Kwanini tunashusha bendera yetu ya Taifa?

hapa nimekuelewa sana kaka
 
Mtoa mada
Kwanza nikupe historia fupi kuhusu bendera.
Matumizi ya bendera yalianza miaka mingi huko nyuma hasa kwenye mapambano na mapigano ya kivita.
Nchi nyingi zilianza kutumia bendera katika karne ya kumi na nane.
Aina ya bendera,namna ya kuipandisha na kuihifadhi inaongozwa ni swala la kiprotokali zaidi.
Zipo protokali ambazo nchi zote zinafuata.
1. Bendera kuwa na umbo la mstatiri
2. Nguzo ya bendera kuwa wima
3. Heshima na matumizi stahiki ya bendera

Kuna mengi ila kwa sababu ya muda nitamalizia mengine nikifika ofisini.
Tuje kwenye swali
Bendera Za taifa zina mambo makubwa mawili
1. kuonyesha uhuru wa nchi na utambulisho wake.Ukiwa UN hutakuta bendera ya Zanzibar kwa kuwa UN haiitambui Zanzibar kama nchi.
2. kuonyesha mamlaka
Kupandisha bendera asubuhi na kuishusha jioni inafanywa hivi kwa mazoea ambayo nchi nyingi imekuwa nazo.
Bendera kwa kuwa ni alama inapaswa kuwekwa mahali ambapo itaoneka na muda ambao itaonekana.
Hivyo nchi nyingi hazipeperushi bendera usiku kwa sababu ya giza. Mfano India pia wanashusha bendera usiku.
Mfano Marekani wao kama bendera inapepea usiku basi hilo eneo lazima liwe na mwanga wa kuifanya bendera hiyo ionekane la sivyo lazima ishushwe. Kwa waliofika Marekani watakubaliana na mimi hapa.


Note. BENDERA kushushwa usiku haina uhusiano wowote na mamlaka ya Rais wala Jeshi la Ulinzi ni utaratibu wa kiprotokali usioathiri nguvu wala majukumu ya Rais ama taasisi yoyote ya Serikali.

Nitarudi baadaye.
 
je kwani bendela za mataifa mengine zenyewe hazishushwi ikifika saa 12:00 jioni? naomba msaada wakuu
 
Huyo anae sema kuwa usiku bendera za jeshi ndio zinasimama anatumia katiba ipi ya nchi ama analeta maneno ya vijiwe vya kahawa humu jukwaani? Acheni maneno ya vijiweni tujikite kwenye fact
katiba haitoi utaratibu, naona watu wengi hawajua nini maana ya katiba, wakizani kila kitu kimeandikwa kwenye katiba, pia hawajui tofauti ya katiba na sheria nyingine, ndiyo maana hata wakati wa kutoa maoni ya katiba mpya kila mtu alisema la kwake akidhani katiba inaandika kila kitu. kuna vitu vingine vingi haviandikwi kwenye katiba, na katiba ingekuwa inaandika kila kitu sijui ingekuwa na ukubwa gani
WHY "ARE YOU"........
...thank you, writing under pressure
 
Hivi maana ya Amiri Jeshi ni nini? Hasa neno Amiri lina maana gani?

Watu humu ndani wachache wanaokubali kukosolewa, tulishasema humu neno Amiri ndiyo UKUU wenyewe kwa hiyo si sahihi kusema 'amiri jeshi mkuu' bali inatosha tu kusema AMIRI JESHI.
 
Jibu sahihi kabisa

 
ccm na chadema pia wanashusha bendera zao jioni,mabalozi nao wanapandisha bendera zao ndani ya nchi yetu,bendeea ya raisi ipo ikulu tu au pale anapokuwepo na sio kila mahali.

huenda bendera ikawa ni utambulisho wa uwepo wa kitu na sio mamlaka ya raisi,ccm,chqdema au jwtz
 

Maelezo mazuri ingawa kuna exception mahali. Bendera ya Nepal haiko katika umbo la mstatili. Sijui Wanepal walifikiria nini?! li mradi tu wawe tofauti na wengine duniani.
 

Kwani Dunia ya leo haina giza?. Hata USA hushusha bendera yao sehem isiyo na mwanga wa kuwezesha kuona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…