Mapato ya Tanzania kwenye sekta ya utalii kwa mwaka ni U$2.9 billion. Mapato ya utalii ya jiji la Paris (siyo France) ni U$89 billion. Bado na wewe unaona una nafasi kubwa kwenye utalii wa Dunia?.
Hivi kujengwa kwa bwawa la umeme au kutojengwa, kuna athari gani kwa mataifa makubwa?
Tusiwe wendawazimu wa kuyahusisha mataifa makubwa kwa hata mambo yetu ya kipuuzi. Kuna watu hata familia zao zikikosa mlo wa jioni, wanatoa sababu ni kwa sababu ya mabeberu. Uwendawazimu mkubwa!
Mataifa makubwa yana shida gani na viwanda vya Tanzania, nchi ambayo haichangii hata 1% ya manunuzi toka nchi za magharibi? Ni argument ya kijinga kabisa kuwa eti ujenzi wa bwawa la umeme la Tanzania unapigwa vita na mataifa makubwa kwa sababu nchi itakuwa na viwanda vingi. Hoja ya mataifa makubwa ilikuwa ni sustainability ya hifadhi ya wanyama - hifadhi ambayo bajeti ya utunzaji wake inayategemea mataifa makubwa.
Umeme ni ingridient ya ujenzi wa vuwanda lakini siyo kisababishi. Tunaweza kuwa na hilo bwawa na wala lisiongeze idadi ya viwanda kama mazingira yaliyopo sasa yataendelea kuwepo kama yalivyo leo.
Nimewahi kushiriki katika kuandaa vigezo vya mazingira ya uwekezaji kwa multinational investing companies. Umeme haupo. Mambo yale ya muhimu kabisa, Tanzania kwa sasa ina rank very low. CONFIDENCE is no. 1. Hakuna investor ambaye ataenda kuwekeza katika nchi ambayo mambo mengi yanategemea kauli ya mtu badala ya sheria