Nalisema hili kwa sababu kipindi hiki ni kipindi cha kuelekea kwenye chaguzi vyama visije vikawa kama kokoro la kubebea wazuri na wabaya.Malengo ya wengi wanaojiunga na upinzani muda huu hayaeleweki,inawezekana ni kusaka vyeo baada ya kuvikosa walikotoka,pia inawezekana ni kupeleleza mbinu na mipango ya vyama husika,kufanya ujasiria siasa kwa maslahi.Hisia zangu kutokana na historia zinanipelekea kuamini kwamba wengi wana nia ovu.Furaha yangu ni kuona nguvu za utawala na upinzani ziko sawa kwa maendeleo,uwazi na haki.Binafsi najiita mdau wa siasa kwa sababu naifuatilia japo nayaona mapungufu mengi sana kwenye vyama ambayo hayarekebishiki kwa sasa labda hapo baadae hivyo sipendi kuumiza kichwa,kwa sasa ni muumini wa dini na sio hiki kinachoitwa sihasa.