,
Tatizo lenu ni moja tu mnawaficha wahamiaji halamu kutoka Burundi, Rwanda na Congo.

Mfano, ukienda Mbeya wanakutajia wahamiaji wote kutoka Zambia, Malawi, na wageni wengine wote.

Pia ninyi Kigoma mnajiona kuwa ni wanyaru, warundi au wakongo kuliko kuwa watanzania.

Mfano, ni rahisi Sana kigoma kumsaidia mrundi au mnyaru kuliko watanzania ambao ni kabila kama za wachaga au wasambaa, wajita n.k.n.k. Hii nimeiona sana nikiwa kigoma miaka ya 79 hadi 82.
 
Usiogope kuhojiwa kijana, kigoma Kuna wahamiaji wengi sana, Ukiona unahojiwa sana tambua kuwa Kuna kitu wanatafuta especially kwny matamshi yako.

Mfano watu wa DRC, BURUNDI au Rwanda Badala ya kusema mtu wao hutamka mutu, hata km awe ameishi Tanzania kwa miaka mingi.

Tofauti ya accent huwa ni rahisi kumgundua asie mzaliwa wa Tanzania
 
chankele kigoma ,
Mkuu,
Tatizo lenu ni moja tu mnawaficha wahamiaji halamu kutoka Burundi, Rwanda na Congo.

Mfano, ukienda Mbeya wanakutajia wahamiaji wote kutoka Zambia, Malawi, na wageni wengine wote.

Pia ninyi Kigoma mnajiona kuwa ni wanyaru, warundi au wakongo kuliko kuwa watanzania.

Mfano, ni rahisi Sana kigoma kumsaidia mrundi au mnyaru kuliko watanzania ambao ni kabila kama za wachaga au wasambaa, wajita n.k.n.k. Hii nimeiona sana nikiwa kigoma miaka ya 79 hadi 82.
Sasa kama inatambulikackuwa kuna wahamiaji haram kwanini operation kimbunga ilikuja fanyika mikoa mingine na kigoma haija guswa? Nakuhusu kuwaficha wahamiaji siyo kweli sema mamlaka husika wanalao.

Ipo siku nita mpa viganja afisa uhamiaji siku akiniletea zakuletwa itakuwa fundisho
 
Mzee Magu uko wapi mbona unatuacha wakigoma tunyanyasike tafadhari chukuwa hatua wakigoma tunasumbuliwa sana tukifikia hatua hiyo ya kutafuta paspoti
 
Usiogope kuhojiwa kijana, kigoma Kuna wahamiaji wengi sana, Ukiona unahojiwa sana tambua kuwa Kuna kitu wanatafuta especially kwny matamshi yako.

Mfano watu wa DRC, BURUNDI au Rwanda Badala ya kusema mtu wao hutamka mutu, hata km awe ameishi Tanzania kwa miaka mingi.

Tofauti ya accent huwa ni rahisi kumgundua asie mzaliwa wa Tanzania
Tatizo siyo kuhojiwa tatizo huja pale ukitaja unatoka kigoma utasikia mjinga anaropoka "wemkimbizi" kaapale kwanza tukuitie mtu wa kukuhojibasi inanikera sana na kuniachia maswali mengi kwani kigoma ni nchi au ule mkoa hauko Tz ?
 
Back
Top Bottom